Nyalandu: Nilikuwa msaidizi wa mama Mkapa kwahiyo nilisafiri sana huko duniani na Rais Mkapa!

Nyalandu: Nilikuwa msaidizi wa mama Mkapa kwahiyo nilisafiri sana huko duniani na Rais Mkapa!

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Mtia nia ya Urais kwa tiketi ya CHADEMA mh Lazaro Nyalandu amesema wakati wa utawala wa Rais Mkapa yeye alikuwa msaidizi wa Mama Anna Mkapa hivyo amesafiri sana huko Duniani na mzee Mkapa.

Nyalandu amesema hayo wakati akiweka saini kitabu cha maombolezo msiba wa mzee Mkapa.

Chanzo: ITV habari

Maendeleo hayana vyama!
 
Nyalandu baada ya Kusomeshwa na zile Scholarships za Kanisa alifanya kazi muda mrefu tu EOTF( Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote) taasis ya ANBEN

Na walimshika mkono kwa kiwango kikubwa katika harakati zake za mwanzoni za kisiasa

Mwingine aliyebahatika na Taasis za First Lady ni Dk. Kigwangala naye safari yake ya kisiasa imeanzia ikulu ya mkwere akiwa mfanyakazi wa Mama Salma(WAMA)

Sijui kwann mama Janet hana kataasis ka kupotezea muda
 
Kwa akili hiyo ndio apewe nchi kusafiri sana na mama
 


Nimeweka link ya video, ulichokifanya ni kama alichokifanya yule mjumbe aliyemuuliza swali mwakyembe kwenye mkutano wa kura za maoni kule kyela, kama alivyojibu mwakyembe na mimi naomba kukuuliza, kwa akili hizi ulifanyaje mtihani wako wa darasa la saba wewe?

Hilo darasa la 7 tulikuwa wote wewe bavicha?!
 
Back
Top Bottom