Nyangumi anaweza kummeza mtu aliye hai?

Nyangumi anaweza kummeza mtu aliye hai?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Kwenye Biblia, kuna habari ya Mhubiri aitwaye Yona kumezwa na "samaki" mkubwa na kisha kutapikwa siku ya tatu. Sijui kama kuna tukio jingine kama hilo Iilishatokea karne hii!

Mwaka 2021, raia wa Marekani, Michael Packard, alinusurika kuwa kitoweo cha nyangumi baada ya kujikuta ndani ya kinywa chake kwa sekunde zisizopungua thelathini. Mwanzoni alifikiri ni papa, lakini baada ya kutokuhisi meno ya papa, akajua kuwa ni nyangumi. Alifichwa kinywani mwa nyangumi kwa kutangulizwa kichwa, kwa hiyo hakuwa akiona chochote zaidi ya giza totoro. Aliingia kinywani mwa nyangumi na vifaa vyake vya kupigia mbuzi, ila inawezekana kiwiliwili kilibaki nje ya kinywa cha nyangumi.

Nyangumi aliyembugia alikuwa "mstaarabu". Hakulazimisha kummeza wala kumbinya kwa kinywa chake, badala yake, "alijongea" mpaka juu ya maji na kumtema hewani juu ya maji na kisha kuendelea na "mishe" zake.

Kwa mujibu wa wataalamu, nyangumi anao uwezo wa kumwua mwanadamu akiamua kufanya hivyo, ingawa hana asili ya uchokozi.

Uwezo wa kuu anao, ila sina uhakika kama anaweza kummeza mtu aliye hai. Inasemekana umio wake hauna uwezo wa kumeza kitu kikubwa kama mwili wa binadamu.

Ukweli ni upi? Nyangumi wa siku hizi wangali na uwezo wa kummeza mtu aliye hai kama ilivyokuwa wa kipindi cha Yona?

Mnusura ni huyo hapo chini.


 
Kwenye Biblia, kuna habari ya Mhubiri aitwaye Yona kumezwa na "samaki" mkubwa na kisha kutapikwa siku ya tatu. Sijui kama kuna tukio jingine kama hilo
Iilishatokea karne hii!

Mwaka 2021, raia wa Marekani, Michael Packard, alinusurika kuwa kitoweo cha nyangumi baada ya kujikuta ndani ya kinywa chake kwa sekunde zisizopungua thelathini. Mwanzoni alifikiri ni papa, lakini baada ya kutokuhisi meno ya papa, akajua kuwa ni nyangumi. Alifichwa kinywani mwa nyangumi kwa kutangulizwa kichwa, kwa hiyo hakuwa akiona chochote zaidi ya giza totoro. Aliingia kinywani mwa nyangumi na vifaa vyake vya kupigia mbuzi, ila inawezekana kiwiliwili kilibaki nje ya kinywa cha nyangumi.

Nyangumi aliyembugia alikuwa "mstaarabu". Hakulazimisha kummeza wala kumbinya kwa kinywa chake, badala yake, "alijongea" mpaka juu ya maji na kumtema hewani juu ya maji na kisha kuendelea na "mishe" zake.

Kwa mujibu wa wataalamu, nyangumi anao uwezo wa kumwua mwanadamu akiamua kufanya hivyo, ingawa hana asili ya uchokozi.

Uwezo wa kuu anao, ila sina uhakika kama anaweza kummeza mtu aliye hai. Inasemekana umio wake hauna uwezo wa kumeza kitu kikubwa kama mwili wa binadamu.

Ukweli ni upi? Nyangumi wa siku hizi wangali na uwezo wa kummeza mtu aliye hai kama ilivyokuwa wa kipindi cha Yona?

Mnusura ni huyo hapo chini.
Viumbe wa kwenye Biblia ni tofauti na viumbe wa sasa, ndio maana hata nyoka wa kwenye Biblia alilikua anaongea na binadamu hadi kufikia kuwashawishi wale matunda ya mti ule
 
Nyangumi ni rafiki wa binadamu ila usimuuzi either kwa kumuwinda akachomoka kwenye mitego yako au kumuulia mwanae ataifuatilia boti yenu mpaka aigonge na kuizamisha.
 
Kuna nyangumi aina nyingi ila baba lao anitwa blue whale huyo ni nyangumi mkubwa sana na anakula tani kazaa ya samaki kwa siku ila sio mkorofi kwa binadam na sijajua kn wanapenda kula binadam
 
Nyangumi ni wastaarabu sana 😍
Ni kweli mkuu nyangumi ni wastaarabu sana. Ndo maana wanajina la utani the gentle Giants.

Kamwe hammezi binadamu. Hata killer whales Orcas ukiwasogelea wanakukwepwa.

Nyangumi mkipishana ukiwa kwenye mtumbwi atazama chini nakupita.

Aina ya nyangumi nayempenda ni Humpback this majestic creature is awesome. Kinachomtofautisha na nyangumi wengine ni its long pictorial fins.

Mwengine ni the Blue whale ambaye ndo kiumbe mkubwa duniani.

Cha kushangaza kuba blue whales wa Sri Lanka hawahami migrate mda wote wako kwenye bahari ya Sri lanka na hiyo siyo kawaida. Imewaumiza kichwa sana wanasayansi na sisi wapendwa nyangumi.

Pia kuna nyangumi wengine wa ajabu sana wa Oman. Fikiria hawa nyangumi ni Humpback hulka yao ni kuhama. Lakini hao wako mda wote kwemaji ya Oman. Idadi yao inapungua lakini srikali ya Yemeni inajitahidi sana kuwaprotect.

Nilishaletaga uzi wa nyangumi wa Oman na Sri lanka jamvin kwa ID nyingine jamvin 2019.

 
Ni kweli mkuu nyangumi ni wastaarabu sana. Ndo maana wanajina la utani the gentle Giants.

Kamwe hammezi binadamu. Hata killer whales Orcas ukiwasogelea wanakukwepwa.

Nyangumi mkipishana ukiwa kwenye mtumbwi atazama chini nakupita.

Aina ya nyangumi nayempenda ni Humpback this majestic creature is awesome. Kinachomtofautisha na nyangumi wengine ni its long pictorial fins.

Mwengine ni the Blue whale ambaye ndo kiumbe mkubwa duniani.

Cha kushangaza kuba blue whales wa Sri Lanka hawahami migrate mda wote wako kwenye bahari ya Sri lanka na hiyo siyo kawaida. Imewaumiza kichwa sana wanasayansi na sisi wapendwa nyangumi.

Pia kuna nyangumi wengine wa ajabu sana wa Oman. Fikiria hawa nyangumi ni Humpback hulka yao ni kuhama. Lakini hao wako mda wote kwemaji ya Oman. Idadi yao inapungua lakini srikali ya Yemeni inajitahidi sana kuwaprotect.

Nilishaletaga uzi wa nyangumi wa Oman na Sri lanka jamvin kwa ID nyingine jamvin 2019.

Shabiki wa mbususu
 
Back
Top Bottom