Nyani Ngabu Mjengoni! Interview: Mapenzi, Utajiri&Mali, Marafiki na Maisha ya ugenini.

Nyani Ngabu Mjengoni! Interview: Mapenzi, Utajiri&Mali, Marafiki na Maisha ya ugenini.

Nyani Ngabu
Kabla ya kufika USA ulikuwa unavuta picha gani kichwani ambayo ulipofika ulikuta ni tofauti kabisa?

Uzuri wangu ni kwamba tokea nikiwa mdogo kabisa nilipata fursa ya kutembelea nchi mbalimbali za Ulaya.

Pia, nikiwa mdogo niliwahi kuishi Uingereza kwa miaka kadhaa.

Mshua wangu alisomea Marekani...shahada zake zote. Nyumbani tulikuwa tunaletewa majarida kibao ya Kimarekani kama vile Reader's Digest na Time Magazine, almanac ya CIA World Fact Book, World Book Encyclopedia, na kadhalika.

Kwa hiyo, ukijumlisha mimi kusafiri nikiwa mdogo, kuishi Uingereza, na kusikiliza stori za mshua kuhusu Marekani, kusoma hayo majarida na hivyo vitabu,picha ya Marekani niliyokuwa nayo kabla sijaenda ndo hiyo hiyo niliyoiona nilipofika. to Hakukuwa na surprise yoyote kabisa.

Halafu majirani zetu tulipokuwa tunaishi walikuwa Wamarekani. Kwa hiyo sikupata culture shock yoyote ile.

So I took to the USA like a duck to water🙂.

Na katika maisha yako ya ugeni ni kitu gani kilikuwa kinakusumbua mwanzoni?

Mwanzoni kusema ukweli nilikuwa homesick sana.

Kumbukua, nilienda USA nikiwa mdogo kwa kweli.

Kwa hiyo huo udogo, umbali, na ukizingatia kwamba mimi sina kaka wala dada, kuna nyakati nilikuwa najikuta napakumbuka sana nyumbani.

Sawa, baba na mama nilikuwa nao na ningeweza kuchukua tu simu na kuwapigia ili kuongea nao, lakini bado mazungumzo ya mtoto na wazazi wake ni tofauti na mazungumzo ambayo mtu unaweza kufanya na kaka au dada zako au hata marafiki zako.

Hivyo homesickness ndo ilinisumbua sana hapo mwanzoni mwanzoni.
 
Uzuri wangu ni kwamba tokea nikiwa mdogo kabisa nilipata fursa ya kutembelea nchi mbalimbali za Ulaya.

Pia, nikiwa mdogo niliwahi kuishi Uingereza kwa miaka kadhaa.

Mshua wangu alisomea Marekani...shahada zake zote. Nyumbani tulikuwa tunaletewa majarida kibao ya Kimarekani kama vile Reader's Digest na Time Magazine, almanac ya CIA World Fact Book, World Book Encyclopedia, na kadhalika.

Kwa hiyo, ukijumlisha mimi kusafiri nikiwa mdogo, kuishi Uingereza, na kusikiliza stori za mshua kuhusu Marekani, kusoma hayo majarida na hivyo vitabu,picha ya Marekani niliyokuwa nayo kabla sijaenda ndo hiyo hiyo niliyoiona nilipofika. to Hakukuwa na surprise yoyote kabisa.

Halafu majirani zetu tulipokuwa tunaishi walikuwa Wamarekani. Kwa hiyo sikupata culture shock yoyote ile.

So I took to the USA like a duck to water🙂.



Mwanzoni kusema ukweli nilikuwa homesick sana.

Kumbukua, nilienda USA nikiwa mdogo kwa kweli.

Kwa hiyo huo udogo, umbali, na ukizingatia kwamba mimi sina kaka wala dada, kuna nyakati nilikuwa najikuta napakumbuka sana nyumbani.

Sawa, baba na mama nilikuwa nao na ningeweza kuchukua tu simu na kuwapigia ili kuongea nao, lakini bado mazungumzo ya mtoto na wazazi wake ni tofauti na mazungumzo ambayo mtu unaweza kufanya na kaka au dada zako au hata marafiki zako.

Hivyo homesickness ndo ilinisumbua sana hapo mwanzoni mwanzoni.
Big up kwa kupuyanga kwenye nchi nyingi,
Enhe hebu tuambie katika nchi zote ulizokatiza, ipi uliyoizimikia sana kuliko zingine? Na kwanini?
 
Nyani Ngabu Unayatafsiri vipi mafanikio?

Mafanikio ni kupata na kuwa na kile ukitakacho na kukifurahia.

Yani ili uwe umefanikiwa kwa upande wako ni ili uwe na vitu gani?

1. Kisura wangu. Kumkuza na kumwona naye anafikia ndoto zake [na atazifikia tu maana ana akili sana na ni mjanja hata kunizidi].

2. Uhakika wa kula chakula nikipendacho, kuwa na sehemu nzuri ya kuishi, kuwa na afya njema, na furaha moyoni.

3. Kuendelea kuziongeza ziro kwenye akaunti zangu za benki.

Je, unadhani umefanikiwa kiasi gani?

Kwangu mafanikio ni suala endelevu na kwa sababu hiyo halina kikomo.

Na kwa sababu halina kikomo nachoweza kusema tu kwa sasa nafurahia mahali nilipo.

Kwa mfano, hata sasa hivi hapa nikiamua kwenda kununua jozi ya sneakers za Philipp Plein [ PHILIPP PLEIN: La Dernière Boutique en Ligne Mode de Luxe - Site Officiel | Philipp Plein ]naweza bila ya kuwa na wasiwasi wowote ule.

Nikiamua niende St. Thomas huko kupunga upepo naweza kwenda bila ya kuwa na wasiwasi wowote ule.

Nilicho nacho kwa sasa kinanitosha kuyafurahia maisha.
 
Hapana, sijaoa.

Ili nimewahi kuoa lakini tukaishia kutalikiana.

Nipo kwenue uhusiano? Hilo ni changamani [complicated]😀
Dah pole sana, labda unaweza kushea nasi japo kidogo sababu iliyofanya mpaka mkatalikiana? Nani alikuwa chanzo cha tatizo? Je, ni vitu gani unavyovimiss kutoka kwenye mahusiano yako ya zamani?
 
Hhahaha, Huenda una kipaji cha ubondia,..
Anyway, ni maisha ya namna gani ambayo uliyapitia na haupendi mwanao aje ayapitie?

Mimi nilikuwa mtundu sana. Pia nilikuwa mchokozi sana.

Kwa vile yeye ni binti basi nisingependa awe mtundu na mchokozi kama nilivyokuwa mimi.

Ila kama ujuavyo, tunda huwa halidondoki mbali sana na mti wake.

So it is what it is....

Hapa nilipo nina makovu kadhaa yaliyotokana na utundu na uchokozi wangu.

Huwa nikiyaangalia naishia kucheka tu.
 
Big up kwa kupuyanga kwenye nchi nyingi,
Enhe hebu tuambie katika nchi zote ulizokatiza, ipi uliyoizimikia sana kuliko zingine? Na kwanini?

USA haina mpinzani.

Kwa zilizobakia naweza kusema ni Ujerumani.

Ujerumani kuzuri bana.

Kumbuka Ujerumani ilibaki magofu tu baada ya vita vikuu vya pili vya dunia.

Ila jinsi jamaa walivyoijenga upya, it is impressive.

Ushaona wapi wewe Mercedes Benz kuwa teksi?

Ujerumani ndo hivyo sasa....

Na yale ma autobahns yao yale...hakuna cha speed limit wala nini....ni mwendo wa kupepea tu.
 
Hahah madada poa hawahesabiki hapa,
Je, baada ya one nite stand kuna kitu chochote ulikijutia?

Oh yeah!

Majuto lazima yawepo aisee.

Kwa sababu, mara nyingi hizo one night stands zilitokea katika mazingira ambayo nilikuwa chini ya ushawishi wa pombe hususan katika mitoko ya kwenda klabu usiku.

Kwenye mazingira kama hayo akili inakuwa haifanyi kazi vizuri.

Kesho yake akili ikikurudia ndo unajiuliza...'what the hell was I thinking'?

Kuna wakati flani hivi nakumbuka kuna kademu kamoja hivi kalikuwa na meno ya papachi halafu dizaini kama yalikuwa yameoza hivi.

Katika hali ya kawaida wala nisingehangaika nako...lakini nilijikuta najihusisha nako na kesho yake nikaishia kupata strep throat.

Oh well...
 
Mimi nilikuwa mtundu sana. Pia nilikuwa mchokozi sana.

Kwa vile yeye ni binti basi nisingependa awe mtundu na mchokozi kama nilivyokuwa mimi.

Ila kama ujuavyo, tunda huwa halidondoki mbali sana na mti wake.

So it is what it is....

Hapa nilipo nina makovu kadhaa yaliyotokana na utundu na uchokozi wangu.

Huwa nikiyaangalia naishia kucheka tu.
Ulishawahi kutumia kipaji chako kuingiza mkwanja? Ni kipaji gani hiko?
 
Dah pole sana, labda unaweza kushea nasi japo kidogo sababu iliyofanya mpaka mkatalikiana? Nani alikuwa chanzo cha tatizo? Je, ni vitu gani unavyovimiss kutoka kwenye mahusiano yako ya zamani?

Nachoweza kusema kwa upande wangu ni kwamba wote tulikuwa 'tatizo' ingawa yeye anaweza kusema labda mimi ndiye nilikuwa tatizo.

Ila kikubwa nadhani ilikuwa ni tofauti ya kiutamaduni.

Hapo kwenye tofauti ya kiutamaduni ndo vikazuka vijitofauti vingine vidogo vidogo.

Ambacho nakikosa ni ile kampani yake na kufanya baadhi ya mambo pamoja kama kwenda grocery shopping, kupika pamoja jikoni, kucheza cheza kama kurushiana mito na kukimbizana, kufyeka majani, kwenda kwenye road trips na mgegedo on-demand😉.

Kuna raha flani hivi kama tuseme umetoka kazini halafu una njaa unarudi nyumbani unakuta mwenzio keshatengeneza msosi au kama hajatengeneza yeye basi kaagiza toka sehemu.

Kama uko mwenyewe tu saa ingine unakuwa huna jinsi. Unarudi umechoka halafu una njaa...itabidi upike tu. Kama si kupika itabidi labda uagize sehemu.

Such is life, though.
 
USA haina mpinzani.

Kwa zilizobakia naweza kusema ni Ujerumani.

Ujerumani kuzuri bana.

Kumbuka Ujerumani ilibaki magofu tu baada ya vita vikuu vya pili vya dunia.

Ila jinsi jamaa walivyoijenga upya, it is impressive.

Ushaona wapi wewe Mercedes Benz kuwa teksi?

Ujerumani ndo hivyo sasa....

Na yale ma autobahns yao yale...hakuna cha speed limit wala nini....ni mwendo wa kupepea tu.
Nice..!
je, elimu uliyoipata darasani inakusaidia?
Kwamfano ungepata nafasi ya kuanza upya husle zako (kuanzia shule ya upili) ungechagua kufanya vitu gani?
 
Back
Top Bottom