Uchaguzi 2020 Nyehunge: Dkt. Magufuli amuamrisha Mfugale atangaze ujenzi barabara ya Sengerema-Nyehunge (KM 46) kisha amuulize hela za kujengea

Hapo watahamisha mafungu kutekeleza hilo agizo haramu huku wakiathiri mipango mingine.

Swali la kujiuliza ni je, kama anaagiza hivi hadharani, nyuma ya pazia huwa anaagiza mangapi?

Ni wazi hata Chato Airport imejengwa kwa style hii.

Jambo lingeni la hatari ni kuwa,yeye ana kinga, ila anaowapa maagizo hawana kinga, hivyo wawe makini kwani tawala zinabadilika.
 
Huyu jamaa hata akishindwa uchaguzi hatoki madarakani atalazimisha kuendelea

Atadai miradi alioianzisha ni mingi kwa hiyo atalazimisha kuwa lazima aione ikiisha

Miradi mingine itachukua hadi miaka 20 ijayo sasa Mtanzania piga mahesabu

Tayari Tanzania imempata raisi wa maisha Dikteta wa maisha
 
Siasa haina shida,shida iko uku kwetu bara jeusi na baadhi ya maeneo uko kwingine wenye akili zinazokaribiana na zetu.Lakini kwa wenye akili zao siasa iko vizuri labda mapungufu madogo madogo tu.ila uku kwetu kuanzia utaratibu hadi wagombea ni tabu tupu.
Hapo kuna wadau wanachekelea 10% .. ila siasa ni ujambazi mkubwa sana kugunduliwa na mwanadamu.
 
Hiyo ni rushwa ya uchaguzi.

Haikubaliki.
Siyo rushwa kila wakati Magufuli akiona jambo haliko sawa hana subira,ni mtu wa vitendo bila kuchelewa.

Lakini pammoja na mihemuko ya uchaguzi wa uraisi,Magu the bulldozer hana mshindani bora arudi kwenye majukumu yake hadi 2025.
 
Rushwa na hili suala TAKUKURU pamoja na Tume ya Uchaguzi NEC inatakiwa walifanyie kazi mara moja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…