Uchaguzi 2020 Nyehunge: Dkt. Magufuli amuamrisha Mfugale atangaze ujenzi barabara ya Sengerema-Nyehunge (KM 46) kisha amuulize hela za kujengea

Uchaguzi 2020 Nyehunge: Dkt. Magufuli amuamrisha Mfugale atangaze ujenzi barabara ya Sengerema-Nyehunge (KM 46) kisha amuulize hela za kujengea

Hiyo ni rushwa kama rushwa nyingine zilivyo!Hata mzee wa ubwabwa aliona tatizo wananchi wana njaa,akaamua kukitatua hapo hapo kwa kuwapa ubwabwa ila akaambiwa hiyo ni rushwa!
Kama ameona kuna hitaji la barabara,kwanini asifanye mawasiliano na huyo mfugale ili mkakati ufanyike na kazi ifanyike?Kwanini atumie jukwaa la kampeni?Hiyo ni rushwa,muiname muinuke hiyo ni rushwa!
Mhh mkuu mwananchi yeye anataka barabara, hajalishi ni uchaguzi au hapana.
Sisi wananchi tunataka haki ya kuwa na barabara na sio sheria ya kuwa na barabara wakati usio wa uchaguzi.Afterall yanini kutumia hesabu mbovu wakati fika yule Magu ataendelea,tunamdanya nani.
 
Haya ndio madhara ya katiba yetu yaani huyo ni mgombea wa kiti cha urais wakati huo huo ni rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania.
 
Tume wako wapi?? Walikataza pilau kuku la Rungwe;kuna mtu amekuja na barabara.....
 
Huyu jamaa swala la aibu kwenye kutokufata sheria. Ninawaza sana wakurugezi watakaotangaza kura kuwa ameshindwa kwenye majimbo yao.
 
DKT. Magufuli akiwa anaendelea na kampeni za uchaguzi 2020, amepita kijiji cha Nyehunge akiwa anaelekea Geita ambapo kutoka Sengerema mpaka Nyehunge ni kilomita 46. Alisimama kuongea na wananchi waliokuwa wakimsubiri barabarani, wakati anaielezea barabara hiyo ghafla aliomba simu yake na kumpigia mtu ambae baadae alijulikana ni mkurugenzi mkuu wa TANROADS, Injinia Mfugale na mazungumzo yao yalikuwa hivi.

Magufuli: Hallo, Chief executive

Mfugale: Naam mheshimiwa Rais

Magufuli: Hujambo

Mfugale: Sijambo mheshimiwa

Magufuli: Uko wapi?

Mfugale: Niko Dar es Salaam TANESCO tunazungumzia habari ya Nyerere dam.

Magufuli: Haya, sasa mimi niko Nyehunge, kutoka Sengerema mpaka Nyehunge ni kilomita 46, hii barabara tumeshaifanyizia feasibility study na detail design, nimesimama hapa na wananchi, nataka hii barabara, mimi si ndio Rais?

Mfugale: Ndio mheshimiwa(Wananchi kicheko cha furaha)

Magufuli: Nyehunge Oyee, Unanielewa Chief? Basi hii barabara uitangaze kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Huu ni mwezi wa ngapi? (Mfugale: Mwezi wa tisa). Haya uandae document zote kabla ya mwezi wa 12 haujafika na kandarasi apatikane, niulize hela nitazitoa wapi. Sawa Mfugale?

Mfugale: Nimekuelewa mheshimiwa Rais

Magufuli: Umenielewa, mueleze na Waziri kwamba hayo ni maagizo yangu wala yasibadilike, Asante sana.

MWISHO WA MAONGEZI

Huyu ni mgombea anaomba kura? Au rais kazini akitoa maagizo ya kiserikali? Au ni rushwa kwa wapiga kura?

Usawa kwa wagombea uko wapi?

Tume endeleeni kufumbia haya kuwa haya wahusu.
 
DKT. Magufuli akiwa anaendelea na kampeni za uchaguzi 2020, amepita kijiji cha Nyehunge akiwa anaelekea Geita ambapo kutoka Sengerema mpaka Nyehunge ni kilomita 46. Alisimama kuongea na wananchi waliokuwa wakimsubiri barabarani, wakati anaielezea barabara hiyo ghafla aliomba simu yake na kumpigia mtu ambae baadae alijulikana ni mkurugenzi mkuu wa TANROADS, Injinia Mfugale na mazungumzo yao yalikuwa hivi.

Magufuli: Hallo, Chief executive

Mfugale: Naam mheshimiwa Rais

Magufuli: Hujambo

Mfugale: Sijambo mheshimiwa

Magufuli: Uko wapi?

Mfugale: Niko Dar es Salaam TANESCO tunazungumzia habari ya Nyerere dam.

Magufuli: Haya, sasa mimi niko Nyehunge, kutoka Sengerema mpaka Nyehunge ni kilomita 46, hii barabara tumeshaifanyizia feasibility study na detail design, nimesimama hapa na wananchi, nataka hii barabara, mimi si ndio Rais?

Mfugale: Ndio mheshimiwa(Wananchi kicheko cha furaha)

Magufuli: Nyehunge Oyee, Unanielewa Chief? Basi hii barabara uitangaze kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Huu ni mwezi wa ngapi? (Mfugale: Mwezi wa tisa). Haya uandae document zote kabla ya mwezi wa 12 haujafika na kandarasi apatikane, niulize hela nitazitoa wapi. Sawa Mfugale?

Mfugale: Nimekuelewa mheshimiwa Rais

Magufuli: Umenielewa, mueleze na Waziri kwamba hayo ni maagizo yangu wala yasibadilike, Asante sana.

MWISHO WA MAONGEZI
Yaani kwenye nchi ya demokrasia ya kweli, alipomaliza tu mazungumzo haya tume ya uchaguzi ingetangaza kumwengua huyu mgombea. Kama kutumia tu gari la serikali kwenye shughuli ya siasa ni marufuku sembuse kutumia haya madaraka. Eti, mimi ni Rais. Sasa kama ni Rais anapiga kampeni za nini?
 
Huyu jamaa swala la aibu kwenye kutokufata sheria. Ninawaza sana wakurugezi watakaotangaza kura kuwa ameshindwa kwenye majimbo yao.
"Nikununulie gari, nikulipe mshahara, nikupe nyumba halafu eti unamtangaza mpinzani kashinda! Hiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii" (Magu, 2019)
 
Back
Top Bottom