sblandes
JF-Expert Member
- Apr 25, 2010
- 6,632
- 4,737
Kama umenielewa vizuri nimekwambia acheni kelele za kila msimu wa uchaguzi dai katiba ya Jaji Warioba kwanza.Hapa unajaribu kusemaje?Kuwa huwa mnashindwa uchaguzi ila mabavu yanawabakiza madarakani?
Tambua kuwa haki huinua taifa na kustawisha amani na utulivu!Unaweza usiwe mkomavu wa kutosha kuelewa haya,ila ikifika wakati wananchi wakadai haki yao kwa namna nyingine,ndio hapo majuta huwa mjukuu!Mifano ipo mingi na hai!Wale wanaodhulumiwa haki yao wakichoka huwa ni suala la muda tu,na ndio hapo hata maadui inakuwa rahisi kupenyeza mambo yao!Mtu akifikia breaking point,ukampa silaha unategemea nini?Uasi hujengwa taratibu,pigieni chapuo uovu ila tambueni kuwa wanaodhulumiwa nao wana kipimo cha uvumilivu!
Vinginevyo rudisha chama kimmoja mpambane ndani kwa ndani kama zamani.