Nyerere aliwagomea TANU kususia uchaguzi ila Mbowe kawashawishi CHADEMA kususia!! Hili laweza kuwa kaburi la CHADEMA

usiwatonye waache wasusie 2025, 2030, 2035, mpaka 2100...huko mwenyekiti atakuwa kitukuu wangu...atupele mapugiro...
CCM inapendwa sana na wananchi.Na itatawala mirere.Vyama vingi vifutwe na chaguzi zifutwe.
 
Sasa mkoloni pamoja na roho mbaya yake alikuwa na tume huru, ccm hawataki tume huru wanataka ya ma DAS ambao ni Masada wao
 
..ungemuuliza mwaka 1958 wagombea wangapi wa Tanu walienguliwa na serikali ya mkoloni?

..halafu tulinganishe na Tume ya uchaguzi ya Tanzania huru inavyoengua maelefu ya wagombea wa vyama vya upinzani.
Wapinzani ni vibaraka wa Mabeberu.
 
Mashabiki/wanachama wa UTO unakiwewee sanaa[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 

Hata kama cdm wataamua kushiriki, sisi wapiga kura tunaojitambua hatuko tayari kuendelea kushiriki huo ushenzi uitwao uchaguzi kwa mapungufu yaliyopo. Kama ni kudai haki na malalamiko tumeshatoa sana, ni ujinga kuendelea kushiriki kwa zoezi ambalo limeshaonyesha ushenzi wa hali ya juu.

Hao wanaotaka kukimbilia kwenye vyama vingine, kikiwemo hicho kinachotaka kuanzishwa na ccm kwa kushirikiana na Tiss ni haki yao, lakini sisi tunaojitambua tutaendelea na msimamo wetu. Na chaguzi hazitakaa zipate tena wapiga kura wengi bila mabadiliko makubwa ya msingi. Muda wa kuburuzwa na chama cha karne iliyopita umekwisha, na mkilogwa mkakubali marekebisho ya msingi kwenye chaguzi, jiandaeni kisaikolojia. Ccm ya kushinda kihalali zaidi ya 50% ya uchaguzi halali ilishatoweka.
 
Mmeona chaguzi zimedoda, sasa mnataka kuwashawishi cdm washiriki ili mpate mvuto. Wananchi ndio tumesusia huo ukhanithi, hata vyama vyote vikiamua kushiriki, bado wapiga kura hatuko tayari kwa ule uhayawani tunaouona kwenye box la kura.
Kwa nini kila anayetoa maoni tofauti na msimamo wa chama anaeonekana adui wa chama au ccm!? Jamani tukubali kufikiri nje ya box, hivi hata wasusie miaka mia unatazamia wataathiri nini!?
 
Unajielewa? haikusaidia chochote? unajua Serikali ya Umoja wa kitaifa ilisababishwa nanini? sema Maalim mwenyewe aliinua mikono kwenye Game angeelendelea kukaza wangepata wanachotaka...shida watu wanataka wapambane leo na wafanikiwe leo batle ya Maalim ingeweza kuipa znz Haki watu wote lkn kujiunga kwenye Serikali ya Umoja bila terms za maana manake wamekubali matokeo ...lkn resistance ikiwa Kali watawala wanarudi mezani
 
Hawa Wakoloni weusi wanaopaka mikorogo na mawigi ni hatari kuliko Mkoloni mweupe.

Mauwaji,utekaji,ubambikaji wa kesi na kuwafunga Innocent Tanzanians kwenye Majela,

Chadema tuko sahihi, kususia Uchafuzi, kwasababu hata tukishinda CCM ndio watakaotangazwa, Mkoloni mweupe hajawahi kufanya hivyo.

Hawa Wakoloni weusi ni very dangerous.
 
Mkuu why chama dola chako hawataki to level the playing field?hivi unaona ni haki kuwa na so called tume ya uchaguzi iliyoteuliwa na mgombea?hivi unaona ni halali kuwa na tume ya uchaguzi kwenye ngazi ya taifa tu huku ngazi zingine wanatumika cadres wa chama dola?ur a middle class pls unaweza kufikiri better kuliko waliowengi huku Lingusenguse. President Nyerere alikua anawaza Urais tu ndio maana akalazimisha tanu ishiriki uchaguzi na elewa tanganyika haikua koloni !
 
Kaburi la nara ngapi?mbona ilishazikwa zamani

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 

Mkuu naheshimu sana mawazo yako lakini jambo moja nikumbushe kilichomfanya maalim anyoshe mikono ni Hali halisi kwani wabunge aliopata safari hii walikuwa wachache mno kuliko ambao angewapata wakati ule aliposusa na ukisema kwamba angeendelea kukaza angeambulia chochote pia sio sahihi kwani ile awamu iliyopita ndipo alikaza alikini bado ameambulia kidogo sana kwa hiyo mambo ya kususia uchaguzi yanakiumiza chama. Ni heri uonewe kisha ulalamike kuwa umeonewa ukiwa na vielelezo vya kuonewa kwako sio kulalamika huku umekimbia ulingo
 
Diwan ccm, mbunge ccm, rais ccm, Mkt wa mtaa ccm, Ded ccm= DSM hakuna maji wala umeme miaka 60 baada ya uhuru.
Wapinzani wametuchelewesha sana.
Au nasema UONGO ndugu zangu jamani????
 
Sjajua watu mnataka wapinzani waishi vipi!?
Wakishiriki chaguzi na kuporwa ushindi mnawanga kuwa ni wajinga, wanashiriki chaguzi wanazojua kabisa kuwa hawatashinda au hata wakishinda hawatpewa ushindi! Sasa wameamua kufanya jambo linaloeleweka ! Huwezi kukaa unaendelea kupanda mbegu shambani wakati kila mwaka hazioti au hata zikiota ndege wanakula mazao yote, huo ni uzwazwa!
Mahala CCM ilipofika sasa hata wakoloni walikuwa nafuu mara mia moja!
Hakuna haja ya kutupa nguvu bure , kwanza tupiganie katiba tu mengine yote yatakaa sawa yenyewe!
 
Diwan ccm, mbunge ccm, rais ccm, Mkt wa mtaa ccm, Ded ccm= DSM hakuna maji wala umeme miaka 60 baada ya uhuru.
Wapinzani wametuchelewesha sana.
Au nasema UONGO ndugu zangu jamani????
Hata ambapo vyama pinzani vimeongoza unaweza onyesha tofauti yoyote tofauti na mahali wameongoza ccm!! Wanasiasa wote lao moja!!
 
Siasa ni mapambano kwa hiyo wapambane kwenye uwanja wa mapambano wasikimbie pambano!!
 
Hata ambapo vyama pinzani vimeongoza unaweza onyesha tofauti yoyote tofauti na mahali wameongoza ccm!! Wanasiasa wote lao moja!!
Tuliaminishwa kwamba sehemu fulani hakuna maendeleo kwa sababu alichaguliwa mpinzani
 
Hakuna ushindi unaopatikana kwa huruma za mshindani wako lazima utunishe msuli ili ushinde.
Dr slaa aliwahi kusema haki hailetwi kwenye kisahani lazima ipiganiwe kwa nguvu
 
kuna tofauti kubwa kwani wakati wa ukoloni walau sheria za uchaguzi ziliheshimika na kura zilihesabiwa kwa uwazi mkubwa aliyeshinda kashinda aliyeshindwa kashidwa, ila kwa sasa ni uharibifu mtupu, mauaji, utekaji wa wagombea na wizi wa kura wa wazi wazi - sasa kuepusha haya yote ni kheri kama kiongozi ukawaeleza watu wako kupigania katiba mpya na Tume iliyo huru ya uchaguzi.
 
Hakuna ushindi unaopatikana kwa huruma za mshindani wako lazima utunishe msuli ili ushinde.
Dr slaa aliwahi kusema haki hailetwi kwenye kisahani lazima ipiganiwe kwa nguvu
Hizo zote ni dalili za kikatili na kidekiteta na upendo haupo,why utumie misuli kushinda chaguzi?na ndio maana tunatakiwa tuzilee family zetu kwa upendo na mashule yetu yawe hivyo hivyo na hii corporal punishments futilia mbali.ccm bila polisi tiss jeshi etc etc hawawezi shinda chaguzi yeyote ile
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…