Nyie mnaopenda kuiga biashara za watu hebu jaribuni kuweni wabunifu, mnaleta chuki ipo siku tutakuja kuonana wabaya

Ukiwa ndani ya jiji la New york peke ake,unaambiwa ukiwa unaenda kula kwenye mgahawa mmoja kila siku,basi utatumia miaka 27 kuitembelea migahawa yote.Piga hesabu idadi ya migahawa iliyopo kwenye hilo jiji.

MORAL OF STORY:
Kuwa m'bunifu,hakuna biashara ya peke yako.Kama hutaki ushindani basi nenda sayari ya Jupiter au Mercury ukafungue huko.
 
Biashara ya kuigana Kariakoo tu ndiyo Imefanikiwa...

Imagine unakuta mtaa mmoja wote Biashara ni moja...Mtaa mwingine hivyo hivyo..
Na kila Duka linauza..
Hakuna shida ilimradi faida ipo kama utashindwa kuhimili ushindani funga Duka.
 
Huyo ni mpuuzi asiyejua biashara
 
Huyo mwenye fremu wako yupo vizuri sana mkuu nawatafuta sana watu wa aina hii , sio wale wenye njaa njaa tu hawajui kama kuna ishu za kugombanisha wapangaji wa fremu
 
Ubunifu gani ambao nimeushindwa mimi?? Nyie ndio mnaoleta nuksi na wanga ili sisi tulioanza tufeli ili nyinyi muendelee kuchukua nafasi yetu
We kubali umezidiwa vitu vingi ndomana unapiga kelele, angekuja na mtaji wa laki tano wala usingepanic ungekuwa unachekea kwenye sufuria, lkn Kwa vile kaja full equipped ndomana unapiga mayowe.
 
Biashara inaangalia ubunifu the way unawaudumia wateja na wewe unavyojamiana na wateja that all don't https://jamii.app/JFUserGuide ur hope ,

Pia hakikisha unasali Sana Biashara bila Nguvu za kiroho huwezi kutoboa Wala kusonga mblele I remember Kuna siku Jamaa alipata hofu baada ya My momy kuongeza mpangaji katika e eneo lile la Biashara yake ,


Lakini mauzo yaliongezeka maradufu so ubunifu dua amka hata saa nane keep prayer
 
Watakuelewa wachache sana binafsi nilikuwa napiga sana pesa akaja mtu Fulani akafungua mbele yangu ..yaani upande unaotokea wateja wangu kwhy nataka kufanya jambo atajuta,
 
Biashara ya kuigana Kariakoo tu ndiyo Imefanikiwa...

Imagine unakuta mtaa mmoja wote Biashara ni moja...Mtaa mwingine hivyo hivyo..
Na kila Duka linauza..
yaah kkoo hata maduka 10 ya mtaa mmoja biashara ni aina mojaa... Ukija uswazi balaa tupuu ndo maaana hata biashara ya dawa inaanza kuwa ngumu maduka na famasi kila konaa.
 
Haelewi biashara huyo mwenye fremu, msomesheni.
 
Ndo nilichojifunzaa kwa mjini huwezi kuta sehemu pamechangamka hakuna biashara unayoifikiriaa utofauti utakuja kwenye gharama za bidhaa au ubora wa huduma mkuu.
 
Upangaji wa biashara ni jukumu la serikali kwa baadhi ya nchi na nchi na sio kiholela kama kwetu

Kuna watu povu limewatoka bila kutembea na kuona Dunia huwezi kujua mambo mengi na ndio maana wengi hawana uelewa

Kwa mfano UK biashara zina namba kuanzia A1,A2,A3,A4, na A5 zote hizo ni biashara tofauti tofauti
Unakuta duka linakodishwa kwa mfano A1 hiyo ni biashara ya posta, au retail goods na huwezi kufungua chakula kama mgahawa

Biashara zinadhibitiwa na serikali na sio kiholela kama sisi

Zipo biashara zinazofanana mtaa mmoja labda kwa sababu ya demand lakini sio kuweka vinyozi 5 mtaa mmoja
 
Comment yangu umeielewa Mkuu?
Hakuna biashara ya pekeyako babu hata wakiwa Mia mtaa mmoja sifa kuu ya soko huria ni ushindani we ufanisi duni hasara zitawatoa kwenye gemu na wenye ufanisi watasavaivu, Sio kazi ya soko kuangalia Nani anauza na Nani hauzi cha msingi bidhaa sokoni iwepo ya kutosha nguvu ya demand n supply ndo itaamua Nani afunge Duka na Nani aendelee
 
Maduka ya kariakoo ni tofauti na maduka tulipo sisi huku mtaani, kule wanawateja wengi na mwingiliano wa watu ni mkubwa tofauti na huku mtaani ambapo watu wakipita unawahesabu kabisa.

Alafu isitoshe mimi sijakataa kuwe na biashara ya aina moja sehemu moja, lakini mimi hofu ni kwamba biashara za aina moja zinapokuwa nyingi sehemu moja kwenye maeneo ambayo hayana mwingiliano mkubwa wa watu unafikiri nini kitatokea kwa wafanyabiashara wa maeneo hayo??

Hapa nilipo mimi kuna stationary kama nne mimi pia nikiwemo, anakuja mtu anafungua stationary apo apo mwisho wa siku wauzaji tunakuwa wengi kuliko wanunuzi na hapo biashara lazima iwe ngumu.

Kingine ni kuhusu hawa wamiliki wa fremu. Unampangisha mtu afanye biashara the same ambayo mpangaji wa awali anaifanya! Howcome?? Apo si nikuleta uchonganishi na kugombanisha watu bila sababu za msingi??

Mwisho wa siku tunaanza kuitana wachawi, yaani acha tu ndugu yangu.
 
Bila shaka bihashara Bado mpya eeh [emoji23][emoji23][emoji23] maana sio kwa makasiriko hayo. Ongeza ubunifu mkuu na namna ya utoaji huduma, hiyo ndiyo silaha yako kuu. Lasivyo utahama hapo bila kupenda [emoji16][emoji16]. Halafu punguza hasira, bihashara haitaki hiyo. Pambana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…