Nyota ya Mandonga imeanza kufifia, sasa ni zamu ya Zumaridi na DJ Ally B

Teko Modise

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2017
Posts
2,331
Reaction score
7,733
Bondia wetu Mandonga taratibu anaanza kutoka nje ya reli. Ule umaarufu wake umeanza kupotea kiaina. Yeye sio wa mwanzo wala sio wa mwisho katika watu walioibuka na ku-vibe kisha kupotea.

Huko nyuma alishawahi kuwepo babu wa loliondo, nabii tito, pierre likwidi, Dr. Shika na wengineo wengi.

Sasa naona zamu ya Zumaridi ambaye anapewa airtime na media ya Tanzania kuongea vitu vya kufikirika.

Pia kuna mtu anajiita DJ Ally B almaarufu Profesa au Asumani.
Yeye hupiga kelele na miluzi akiwa kwenye gari lake...basi nae kawa maarufu.

Wakati ni ukuta!
 
Mandonga anapotea TZ ila Kenya ana trend sana, hii itamsaidia, ukiwa maarufu hapa TZ ukajulikana Kenya basi umeshamaliza.

Kina MR Nice mpaka sasa wanapiga show Kenya huko
Hivi kale kajamaa ka mr Nice kumbe bado kapo?
Maana kuna mwaka flani kaliugua sana akakonda na kubaki kichwa tu badae wakazusha amekata kamba kumbe alitoboa?!
 
Huu ni wakati wa Zuma akee, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kwani kuna pambano hapa kati amepigana kimyakimya?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…