NYUMA YA PAZIA: CHADEMA ilivyosalitiwa 2015 - Dkt. Slaa

NYUMA YA PAZIA: CHADEMA ilivyosalitiwa 2015 - Dkt. Slaa

Ameeleza sababu za kupigwa mlinzi wake akiwa Katibu Mkuu pale chadema ,na wapigaji ni kina Boniface
 
Nakumbuka kwenye orodha ya mafisadi awamu ya pili alimtaja na Magufuli,je ameandika kwenye hicho kitabu kwamba alimtaja Kama fisadi?
 
asante kwa dibaji nzuri,nitachukua nakala yangu leo
Chadema hawawezi kununua hata uwape bure,kuna ukweli mchungu humo
Mkuu. Wale CHADEMA original lazima tukinunue tukumbushie enzi zetu kabla akina Tundu Lisu na mwenyekiti hawajakiuza chama chetu kwa CCM.
 
Naomba mzee mwanakijiji utuelezee na summary ya list ya mafisadi ya pale Igunga tafadhali
 
Akirudi kutoka Swedeni kwenye maandishi ya mwanakitongoji atamkuta Lowasa CCM "strange bed fellows "...alikuwa hataki kulala na Lowasa kitanda kimoja sasa atalala naye.
Duh!
Mi bado sijakisoma hicho kitabu kamanda.
Kaandika amerudi CCM kama akina Prof Mkumbo na Anna Mgwira?
 
Japo sijakisoma hicho kitabu ila kuna vitu Dr. Slaa hawezi kusema, kwa vile mimi nilibahatika kukaa nae mahali akiwa na mkewe Josephine, just the three of us, Josephine ndio kila kitu kwa Dr. Slaa, kule kujidai kususa kwa sababu ya kugombea urais it's all just lies kwa sababu msimamo naujua from horses mouth, kwa vile yalikuwa maongezi ya off the record, sio ustaarabu kusema walisema nini ila mimi humu nilisema haya kuhusu Chadema, hakuna akiyeamini ila ukweli ni huu.


P

Nashukuru mkuu kwa kunipandishia hizo na kuielewa hoja yangu, Unapodhamiria kuandika kitabu usifocus tu biashara bali ni vyema pia ukafocus ukweli wa mambo mengi yaliyojificha hata kama ni aibu kuyasema ni vyema tu ukayasema maana umeamua kuandika kitabu uondoe sintofahamu kwenye jamii tofauti na hapo bado utakuwa umeiacha bado jamii kwenye sintofahamu..

Kitabu hiki maudhui yake pia yanapaswa kutuambia JE NI KWELI GWAJI BOY ANAFAA KUWA NA WAFUASI/NABII/MCHUNGAJI WA KWELI AU NAYE NI MSANII TU aka Opportunistic anayetafuta msosi tu hasa katika kila fursa ikiwemo fursa ya 2015..
 
Huyu Mwanakijiji was siku hizi hata simuelewi elewi kabisa. Anyway kila zama na watu wake kwa sasa tuna " 🔑gogo" walau anatoa vitu halisi na haja egemea kokote.
 
Nashukuru mkuu kwa kunipandishia hizo na kuielewa hoja yangu, Unapodhamiria kuandika kitabu usifocus tu biashara bali ni vyema pia ukafocus ukweli wa mambo mengi yaliyojificha hata kama ni aibu kuyasema ni vyema tu ukayasema maana umeamua kuandika kitabu uondoe sintofahamu kwenye jamii tofauti na hapo bado utakuwa umeiacha bado jamii kwenye sintofahamu..

Kitabu hiki maudhui yake pia yanapaswa kutuambia JE NI KWELI GWAJI BOY ANAFAA KUWA NA WAFUASI/NABII/MCHUNGAJI WA KWELI AU NAYE NI MSANII TU aka Opportunistic anayetafuta msosi tu hasa katika kila fursa ikiwemo fursa ya 2015..
Umesoma ukaona hayo uliyoyatarajia hayamo?
 
Kuna mambo mengi mno KWENYE SIASA yanayohitaji utulivu wa kutosha kuyaelewa
Dk Slaa katika hatua za awali alikubaliana na wazo la LOWASA kujiunga na CHADEMA
Tulipomuuliza kwenye kamati kuu kwanini alikubali kujiunga kwa Lowasa kwenye chama, akatujibu kwamba Lowasa alisema atakuja na mtaji ambao kwa wakati ule Dk alisema hakuuona
Pili alisema alidhani Lowasa atakuwa mwanachama tu lakini hatakuwa mgombea urais
Tatu ,alisema Lowasa atoke hadhani kwa watanzania ajisafishe kwanza kuhusu tuhuma za ufusadi ambazo yeye(Dk slaa)ana ushahidi nazo.
Sisi tulimuita Lowasa mbele ya Dk slaa( katibu mkuu) wetu kipindi hicho na Lowasa akatolea ufafanuzi kila jambo kwa ufasa.
Katika hatua hiyo Dk Slaa akaridhika lakini baadaye hatukumuona bali tulichoona ni barua ya kumkaimisha Salum Mwalimu nafasi yake.
Maoni yangu ya ujumla ni kwamba Dk Slaa alikuwa sahihi kusimamia kile alichokiamini lakini alichoghafilika kidogo ni kuharibu kazi kubwa aliyoipigania kwa miongo miwili mizima yaani robo ya umri wake kwa kukwazwa tu kwa mara moja.
Lazima katika haya mapambano tupime baina ya masilahi mslapana ya jamii na taasisi tunazozisimamia ukilinganisha na masilahi yetu. Nadhani Dk amesimamia masilahi yake zaidi kuliko masilahi mapana ya jamii ya wapenda mageuzi makububwa ya mfumo wa kiutawala.
Kitabu cha Dk mambo mengi ameyasema kwa ukweli kufurahisha watu fulani wa makundi fulani na ndio maana nasema ni wakati wa watanzani kupima wanasisa vizuri bila kujali vyama vyao.
Dk Slaa hawezi kuwaona viongozi wa CHADEMA kama viongozi waliodalalia chama chao. Mwanzoni
kiongozi kama Mbowe,Tindu Lisu,Mnyika walikuwa hawkubaliani kabisa na swala la LOWASA kujiunga na CHADEMA lakini sisi wajumbe wa Kamati kuu ndio tuliowalazimisha baada ya kuona uwezo na nafasi ya Lowasa kukiletea chama ushindi
Hatukukjbsliana kirahisi ila tulipata nguvu ya kuwashawishi baada yakuona kwamba katika hatua za awali Dk Slaa aliunga wazo hilo mkono.
Kwahiyo Dk kushutumu vio gozi wenzake ni kujitetea kusiko na mashiko yoyote.
Lakini mwisho wa siku yote ni historia CHADEMA ipo na itaendelea kuwepo bila kujali mawimbi yanayoikumba,
tukumbuke dr Slaa anatumiwa na chama chake kipya, ccm kuiua CHADEMA.
uchaguzi mwakani atarudishwa kukitetea chama cha ccm,

Moja ya Mjumbe wa kamati kuu aliyekwenda na ujumbe wa kamati ndogo ya kamati kuu kwenda kuongea na Dk Slaa kuhusu uamuzi wake huo.
Jambo kubwa alilolalamika ni kwamba hamkubali LOWASA lakini tatizo kubwa lilokuwa dhahiri ni kwamba alishafanyiwa maandalizi yote ya kuwa mgombea Urais kwanini ghfla tu Kamati kuu inafanya mabadiko ya mgombea.
Tulimpa facts zote lakini hakutaka kutuelewa.
Katika kikao Cha kamati kuu alipewa facts zote kwanini ni muhimu kumkubali Lowasa licha ya upungufu ambao uitajwa kwa LOWASA na kwamba yeye hawezi kukipa chama ushindi au upinzani ambao ungefanana na wa LOWASA pamoja na upungufu ambao LOWASA alisemekana anao.
Kamati kuu ilimuambia Demokrasu ni kuhusu watu na watu wanasema nini kwa wakati huo.
Mwaka 2015 LOWASA alikuwa ni mwanasiasa anayekubalika kwa jamii ya makundi yote kuliko mwanasiasa yoyote kwa kipindi kile hususani kwa wagombea Urais waliokuwa wametia nia.
Tulimueleza Dk kuanza kutafakarifu udhaifu wa Lowasa ambao kwa maeneo mengine umeongezewa chumvi ilihali wananchi wanampenda hakutusaidii kupata ushindi au kutoa upinzani wa kutosha kwa mgombea wa CCM.
Na mimi binafsi nilimuambia Dk Slaa hata kama LOWASA hatashinda Urais lakini atakuwa Katibu mkuu wa Chama kikibwa sana nchini.
Naamini uwezo wa Dk Slaa ni Mkubwa sana kwahiyo angesimama kwenye nafasi ya ukatibu mkuu kipindi kile cha uchaguzi tungepata idadi kubwa ya wabunge na madiwani kuliko tuliopata sasa
Lakuni hata kura za uais huenda zingekuwa nyingi kuliko zilizopatikana kwa matangazo ya Tume ya Uchaguzi
Kwahiyo nadhani kitabu chake anataka tu kuwaaminisha wananchi kuhusu uhalali wa uamuzi wake lakini kama hakuwa na mbegu ya ubinafsi hakupaswa kufanya uamuzi ule aliofanya.
Yote yamepita ,
CHADEMA tunapaswa kusonga mbele kwani haya tunayopitia ndio kanuni za mchakato wa safari tunayotaka kwenda
Kwavyovyote vile safari lazima ifike mwisho
Hivi kuna fact gani ya kumfanya mchadema HALISI enzi zile akubali eti LOWASA ndo apeperushe bendera ya CHADEMA?
Hata mimi hiyo sikukubaliana nanyi. Ndo maana hata kwenye UCHAGUZI niliona Bora kura yangu ya URAIS nimpe Magufuli tu.
Wengi tulioumizwa na uamuzi wa kihayawani kama ule tulimpa kura yetu JPM.
 
Lipumba aliishaeleza na akaeleweka,sikuwahi kudhani inahitajika kuandika kitabu kuelezea ule upuuzi. Credibility ya Dr. Slaa kuelezea nini kilichokuwa nyuma ya pazia ni ndogo sana, sababu gwajima aliishatueleza na Dr. Slaa hakukanusha kwamba kitu chochote ambacho Dr anataka kutujuza kwenye kitabu hicho kitakuwa ni hearsays, sababu wakati mambo yanahappen Josephine alikuwa amemfungia ndani asitoke. sasa anataka kuelezea yaliyokuwa nyuma ya pazia huko kwa Josephine au wapi?
 
Dr Slaa hawezi kuwa mwalimu mzuri wa siasa kwa sasa.

CHADEMA ni center party kinachofuata ideology ya social democracy na kwa miaka yake yote katika siasa amehubiri ideology alipohama CDM hakutangaza kuwa ideology hiyo ilikuwa haifai je kuhamia Kwake ccm amekubaliana na ideology ya ujamaa ya ccm ?

Kwangu mimi Dr Slaa ameshapoteza moral authority ya kuwa mwalimu wa siasa ije mvua like mvua hana ideology anayoiamini zaidi ya useless activism tu.
(Pichani kitabu kikianza kupatikana kwa Wabunge, Dodoma)

Na. M. M. Mwanakijiji

Umpende au umchukie, umkatae au umkubali, umpinge au umuunge mkono Dkt. Wilbrod Slaa Dr Willibrod Slaa anabakia kuwa miongoni mwa wanasiasa wachache Tanzania ambao alama zao katika zama na nyakati za kisiasa ni vigumu kufutika. Unaweza kumuita majina mengi na ya rangi mbalimbali ya kejeli lakini ni vigumu kupuuzia, kudharau au kutupilia mbali mchango wake katika siasa za Tanzania kwa karibu miaka ishirini na mitano. Mchango wake katika kuimarisha siasa za Tanzania akiwa miongoni mwa wabunge wa kwanza kabisa wa upinzani umeacha historia kubwa kuanzia Karatu hadi Dar, toka Tunduru hadi Tarime.

Hata hivyo, matukio ya kisiasa ya mwaka 2015 yanabakia katika historia yetu kama mafundisho makubwa kabisa ya siasa zinavyoweza kuwafanya ndugu wawe maadui, marafiki wake mahasimu, na kutengeneza kile ambacho wenzetu Wamarekani wanasema ni “strange bed fellows” yaani kuwaona watu usiowadhania wamelala kitanda kimoja. Matukio haya yalitokea taifa likiwa katika mwamko mkubwa wa uchaguzi mkuu wa Rais na Wabunge.

Dkt. Slaa akiwa Katibu Mkuu wa chama Kikuu cha upinzani cha CHADEMA, alitarajiwa na alipitishwa na chama chake kuwa mgombea wa Urais huku mtifuano mkubwa ukitarajiwa na hatimaye ulitokea ndani ya Chama cha Mapinduzi. Kwa baadhi ya wachunguzi wa siasa mtifuano au mnyukano uliokuwa unatokea CCM ulifanya kazi ya mgombea wa upinzani uliounganika kuwa ya afueni zaidi.

Hata hivyo, kinyume na matarajio ya watu wengi na kinyume na mantiki zilizozoeleka za kisiasa Edward Lowassa aliyekatwa jina lake ndani ya CCM ambako alikuwa anaongoza kwa mashabiki na kura za maoni alikimbilia CHADEMA na kusababisha chama hicho cha upinzani kulala kitanda kimoja na mtu ambaye walitumia muda mwingi kumhusisha na ufisadi nchini. Ilisemwa “yeyote” isipokuwa CCM. Dkt. Slaa akafyekelewa mbali na chama chake na kusababisha mpasuko wa aina yake ndani ya CCM na CHADEMA.

Dkt. Slaa akaamua kuachana na siasa za vyama na yeye na familia yake wakahamia Canada. Miezi michache baadaye Rais John Magufuli alimteua Dkt. Slaa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Sweden kitu ambacho kilitafsiriwa na baadhi ya watu kwa namna mbalimbali.

Katika kitabu cha NYUMA YA PAZIA Dkt. Slaa anaelezea kwa kina matukio mbalimbali ambayo yalitokea hadi kufikia Lowassa kukaribishwa CHADEMA na kwa nini hakuwa tayari kusimama jukwaani kumnadi Lowassa na akabakia na utimamu wa kimaadili na akili. Hata hivyo, kitabu hiki kinaenda zaidi ya nyuma ya pazia la siasa za 2015. Inatufunulia kumuelewa Dkt. Slaa kwani kwa kiasi chake kitabu hiki pia ni bibliografia (historia ya maisha) ya mwanasiasa huyu nguli, mcheshi, na msomi.

Ndani ya kitabu hiki tunaweza kukutana na mtu ambaye anatufundisha mambo mbalimbali kuhusiana na uongozi. Mojawapo ya mambo ambayo msomaji atayafurahia atakapokutana nayo ni jinsi gani Dkt. Slaa ni mtunzaji mzuri sana wa kumbukumbu. Siyo tu katika akili lakini katika nyaraka na vielelezo mbalimbali. Anataja tarehe, mahali na siku kama shahidi katika kesi nzito. Bila utata anataja pia majina mbalimbali ya wahusika mbalimbali katika ujasiri ambao utawakumbusha watu wengi ile hotuba yake ya “Orodha ya Mafisadi” ya pale Mwembe Yanga.

Kitabu hakigusi siasa tu za 2015 lakini pia kinatudokeza safari ya Dkt. Slaa kutoka upadre hadi kuwa mwanasiasa mbobezi. Wengi watashtushwa, kushangazwa na kuburudishwa na masimulizi yake ya mikutano yake na Baba wa Taifa Mwl. Nyerere wakati huo Dkt. Slaa akiwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu. Pia watakutana na jinsi gani Dkt. Slaa alisimamia kupinga ufisadi ndani ya Kanisa Katoliki kiasi cha kumgonganisha yeye na mmojawapo wa maaskofu waandamizi wa wakati huo. Msomaji pia ataburudishwa na masimulizi yake ya kujaribu kuinua hali na maisha ya watu wa Karatu katika kile ambacho kilimsababishia kuwa mbunge mpendwa sana wa wana Karatu na kuthubutu kufanya kitu ambacho hakikuwahi kufanywa Tanzania – Karatu kuwa Halmashauri ya kwanza ya mji kuongozwa na upinzani.

Kubwa hata hivyo, ni sakata zima la siasa za 2015 na matokeo yake katika upinzani na siasa za Tanzania. Kitabu hiki kinatoa maonyo, mwongozo, na elimu kwa wanasiasa wanaofuatia katika upinzani na chama tawala na wapinzani watarajiwa na watawala watarajia. Mwanasiasa yeyote ni lazima apate nakala ya kitabu hiki, mwanahistoria yeyote ni lazima anunue nakala yake wakati wanafunzi wa shule na vyuo watapata elimu muhimu juu ya uongozi kutoka katika kitabu hiki kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili.

Nyuma ya pazia ni kitabu kinachomfunua mbele yetu na kutujulisha kwa undani juu ya mtu, maisha, zama na nyakati za Dkt. Wilbrod Slaa, Balozi, Baba, Mume na miongoni mwa viongozi maridadi ambao Tanzania imepata nafasi ya kuwa nao na wameacha alama zisizofutika. Umpende au umchukie, umkatae au umkubali, umpinge au umuunge mkono Dkt. Wilbrod Slaa ametupatia hazina ya maarifa ambayo wenye hekima watawahi kuipata katika nakala chache ambazo zimeshaingia nchini.

UNAWEZA KUPATA NAKALA YAKO WAPI?
Unaweza kupata nakala yako kwa bei ya jumla au rejareja. Bei ya reja reja ni shilingi 20,000/- TU na kwa bei ya jumla unaweza kupata punguzo kubwa kufuatana na mahitaji yako.
Maeneo ya posta, mkabala na Jengo la Benjamin Mkapa karibu na Mahali yanapoegeshwa magari yaendayo Sinza yenye michoro ya Rangi Nyekundu.
Mhudumu Genoveva - 0753 059 144
Au wasiliana na Erasto Tumbo kuweza kuagiza nakala zako:
0713 474707/0688 211683
 
(Pichani kitabu kikianza kupatikana kwa Wabunge, Dodoma)

Na. M. M. Mwanakijiji

Umpende au umchukie, umkatae au umkubali, umpinge au umuunge mkono Dkt. Wilbrod Slaa Dr Willibrod Slaa anabakia kuwa miongoni mwa wanasiasa wachache Tanzania ambao alama zao katika zama na nyakati za kisiasa ni vigumu kufutika. Unaweza kumuita majina mengi na ya rangi mbalimbali ya kejeli lakini ni vigumu kupuuzia, kudharau au kutupilia mbali mchango wake katika siasa za Tanzania kwa karibu miaka ishirini na mitano. Mchango wake katika kuimarisha siasa za Tanzania akiwa miongoni mwa wabunge wa kwanza kabisa wa upinzani umeacha historia kubwa kuanzia Karatu hadi Dar, toka Tunduru hadi Tarime.

Hata hivyo, matukio ya kisiasa ya mwaka 2015 yanabakia katika historia yetu kama mafundisho makubwa kabisa ya siasa zinavyoweza kuwafanya ndugu wawe maadui, marafiki wake mahasimu, na kutengeneza kile ambacho wenzetu Wamarekani wanasema ni “strange bed fellows” yaani kuwaona watu usiowadhania wamelala kitanda kimoja. Matukio haya yalitokea taifa likiwa katika mwamko mkubwa wa uchaguzi mkuu wa Rais na Wabunge.

Dkt. Slaa akiwa Katibu Mkuu wa chama Kikuu cha upinzani cha CHADEMA, alitarajiwa na alipitishwa na chama chake kuwa mgombea wa Urais huku mtifuano mkubwa ukitarajiwa na hatimaye ulitokea ndani ya Chama cha Mapinduzi. Kwa baadhi ya wachunguzi wa siasa mtifuano au mnyukano uliokuwa unatokea CCM ulifanya kazi ya mgombea wa upinzani uliounganika kuwa ya afueni zaidi.

Hata hivyo, kinyume na matarajio ya watu wengi na kinyume na mantiki zilizozoeleka za kisiasa Edward Lowassa aliyekatwa jina lake ndani ya CCM ambako alikuwa anaongoza kwa mashabiki na kura za maoni alikimbilia CHADEMA na kusababisha chama hicho cha upinzani kulala kitanda kimoja na mtu ambaye walitumia muda mwingi kumhusisha na ufisadi nchini. Ilisemwa “yeyote” isipokuwa CCM. Dkt. Slaa akafyekelewa mbali na chama chake na kusababisha mpasuko wa aina yake ndani ya CCM na CHADEMA.

Dkt. Slaa akaamua kuachana na siasa za vyama na yeye na familia yake wakahamia Canada. Miezi michache baadaye Rais John Magufuli alimteua Dkt. Slaa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Sweden kitu ambacho kilitafsiriwa na baadhi ya watu kwa namna mbalimbali.

Katika kitabu cha NYUMA YA PAZIA Dkt. Slaa anaelezea kwa kina matukio mbalimbali ambayo yalitokea hadi kufikia Lowassa kukaribishwa CHADEMA na kwa nini hakuwa tayari kusimama jukwaani kumnadi Lowassa na akabakia na utimamu wa kimaadili na akili. Hata hivyo, kitabu hiki kinaenda zaidi ya nyuma ya pazia la siasa za 2015. Inatufunulia kumuelewa Dkt. Slaa kwani kwa kiasi chake kitabu hiki pia ni bibliografia (historia ya maisha) ya mwanasiasa huyu nguli, mcheshi, na msomi.

Ndani ya kitabu hiki tunaweza kukutana na mtu ambaye anatufundisha mambo mbalimbali kuhusiana na uongozi. Mojawapo ya mambo ambayo msomaji atayafurahia atakapokutana nayo ni jinsi gani Dkt. Slaa ni mtunzaji mzuri sana wa kumbukumbu. Siyo tu katika akili lakini katika nyaraka na vielelezo mbalimbali. Anataja tarehe, mahali na siku kama shahidi katika kesi nzito. Bila utata anataja pia majina mbalimbali ya wahusika mbalimbali katika ujasiri ambao utawakumbusha watu wengi ile hotuba yake ya “Orodha ya Mafisadi” ya pale Mwembe Yanga.

Kitabu hakigusi siasa tu za 2015 lakini pia kinatudokeza safari ya Dkt. Slaa kutoka upadre hadi kuwa mwanasiasa mbobezi. Wengi watashtushwa, kushangazwa na kuburudishwa na masimulizi yake ya mikutano yake na Baba wa Taifa Mwl. Nyerere wakati huo Dkt. Slaa akiwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu. Pia watakutana na jinsi gani Dkt. Slaa alisimamia kupinga ufisadi ndani ya Kanisa Katoliki kiasi cha kumgonganisha yeye na mmojawapo wa maaskofu waandamizi wa wakati huo. Msomaji pia ataburudishwa na masimulizi yake ya kujaribu kuinua hali na maisha ya watu wa Karatu katika kile ambacho kilimsababishia kuwa mbunge mpendwa sana wa wana Karatu na kuthubutu kufanya kitu ambacho hakikuwahi kufanywa Tanzania – Karatu kuwa Halmashauri ya kwanza ya mji kuongozwa na upinzani.

Kubwa hata hivyo, ni sakata zima la siasa za 2015 na matokeo yake katika upinzani na siasa za Tanzania. Kitabu hiki kinatoa maonyo, mwongozo, na elimu kwa wanasiasa wanaofuatia katika upinzani na chama tawala na wapinzani watarajiwa na watawala watarajia. Mwanasiasa yeyote ni lazima apate nakala ya kitabu hiki, mwanahistoria yeyote ni lazima anunue nakala yake wakati wanafunzi wa shule na vyuo watapata elimu muhimu juu ya uongozi kutoka katika kitabu hiki kilichoandikwa kwa lugha ya Kiswahili.

Nyuma ya pazia ni kitabu kinachomfunua mbele yetu na kutujulisha kwa undani juu ya mtu, maisha, zama na nyakati za Dkt. Wilbrod Slaa, Balozi, Baba, Mume na miongoni mwa viongozi maridadi ambao Tanzania imepata nafasi ya kuwa nao na wameacha alama zisizofutika. Umpende au umchukie, umkatae au umkubali, umpinge au umuunge mkono Dkt. Wilbrod Slaa ametupatia hazina ya maarifa ambayo wenye hekima watawahi kuipata katika nakala chache ambazo zimeshaingia nchini.

UNAWEZA KUPATA NAKALA YAKO WAPI?
Unaweza kupata nakala yako kwa bei ya jumla au rejareja. Bei ya reja reja ni shilingi 20,000/- TU na kwa bei ya jumla unaweza kupata punguzo kubwa kufuatana na mahitaji yako.
Maeneo ya posta, mkabala na Jengo la Benjamin Mkapa karibu na Mahali yanapoegeshwa magari yaendayo Sinza yenye michoro ya Rangi Nyekundu.
Mhudumu Genoveva - 0753 059 144
Au wasiliana na Erasto Tumbo kuweza kuagiza nakala zako:
0713 474707/0688 211683
Mwanakijiji Slaa anakula, tukiwa tunakula Africa hatuongei tukiongea ni kwa ruhusa ya baba au mama. Huyu (sijasoma na sitasoma kitabu hicho) ameandika kusifia Jiwe, most likely, ANAKULA, HARUHUSIWI "KUONGEA"
 
AANDIKE KILICHOMTOA KWENYE UPADRE BLAA BLAA ZINGINE NI KUPOTEZA WAKATI, YEYE ANA LAANA.YA YESU
 
Ndiyo kinyesi kimerudi chooni ambako na yeye yuko. Kumbe alisema ivyo kwa kuwa alijua mwisho wa siku atarudi chooni?

Sebule imeshakuwa safi, jee choo kinaweza kugeuka kuwa chumba cha kulala ama sebule?
harufu bado ipo sebleni; mjifunze kuishi kwa misingi.
 
Back
Top Bottom