Kwahiyo alivyokataa ushauri wake akaamua kumnyonga! Sidhani kama ni kweli.Alinyongwa, Mwalimu alimsihii akane awe aliua bila kukusudia alikataa katu. Dr. Kreluu alikua mwasherati wa kutembea na watoto pia wake za watu. Adabu aliipata, shujaa Mwamwindi..
iliyo mnyonga ni sheria ya nchi mzee, au hujui kama rais still yuko chini ya katiba!Kwahiyo alivyokataa ushauri wake akaamua kumnyonga! Sidhani kama ni kweli.
Kuna watu wamehukumiwa kunyongwa lakini imeshindikana kunyongwa kwa sababu rais hajasaini hukumu kutekelezwa au hujui? Kwahiyo angetaka hasinge nyongwailiyo mnyonga ni sheria ya nchi mzee, au hujui kama rais still yuko chini ya katiba!
Mkuu hebu funguka, niliwahi kuwaukiza wenzangu same question why alienda mwenyewe? Why ali drive mwenyewe?
Munyalukolo mwamwindi akakamata riffle akasema this my riffle, this my gun, tis for fighting, this for fun. Akamtandika Dr kleruu akarest in peace.......
Uoga upi wa kuishi nyumba hiyo? Alafu naona kama nyumba imetelekezwa kama gofu vile. Watenge bajeti waikarabati watumishi wa serikali wanahangaika na uhaba wa nyumba za umma
..Magufuli hakuipiga bei hiyo nyumba?
..nashangaa kwanini mafisadi hawakuiona hiyo nyumba wakainunua kipindi kile Dr.Magu anauza nyumba za serikali.
Cc Bukyanagandi
Mkuu J.kuu, kitu cha kwanza wanasema ina mizimu sijui ghost ya mtu gani - watu uogopa kuinunua inanikumbusha English farmhouse.
Tukija suala la Dk.Magufuli tukumbuke yeye alikuwa ni mtekelezaji wa amri za Waziri mkuu one F. Sumaye na Rais - kama nakumbuka vizuri Sumaye aliwahi kusema kwamba yeye ndiye anaweza kuwapa ufafanuzi wa kina kuhusu uuzwaji wa nyumba za Serikali kwa seating tenants ambao ni waswahili wenzenu, je, wangewauzia matajiri/ wafanya biashara tungeweza kulalamika kweli? - Ukweli ni kwamba tungekaa kimya.
Binafsi huwa sielewi upinzani mkubwa wa zoezi hili, mashirika mengi yaliwauzia nyumba wafanyakazi wao mfano: Tazara na Bandari just 2 mention a few sasa tatizo ni nini hasa - nikisema labda tatizo ni la kisaikolojia zaidi yaani la "KWA NINI" je, ntakuwa nimekosea?
Siyo kwamba watu wana uchungu wa kweli wa nyumba hizo kuuzwa kwa Watanzania wenzao, nyumba zenyewe za enzi za ukoloni nyingi zinahitaji facelift ya kufa mtu - nikienda nikaziagalia zinazidiwa na nyumba iliyo jengwa na mzee wangu kijijini mwaka 1946 ingawa vigae zinafanana.
Sasa lawana kubwa kwa nini huwa inaelekezwa kwa mtu mmoja, huwa sijui kwa nini members wengi wa JF upenda sana ku - "KILL THE MESSENGER" (JPJM) na kuwahacha Waziri mkuu, Rais na baraza lote mawaziri - it was a collective decision I guess - why pick on Dk.Magufuli if I may ask?
..it was a collective decision lakini Magu ndiye alikuwa mtekelezaji.
..ppl want to get to the bottom of this issue na ndiyo maana wanamchokonoa huyu bwana.
..ni kweli nyumba zile zilikuwa zimechakaa. Lakini je ingekuwa mali binafsi ya Magu angeuza kwa bei ile ya hasara??
..je walikuwa hawajui kwamba wanakwenda kuitia nchi hasara?
..HASARA hiyo ndiyo inayowafanya wengi tuhoji uhalali wa zoezi lile.
Mkuu J.Kuu, watu wanacho sahau ni kwamba kinacho fanyika ni kwamba unangalia nyumba ulijengwa kwa gharama gani, je tangu wakazi/tenants waanze kulipa kodi, je, sum total ya kodi over the years ilishavuka return of investment na kuhanza kuvuna faida au la?
Tukiweka maanani kwamba nyumba hizo zilijengwa zamani sana ni dhahili ziliisha jilipa na faida juu, hivyo Serikali ikiwahuzia wapangaji kwa bei ya kawaida haitapata hasara after all lengo la Serikali lilikuwa ni kuwawezesha wapangaji kumudu kununua nyumba hizo kwa bei ndogo siyo Serikali kupata faida ya ziada.
Zamani hata National Housing Corp iliwahi kuwauzia tenants nyumba, hata Ulaya specifically Uingereza huwauzia wapangaji Council flats bila ya kujali kama mpangaji ni raia au la - what counts ni hela yako tu.
Kwa hiyo suala hili ya nyumba za Serikali tusilivalie njuga sana, hakuna haja ya kulichukulia kama ni suala la uhaini vile, mimi mpaka sasa nina imani kwamba Serikali ilikuwa na nia safi kuwauzia wapangaji nyumba.
Aise! ni HATARI ndugu.Ninaposoma kauli za wadau hapa ninapatwa na hofu sana. Ndani ya mioyo ya watu yapo mengi sana. Ukipewa uwezo wa kuyaona unaweza bakia umejifungia ndani..
wengine wana roho za ajabu sana ndugu.Aisee ninanusa harufu ya uchochezi kwenye post yako hii Mkuu! Umejipangaje?
Wewe ndo unayepotosha. Toka lini mkuu wa mkoa akaenda oparesheni peke yake, na gari la ofisi, bila walinzi hata dereva!!!!
Fikiria mara mbili kabla ya kuubishia ukweli
Kaka usipate tabu watoto wengi wa juzi humu JF. Mbaya zaidi, hawapendi kusoma wao hukurupuka kwa conclusion zao bila kuulisha ubongo vema maarifa.Someni kisa hicho kipo gazeti la mwananchi la wiki hii yote...
Wacheni kupotosha.
Mwamindi alikua shujaa pekee aliepinga siasa za ujamaa za kunyanganya watu mashamba yao na kuwataka watu kulima ujamaa