Nyumba aliyoishi RC wa Iringa Dr. Kleruu kabla ya kuuawa na Said Mwamwindi

Nyumba aliyoishi RC wa Iringa Dr. Kleruu kabla ya kuuawa na Said Mwamwindi

Hata Said Mwamwindi 'kosa lake' ni kulima zao lisilotakiwa kulimwa lakin hakukimbilia 'ITV' matokeo yake alitafakari akachukua Hatua
Km tumejiwekea sheria alafu hatuwezi kuzitii.kulikua hakuna haja ya kuwa na sheria au kutenga maeneo hasa ya hifadhi.je ungependa wapigane? Sheria ya hifadhi za taifa zinasemaje? Nchi inapozidi kupata wasomi tutarajie uelewa uongezeke na si vinginevyo.
Tuwasaidie wananchi kuhusu haki wajibu wao km raia wema
 
H
Dr. Kleruu wapo wengi sana Nyakati hizi ila Majasiri kama akina Said Mwamwindi hawapo!!
Huyu Mkulima alimtandika Risasi RC akamtia kwny Trekta lake akampeleka kwa RPC akamwambia nimewaletea Mzoga Wenu.
Juzi kati hapa Mgambo tu wa TANAPA wameharibu mashamba ya Mahindi zaid ya heka 400 huko Mbeya kisa wamelima kwenye Hifadhi, halafu wanakijiji wanakimbilia ITV !!!
ahahahahahahahahaaaa!!!!
 
Dr. Kleruu wapo wengi sana Nyakati hizi ila Majasiri kama akina Said Mwamwindi hawapo!!
Huyu Mkulima alimtandika Risasi RC akamtia kwny Trekta lake akampeleka kwa RPC akamwambia nimewaletea Mzoga Wenu.
Juzi kati hapa Mgambo tu wa TANAPA wameharibu mashamba ya Mahindi zaid ya heka 400 huko Mbeya kisa wamelima kwenye Hifadhi, halafu wanakijiji wanakimbilia ITV !!!
Haya maneno yanatoka kwako ndugu yangu??
 
hapana mwamindi alikua anapinga kuchukuliwa mke wake mdogo na Dr. Kleruu
Ni kweli, Dr. Kleruu hakuwa na ethics. Siku hiyo ya krismas aliyokumbwa na mauti aliondoka kwenda kumchukua yule mwanamke wa mzee Mwamwindi bila hata kuwa na dereva wala askari mlinzi. Kwa bahati mbaya alipofika pale akamkuta mzee Mwamwindi mwenye mali mwenyewe akiwa yupo nyumbani. Yaliyobaki leo ni historia tu.
 
Na mimi ndivyo nilivyo adithiwa, wa lisema siku yenyewe ilikuwa ni Chrismas kama nakumbuka vizuri.

Inaelekea Dk. Kleruu (RIP) alipata taarifa kuhusu Mwamwindi kuwepo shambani kwake akiwa na wafanyakazi wake - nadhani mwaka huo ndio itikadi za ujamaa zilikuwa zimepamba moto nchini, mabepari wakawa wanafananishwa na wanyama,wakaitwa wanyonyaji, wanaibwa kwa nyimbo za kejeri na chuki - yaani wananchi walikuwa primed kuwaona mabepari kama ni wabaya kuliko wakoloni.

Misimamo ya kuchukia Ubepari nchini ilikuwa ina walakini sana, kuna baadhi ya wananchi waliokuwa na uwezo kifedha walipata wakati ngumu sana kwa kunyaganywa mali zao walizo chuma kwa jasho lao!!

Atittude zilizokuwa zimejengeka wakati huo ndizo zilimpa jeuri Dk.Kleruu kwenda kumudhihaki/dhalilisha Mr.Mwamwindi skiwa shambani kwake - kisa? Mwamwindi ni bepari, eye witness walisema walimuona Dk.Kleruu ameshikilia kifimbo akikisukuma sukuma kwenye tumbo la Mwamwindi - hakuna mwanamume worthy his salt angeweza kuvumilia provocation ya kiwango hicho - alicho kosea Mwamwindi ni kule kwenda kuchukua Rifle kutoka nyumbani kwake na kurudi shambani kumpiga risasi Dk.Kleruu - sasa time lag ya kutoka shambani kwenda nyumbani kuchukua bunduki na kurudi tena shambani hasira zilipashwa kuwa zimepungua ndio maana mahakama ilimuhukumu kunyongwa kutokana na kuonekana kwamba iliuua kwa kukusudia "murder case"

Ile ilikuwa sera yakutaifisha mali za waislamu wengi waliojaa mijini na vijijini hasa Dar, kumbuka huko maporini shinyanga na kigoma kulikuwa na simba na mafisi tu ndio wametawala. Mfano likaundwa shirika la nyumba ili kujimilikisha nyumba za waislamu waliowengi.

Kama Mwamwindi angekuwa na bunduki shambani alafu Dk.Kleruu akaja akamu-provoke hapo angehukumiwa kuua bila ya kukusudia akafungwa kwa muda.
 
Ni kweli, Dr. Kleruu hakuwa na ethics. Siku hiyo ya krismas aliyokumbwa na mauti aliondoka kwenda kumchukua yule mwanamke wa mzee Mwamwindi bila hata kuwa na dereva wala askari mlinzi. Kwa bahati mbaya alipofika pale akamkuta mzee Mwamwindi mwenye mali mwenyewe akiwa yupo nyumbani. Yaliyobaki leo ni historia tu.

Na huo ndio ukweli usiosemwa!!
 
Dr.Kleruu alipigwa Risasi Shambani kwa Mwamwindi akiwa Kaenda kumzuia asilime Mazao anayoyataka badala yake alime zao la biashara kwa Gharama zake halafu akawauzie vyama vya ushirika kwa bei waliyojipangia serikali halafu watalipa siku wakijiskia, hata Risasi alipigiwa shambani sio gesti wala kitandani.
Enzi zile ni enzi za Propaganda kama uliweza kuaminishwa Iddi Amin anakula watu na wewe ukaamini huwezi kuacha kuamini uongo eti kisa Kilikuwa uzinzi!
Hii siyo kweli, Mwamwindi hakwenda shamba na gobole lake alilotumia kufanya mauaji. Dr Klerru alipigwa gololi la gobole kifuani akiwa nyumbani kwa Mwamwindi, ndipo mzee huyo akavuta mwili huo na kuuweka ndani ya buti la ile Peugeot 404 ya mkuu wa mkoa aliyokuwa amekuja nayo ikiwa na bendera taifa na kwenda polisi mkoani akiwa na gobole alilotumia kummaliza mwizi wa mke wake.

Dr. Kleruu aliponzwa na ufuska wake!
 
Mwamwindi hakika ni shujaa anayetakiwa kuenziwa. Nadhani historia yake iwekwe vizuri sio kupindishwapindishwa, hii ni moja ya cost na laana zilizoletwa na UJAMAA, R.I.P nyerere on the other side
 
Upo sahihi kabisa Isimani imekua kama jangwa nlipita kwa babu kijiji cha Matembo nikaoneshwa mashamba yake ya zamani ambayo yalitaifishwa enzi hizo yamebaki pori tuu
mi ni mzaliwa wa matembo babu yako ni nani?
 
Dr. Kleruu wapo wengi sana Nyakati hizi ila Majasiri kama akina Said Mwamwindi hawapo!!
Huyu Mkulima alimtandika Risasi RC akamtia kwny Trekta lake akampeleka kwa RPC akamwambia nimewaletea Mzoga Wenu.
Juzi kati hapa Mgambo tu wa TANAPA wameharibu mashamba ya Mahindi zaid ya heka 400 huko Mbeya kisa wamelima kwenye Hifadhi, halafu wanakijiji wanakimbilia ITV !!!



Mimi nipo ila hawajafika shambani kwangu nitawafanya kama mwanaCCM mwenzao


ila umechapia mkuu hakumuweka kwenye trecta yake ila alitumia gari ya marehemu na hakumpeleka kwa rpc ila kituoni alimkuta askari kijana mmoja hivi
 
Mimi nipo ila hawajafika shambani kwangu nitawafanya kama mwanaCCM mwenzao. ila umechapia mkuu hakumuweka kwenye trecta yake ila alitumia gari ya marehemu na hakumpeleka kwa rpc ila kituoni alimkuta askari kijana mmoja hivi

Sasa hivi "yule kijana" Ni Mzee. Ni mstaafu.Ni Mzazi wa Wana michezo walio pata kutamba hapa nchini. Mmoja kwenye Soka na mwingine kwenye Mpira wa Pete..Huyu "Askari kijana mmoja hivi.." bado yu hai..
 
Mwamwindi alihukumiwa kunyongwa hadi kufa maana waliprove kosa la kuuwa kwa kukusudia
inasemekana jamaa alikuwa na bifu vilevile, mkulu huyo alikuwa anambandulia moja wapo wa wake zake, kun asiri nzito inavyosemekana.
 
Sasa hivi "yule kijana" Ni Mzee. Ni mstaafu.Ni Mzazi wa Wana michezo walio pata kutamba hapa nchini. Mmoja kwenye Soka na mwingine kwenye Mpira wa Pete..Huyu "Askari kijana mmoja hivi.." bado yu hai..
Asante kumbe yako mengi sana
 
Majid Mjengwa

Bongo Hapo Zamani: Hii Ndio Nyumba Namba Moja Iringa!
-Ni ' Ikulu Ndogo' Aliyoishi RC Dr Kleruu Aliyeuawa Na Mkulima Said Mwanwindi

Ndugu zangu,
Picha hii niliipiga mwaka juzi.

Ikulu Ndogo ya zamani ya Iringa, kwa maana ya makazi ya RC, imejengwa na Mjerumani mwaka 1906. Ndivyo inavyoonekana mpaka leo.

Ina master-bedroom. Bedroom tatu. Chumba cha kusomea , sebule kubwa, jiko na stoo. Style yake haijabadilishwa tangu Dr Kleruu aiache; madirisha, milango, ukuta na paa ni ile ile.

Baada ya kuuawa kwa Dr Kleruu ma- Rc waliofuata ni kama walikuwa na woga nayo.

Inasimuliwa, kuwa enzi za RC Dr Kleruu, alikuwa akisimama hapo mbele ya nyumba yake na kuongea na wananchi. Nyumba iko mlimani na mji wa Iringa unauona ukiwa kwenye baraza ya Ikulu Ndogo.

Kwanini nyumba hii inaogopewa?

Ni abrakadabra, si kitu kingine. Mfano, Serikali imegharakia kujenga nyumba ya DC Iringa wakati hiyo hapo pichani DC angeweza kukaa.

Shida ukimweka DC au RC hapo, usishangae DC mzima akaamka asubuhi moja kutaka kuhama nyumba au kuhamishwa mkoa kabisa, kisa? Atakwambia usiku amemwona Mkulima Mwamwindi anamjia na bunduki yake mkononi!

Naam, ingawa hivyo, kwa nyakati tofauti nyumba hiyo imetumiwa na jeshi. Si wengi Iringa wenye hata kujua ilipo nyumba hii muhimu iliyokuwa ya Serikali na yenye kumbukumbu muhimu ya kihistoria.

Nami nimeipiga picha hiyo kuhifadhi kumbukumbu hiyo, maana siku hizi majengo kama haya ambayo ni hazina kwa taifa hayakawii kuvunjwa na kujengwa maghorofa.
Maggid.
Iringa.
 

Attachments

  • FB_IMG_1526132549520.jpg
    FB_IMG_1526132549520.jpg
    23.1 KB · Views: 127
Nashangaa huyu Dr Kleruu kuazimishwa kama miongoni mwa mashujaa wa Taifa hili wakati aliuwawa kwa kua alikua anawaletea kero watu na hasa wanamji wana Iringa kindakindaki, wakulima wakubwa. Alimletea dharau Mzee Mwamwindi. Inasemekana Kleruu alikua akitembea na mke wa Mzee Mwamwindi na Mzee alikua najua. pamoja na hayo Kleruu alikua anam harass sana Mzee Mwamwindi kwa maneno ya kashfa,Mzee mwisho akaamua kuondoa udhia kwa mikono yake
 
Back
Top Bottom