Nyumba zaidi ya 30 za Kitanzania ambazo waweza chagua kujenga kulingana na bajeti yako

Nakopa million kumi bank af kwa mtu nakopa million sita nataka mnijengee hiyo ya vyumba vitatu...ila BADO Sina kiwanja nipeni muda nitafute.
 
Mkuu unamaanisha hiyo milioni 16 nyumba inatoka kama hiyo ya kwenye picha...?

Nikimaanisha kila kitu kinakuwa tayari bado kuhamia tu au inakuwa bado finishing kiongozi...?
Kwa nilivyosoma hapo, hiyo bei iliyowekwa inajumuisha Design+Map+Foundation+Wall+Roof. Kwa kifupi hizo gharama zinaishia kwenye kupaua tu.
 
Heading amesema unahamia kwa gharama ya 8m.

Sasa hii hoja yako hebu inyooshe
 
Mkuu kwa uzoefu wangu katika ujenzi siku zote gharama za ujenzi hutegemea;

1. Landscape ya kiwanja chako kama kipo tambarare, bondeni au kilimani.

2. Umbali na upatikanaji wa materials kama maji, mchanga, kokoto, cements, mbao, mabati, nondo n.k hadi kufika hapo site kwako.

ANGALIZO.
Usiaminishe watu bei za kitonga mwisho wa siku ukaja kuonekana tapeli na ukizingatia bei ya materials hivisasa ipo juu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…