Nywele zinavyohusishwa na roho na mapepo

Kuna imani wanajiita waaminio hawa mwanamke hanyoi nywele kaka angu binti zake hawakatwi nywele za utoto wanakuwa nazo wana nywele refu sana sasa sijui wanaungana na nini
 

Mkuu majeshi yanazindiko lake amin usiamin zile stail Zao za kutembea kusalimiana n.k znamaana yake kubwa sana kwahyo hata nywele znamaana yke
 
pia kuna kitu watu huishndwa gundua au huchukulia poa. Kuna kitu kikubwa cha kiimani katika kitu chochote ambacho unakimiliki maana kimebeba uniq identity yako. So huweza tumika kukupata fasta tu, kaam ilivyo mtu akijua majina yako yako matatu, au majina ya mama yako, kwisha kazi sembuse nywele au kucha.

Pia ladies kuwa makini sana na huu mchezo wa ku attach nywele za watu wenhine kichwani kwako, ni hatari mno mshana jr eleza kidogo hapa maana wengine kueleza ni kipaji
 
Last edited by a moderator:
Ni kumi kwa moja halafu asilimia kubwa ni hiki kizazi chetu wazee wa zamani huthubutu kumuacha mtoto na nywele alizotoka nazo tumboni

Hii sabrinah..
Mara nyingi kiimani nywele za mtoto mchanga zinanguvu sana katika mambo ya kichawi. Mara nyingi nywele huashiria ufahamu wa mtoto. Zamani wengi nywele zilichukuliwa na kufanyiwa mila au matambiko. Kufanya hivyo unamfunga mtoto ufahamu wake unamkabidhi over the other side. Si lazima kumnyoa mtoto nyewele zake na hata zikinyolewa zikatupwe mahali mtu mbaya haezi fukia.
mfano mchawi anapomnyoa mtoto hata wa secondary nywele anaweza kuhamisha ufahamu wake na akili yake kwa mtu mwingine ndipo unaanza kusema mtoto amekuwa mjinga ghaflaa au ameanza kufeli ghaflaa tu. Ukiona hivyo jua kuna jambo.

Tukienda nje ya mada kitovu nacho huashiri uhai wa mtu na nafsi yake wengi wamefungwa kozi vitovu vilifanyiwa mila. So ni vyema kumnyoa mtoto mwenye na kitovu chake ukipe mwenye baada ya kukuombea.
 
yaani nikifungua uzi niaona mwanzilishi jina linasoma Mshana jr roho inaanza kudunda najua sasa nahamishwa duniani sasa kumekucha haya twende kikore
 

Hapo nimekupata ila kwa sasa sijui kama kuna anaeamini haya maana hata ule mvuje anaovalishwa mtoto kuepusha kushituka watu wakimuona unaambiwa mvue mtoto hirizi
 
Mkuu tangaza nia!!
 
Hapo nimekupata ila kwa sasa sijui kama kuna anaeamini haya maana hata ule mvuje anaovalishwa mtoto kuepusha kushituka watu wakimuona unaambiwa mvue mtoto hirizi

Ndio yamepungua ila yapo na yanatokea sana. Huoni pande zingine huwa wanshupalia sana kitovu, kucha au nywele apewe bibi?! Unajua zapelekwa wapi au wanafanyia nini? Tunayapotezea ila wachawi wanatumia sana hivi vitu. Hata mimi nasemaga ni hirizi maana naamini mwenye uwezo wa kukinga mtoto na macho mabaya au mambo ya imani mbaya ni mungu pekee sio kitu cha kutengenezwa na binaadam. Muhimu ni wewe kama mama kuwalinda wanao kimwili na kwa kumuomba mungu atakecare ya yale usioweza pigana nayo through sala na sadaka.
 
Ndomaana nivizuri baada ya kunyoa nywele uzichimbie na kuzifukia, ila kabla unatakiwa uangalie kushoto na kulia kama kuna anaye kuona. Kama hayupo fukia kisha sepa!!

Roho zinazo tangatanga zinakuona, usidhani unaweza kujilinda mwenyewe, huna huo ujanja (only God can..) mara nyingi umeacha nywele zako saloon wakati hata kinyozi humjui..
 
Sio nywele tu...
Kitu chochote kinachotoka mwilini mwako kinakuwa kimebeba DNA yako...
DNA ni kama formula ya mwili wako, ni sawa na hackers wabebe system file la program yako...
Wachawi ni hackers ambao wanahack DNA system yako...

Ndugu hapa umezungumza jambo la kitaalamu sana. Naenda fanya study in this, biblical and other rellated books.
 
Kwa mambo kama haya bila ulinzi wa Mungu mwanadam hakika hafurukuti
Nakumbuka kule kwetu uchagani ukitokea msiba siku ya 3 au ya 4 baada kuzika inaitwa siku ya kuanua tanga na nilazima kila mwana ndugu mhusika wa karibu anyolewe nywele sahem karibu na paji la uso na kisha kuzichimbia sehemu. mshana jr hii ina weza husika na na ulichokisema au ni kawaida tu?
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…