ubongokid
JF-Expert Member
- Apr 30, 2017
- 2,154
- 4,184
Habari za wakati huu;
Ni matumaini yangu kwamba mnaendelea vyema na majukumu yenu ya Ujenzi wa Taifa letu hili tukufu la Tanzania. Kwa wale ambao wanaifahamu Siasa sidhani kama hili la Paul Makonda kuwa Mwenezi wa Chama ni Jipya na la kushangaza kwao. Actually, kama wakisoma alama za nyakati vizuri basi wataona kwamba uelekeo ni kwamba kuna mabadilko yanaendelea.
Najua kichwa cha mada yangu kina sauti ya kejeli ila sio lengo la mada hii kukejeli bali nataka tujadili katika misingi ya maslahi mapana ya nchi,chama na serikali.Katika Nchi yetu,Chama Ndio kinashika hatamu.
Katika Siasa za Nchi yetu Paul Makonda Alifika katika hatua ya kisiasa ambayo kwanza ilimjengea profile kubwa, ilimjengea maadui na ilimjengea marafiki. Ila ni ukweli usiopingika kwamba Yeye Binafsi alibeba sifa za aina ya viongozi ambao Watanzania wanawapenda, wanawahitaji na ambao wanawafaa watanzania. Viongozi ambao wanajua Fitna, wanaweza unafiki,wanaweza kusimami kile wanachokiamni na hata kama wamekosea wana uwezo wa kushawishi kwamba wao wako sahihi.
Changamoto aliyokuwa nayo Paul haikuwa kubwa na wala anguko lake la kisiasa halikuwa kubwa.Hata hivyo alichofanya baada ya kutoka kwenye Mfumo kilimtofautisha. Tetesi zinasema kwamba Alirudi shuleni kuongeza Maarifa. Alikaa kwa nyuma akiendeleza harakati zake binafsi za kisiasa huku akijaribu kwa kiwango kikubwa kutokuwa kwenye Lime light. Subira na Upole wake pamoja na changamoto za kisiasa ndani ya Chama cha Mapinduzi zikatengeneza nafasi ambayo kimsingi inaweza kumpa Paul Makonda nafasi ya ama kujijenga zaidi ndani ya chama na serikali au kujibomoa zaidi ndani ya Chama na serikali
Kama nilivoeleza katika kichwa cha mada hii kwamba Nzi akitulia anaweza kutengeneza Asali,Basi nihitimishe kwa kusema kwamba Cmrd Paul Makonda Akituliza Kichwa chake sasa hivi Anaweza kuleta mabadiliko makubwa katika siasa za nchi ndani na nje ya chama.
Aaachane na kasumba kama zile za kuwakosema heshima watu,kujikweza kupitiliza na zaidi unapopanda Juu Usivunje ngazi ulizopitia maana ndio utazitumia kushuka chini.
Nakutakia kila la heri katika utumishi wako
Ni matumaini yangu kwamba mnaendelea vyema na majukumu yenu ya Ujenzi wa Taifa letu hili tukufu la Tanzania. Kwa wale ambao wanaifahamu Siasa sidhani kama hili la Paul Makonda kuwa Mwenezi wa Chama ni Jipya na la kushangaza kwao. Actually, kama wakisoma alama za nyakati vizuri basi wataona kwamba uelekeo ni kwamba kuna mabadilko yanaendelea.
Najua kichwa cha mada yangu kina sauti ya kejeli ila sio lengo la mada hii kukejeli bali nataka tujadili katika misingi ya maslahi mapana ya nchi,chama na serikali.Katika Nchi yetu,Chama Ndio kinashika hatamu.
Katika Siasa za Nchi yetu Paul Makonda Alifika katika hatua ya kisiasa ambayo kwanza ilimjengea profile kubwa, ilimjengea maadui na ilimjengea marafiki. Ila ni ukweli usiopingika kwamba Yeye Binafsi alibeba sifa za aina ya viongozi ambao Watanzania wanawapenda, wanawahitaji na ambao wanawafaa watanzania. Viongozi ambao wanajua Fitna, wanaweza unafiki,wanaweza kusimami kile wanachokiamni na hata kama wamekosea wana uwezo wa kushawishi kwamba wao wako sahihi.
Changamoto aliyokuwa nayo Paul haikuwa kubwa na wala anguko lake la kisiasa halikuwa kubwa.Hata hivyo alichofanya baada ya kutoka kwenye Mfumo kilimtofautisha. Tetesi zinasema kwamba Alirudi shuleni kuongeza Maarifa. Alikaa kwa nyuma akiendeleza harakati zake binafsi za kisiasa huku akijaribu kwa kiwango kikubwa kutokuwa kwenye Lime light. Subira na Upole wake pamoja na changamoto za kisiasa ndani ya Chama cha Mapinduzi zikatengeneza nafasi ambayo kimsingi inaweza kumpa Paul Makonda nafasi ya ama kujijenga zaidi ndani ya chama na serikali au kujibomoa zaidi ndani ya Chama na serikali
Kama nilivoeleza katika kichwa cha mada hii kwamba Nzi akitulia anaweza kutengeneza Asali,Basi nihitimishe kwa kusema kwamba Cmrd Paul Makonda Akituliza Kichwa chake sasa hivi Anaweza kuleta mabadiliko makubwa katika siasa za nchi ndani na nje ya chama.
Aaachane na kasumba kama zile za kuwakosema heshima watu,kujikweza kupitiliza na zaidi unapopanda Juu Usivunje ngazi ulizopitia maana ndio utazitumia kushuka chini.
Nakutakia kila la heri katika utumishi wako