Kwa wale wasio ona kazi na mafanikio ya serikali yetu walau wakubwa huko wanayaona.
Kweli wahenga walisema mitume haikubaliki makwao...
Tupate habari zaidi;
Kwa wale wenye wivu.... just do it!
Kweli wahenga walisema mitume haikubaliki makwao...
Tupate habari zaidi;
RAIS wa Marekani, Barack Obama, ameisifu Tanzania kuwa ni mfano wa kuigwa katika Bara la Afrika kwa kuwa na uongozi unaojali na kusaidia maendeleo ya watu wake. Obama amesema uongozi wa Tanzania umeonesha mfano kwa nia ya dhati ya kuwasaidia wananchi kwa kuboresha huduma muhimu za kijamii.
Rais huyo ambaye kesho anaanza ziara yake ya kwanza Afrika tangu kuchaguliwa kwake kuwa Rais akianzia Ghana, alisema jana kuwa kila atakakopita ataziambia nchi hizo za Afrika ziige mfano wa Tanzania. Katika mahojiano aliyofanya na waandishi wa tovuti ya All Africa, alisema nchi hiyo haitasita kuziunga mkono nchi zinazoonesha nia thabiti ya kuwainua watu wake.
Obama ambaye aliulizwa kama kuna nchi muhimu ambazo anazipa kipaumbele katika safari zake za kutembelea Afrika, alisema nchi zote ni muhimu lakini ujumbe atakaopeleka kwa kila nchi ni kuiga mfano wa Tanzania. "Msisahau, kwamba pamoja na kwamba ninatembelea Ghana, Waziri Mkuu wa Zimbabwe, Morgan Tsvangirai na Rais Jakaya Kikwete wameshatembelea Ikulu ya Marekani.
"Bila shaka mmeona kazi nzuri iliyofanywa na uongozi wa Tanzania ya kuelekeza nguvu zake katika kutoa huduma kwa wananchi wake, na popote marafiki wanapotaka kujikwamua wenyewe, tutakuwa nyuma yao kama washirika," alisema Obama.
Alisema anaamini Afrika ina uongozi mzuri ambao unataka kwenda mbele na Marekani inataka kwenda pamoja na Bara la Afrika katika juhudi zake za kujikwamua. Rais huyo alisema ushirika anaohitaji na Afrika si tu wa kutoa misaada bali wa kufungua fursa bora zaidi za kiuchumi kati ya Marekani na Bara hilo. "Hii ina maana ni pamoja na kuimarisha uwezo wa ndani ya nchi wa kujiendeleza na kuimarisha uhusiano baina ya Marekani na nchi moja moja," alisema Obama.
Kwa wale wenye wivu.... just do it!
Last edited: