Nilikua naongea na jamaa yangu ni Daktari, alioa Mke wake pia ni Daktari, wamebahatika kupata watoto wawili, mke wake anafanya kazi NGOs, na wememwambia inabidi aende training Marekani mwaka mzima, alafu akikamilisha wanataka kufungua hospital Tanzania na yeye akae kama in charge, jamaa anawaza sana ampe ruhusa au amkatalie, itabidi aache watoto aende mwenyewe, first born yuko na Miaka 5, na anaemfatia yupo na miaka 2.
Ushauri wako ni upi? Mimi nimemwambia amruhusu aende akatafute fursa za maisha, lakini ajiandae kwa Kila kitu, akiona Kuna mabadiliko yoyote ya dharau au usaliti asiogope kupiga chini.