Ofisi ya CAG ifutwe kama hatutaki kupambana na ufisadi

Ofisi ya CAG ifutwe kama hatutaki kupambana na ufisadi

econonist

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
20,189
Reaction score
29,663
Kwa maoni yangu yanayotokana na mashambulizi dhidi ya ofisis ya CAG, ni bora tuifute ofisi hiyo maana ni Kama inadharaulika.

Naomba nijadili matukio mawili ambayo yamesabaisha nifikie hitimisho hilo. Nikiondoa tukio la CAG Assad kuitwa mbele ya kamati ya bunge kujieleza kipindi Cha ndugai.

Kwanza, bunge limeonesha kupambana na ofisi ya CAG. Kwa Sasa bunge haliipi ripoti ya CAG uzito wowote. Ni Bora bunge lijadili azimio la kumpongeza Rais au maadili, lakini kutenga siku tatu kujadili mambo mazito Kwenye ripoti inaonekana ngumu mpaka kurushwa mwezi wa kumi na moja amabpo ushahidi utakuwa umeondolewa na maofisa wa CAG kunyamazishwa.

Pili, serikali kupitia msemaji wake imeishambulia ofisi ya CAG kwa kudai kuwa wafanyakazi wa ofisi hiyo ndio wenye kasoro. Moja kwa moja inaoenekana serikali haiamini ripoti za CAG na kuwashuku maafisa wa CAG kupika takwimu.

Sasa Kama bunge na serikali haiiamini ofisi ya CAG basi ni bora tuifute hiyo ofisis ili ufisadi uendelee bila ufuatiliaji, Kuliko kuizodoa na kuikashifu ofisi ya CAG kisa imetoa ripoti yenye kuonesha ufisadi mkubwa.

Ni unafiki wa kuendelea kulipa mabilioni ya shilingi Kwenye ofisi ya CAG wakati ripoti yake tunaidharau na kuishamblia na wala haitekelezwi.
 
Ripoti inasema pesa zilizoibiwa ni zaidi ya bajeti ya nchi ambayo hata utekelezaji wake ni almost 40 % ni mwehu tuu anayeweza iamini hyo ripoti
 
Ripoti inasema pesa zilizoibiwa ni zaidi ya bajeti ya nchi ambayo hata utekelezaji wake ni almost 40 % ni mwehu tuu anayeweza iamini hyo ripoti
Tatizo ni ripoti au ofisi iliyoandaa hiyo ripoti ?
 
Ripoti inasema pesa zilizoibiwa ni zaidi ya bajeti ya nchi ambayo hata utekelezaji wake ni almost 40 % ni mwehu tuu anayeweza iamini hyo ripoti
Ndio maana nikasema hiyo ofisi iondolewe watu wajiendeshe wanavyotaka. Maana inaonekana hatuiamini ripoti yake.
 
Shida sio katiba mpya utashi wa kisiasa wa hawa Viongozi wa bunge na serikali.
Huo utashi wa hao viongozi utapatikana lini?.Waliopo ndio hawa hawa usitegemee watazaliwa wengine tofauti.Mambo yote ya ovyo yanatokana na mapungufu ya katiba tuliyonayo.Tungekua na katiba bora inayompa Cag nguvu na mamlaka kusingekua na haya unayoyaona kwenye hiyo ofisi.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Shida ni katiba. Kwa nini usubiri hisani ya utashi wakati ukiweka instruments sheria inafuata mkondo wake bila kusubiri au kuhitaji hisani??
Kwa Tanzania hata Katiba iwe nzuri kiasi gani bila utashi wa kisiasa hakuna litakalofanikiwa. Katiba inampa mamlaka CAG kuwa huru, lakini Kuna kipindi alihojiwa ikulu Kama Ni kweli Trilioni 1.5 zilipotea.
 
Huo utashi wa hao viongozi utapatikana lini?.Waliopo ndio hawa hawa usitegemee watazaliwa wengine tofauti.Mambo yote ya ovyo yanatokana na mapungufu ya katiba tuliyonayo.Tungekua na katiba bora inayompa Cag nguvu na mamlaka kusingekua na haya unayoyaona kwenye hiyo ofisi.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app

Mbona Katiba ya Sasa inampa mamlaka CAG au unataka mamlaka gani?
 
Ngoja kwanza niwape maarifa,kwani afisi Iko chini ya nani,Sasa kwa nini ifutwe wakati haina madhara? Mi napendekeza afisi tuwape jeshi.
 
Back
Top Bottom