Ofisi ya CAG ifutwe kama hatutaki kupambana na ufisadi

Ofisi ya CAG ifutwe kama hatutaki kupambana na ufisadi

Kwa maoni yangu yanayotokana na mashambulizi dhidi ya ofisis ya CAG, ni bora tuifute ofisi hiyo maana ni Kama inadharaulika.

Naomba nijadili matukio mawili ambayo yamesabaisha nifikie hitimisho hilo. Nikiondoa tukio la CAG Assad kuitwa mbele ya kamati ya bunge kujieleza kipindi Cha ndugai.

Kwanza, bunge limeonesha kupambana na ofisi ya CAG. Kwa Sasa bunge haliipi ripoti ya CAG uzito wowote. Ni Bora bunge lijadili azimio la kumpongeza Rais au maadili, lakini kutenga siku tatu kujadili mambo mazito Kwenye ripoti inaonekana ngumu mpaka kurushwa mwezi wa kumi na moja amabpo ushahidi utakuwa umeondolewa na maofisa wa CAG kunyamazishwa.

Pili, serikali kupitia msemaji wake imeishambulia ofisi ya CAG kwa kudai kuwa wafanyakazi wa ofisi hiyo ndio wenye kasoro. Moja kwa moja inaoenekana serikali haiamini ripoti za CAG na kuwashuku maafisa wa CAG kupika takwimu.

Sasa Kama bunge na serikali haiiamini ofisi ya CAG basi ni bora tuifute hiyo ofisis ili ufisadi uendelee bila ufuatiliaji, Kuliko kuizodoa na kuikashifu ofisi ya CAG kisa imetoa ripoti yenye kuonesha ufisadi mkubwa.

Ni unafiki wa kuendelea kulipa mabilioni ya shilingi Kwenye ofisi ya CAG wakati ripoti yake tunaidharau na kuishamblia na wala haitekelezwi.
Umemaliza kila kitu !! Lakini walishaga tudharau kitambo sana !!
 
😂😂😂 Mpambanaji mkuu Tutamkumbuka!
Alivyozima mjadala wa Trilioni 1.5 na kumfukuza kazi CAG. Wahuni wa Sukuma Gang sasa hivi ndio wanaona fedha za umma zinawauma. Wakati ule wanagawana za plea bargain hawakuona kama ni ufisadi.
 
Kwa Tanzania hata Katiba iwe nzuri kiasi gani bila utashi wa kisiasa hakuna litakalofanikiwa. Katiba inampa mamlaka CAG kuwa huru, lakini Kuna kipindi alihojiwa ikulu Kama Ni kweli Trilioni 1.5 zilipotea.
Ni kwa sababu tume "politicized" kila kitu ikiwemo ufisadi na jinai nyingine. Siasa tupu hata paspo hitajika siasa na "utashi".

Nikupe mifano kuonyesha ubovu na udhaifu wa Katiba na mfumo wetu wa sasa - na kwa nini "maadui" Rushwa, Ufisadi, Umaskini na Ujinga vimetushinda tangu uhuru.

1. Rais wetu - mwenye mamlaka ya kifalme/emperor anamteua CAG, Director of PCCB, DPP, DCI, IGP, RPC, RC Mawaziri na ma DED (wote hao ni mhimili wa Dola - Utawala). Wanakula kiapo cha utii kwake. Pamoja na wenzao hapo chini #2.

2. Halafu Rais anawateua Jaji Mkuu na Jaji Kiongozi na majaji (Mhimili Mwingine wa Pili wa Dola uitwao Mahakama)

3. Tena Rais wetu ni mwenyekiti wa chama chake na anamteua Spika na Naibu wake kuongoza Mhimili wa Tatu wa Dola uitwao Bunge.
Na 2020 Rais Magufuli aliteua Wabunge wote i.e. Bunge lote la sasa!

NB: Duniani hakuna mwanadamu yeyote chini ya jua mwenye uwezo au ni genius wa kutenda kwa ufanisi, weledi wala haki hayo majukumu yote. Na ni kawaida kabisa Rais yeyote atazidiwa na/au kuwa influenced na wanaomzungaka!
Watu hutoa utetezi 'dhaifu' kuwa Rais ni taasisi na sio mtu mmoja, lakini hakuna mantiki, uhalali wala ukweli kwenye hilo. Hayati Magufuli aliwahi kusema hataki kushauriwa wala "kuingiliwa"!

Ona maigizo na vichekesho sasa:-

CAG anakagua mahesabu, anamaliza na kutoa ripoti kwa Mamlaka ya Uteuzi - Rais.
Ripoti yake inakabidhiwa kwa Bunge ili kubaini na kutolewa "Mazimio ya Bunge" ili Serikali i.e Mamlaka ya Uteuzi ichukue hatua. (Usisahau sifa za kuwa mbunge ni kujua kusoma na kuandika). Eti hao wakae kama Mahakama ya Kangaroo inayoitwa 'Kamati' kupitia na kuamua mambo ya kitaalam na kiweledi ya kijinai ya ripoti ya CAG!
Halafu kuna wanaotaka kumlaumu Rais ki rejareja wakati sheria zetu zinatamka hivyo.

Worst still, hata Azimio la Bunge likesema fulani ashtakiwe, PCCB, Police na DCI watachunguza na kuandaa mashtaka, lakini ni DPP atakayeamua kesi iende mbele au la, na pia iendeje! Huo nao ni mhimili wa kiaina ktk mfumo wa sasa. Plea bargains za hayati Magufuli na Biswalo ni mfano mzuri.

Si utaona wazi tu shida iko wapi.

Jamani hatujawahi kuwa serious kupambana na rushwa wala ufisadi-ni siasa tu.

Tumejidanganya na kudanganywa kuna mihimili mitatu, ukweli ni kwamba uko mmoja tu "uliojichimbia chini" unaoamua na kufanya kila kitu nchini. "Check and Balance" ni hadithi ya kusadika tu. Ndugai alipotofautiana na huo, alikaa pembeni fasta! CAG Assad alitupwa bench alipotofautiana nao. Hamuoni?? Hamsikii??

Inatosha! Tupeni Katiba Mpya sasa.

::Katiba ni utaratibu tutakaojiwekea wa kujitawala; kupambana na changamoto za sasa na mazingira na mahitaji ya sasa na ya baadaye. Pia ni uti wa mgongo wa Sheria zote za nchi na pia chimbuko la MAMLAKA na Power.

Tutapunguza madaraka na influence ya Rais. Tutaunda mfumo tofauti na huu, tutangeneza Taasisi huru na zenye nguvu na mamlaka kiutendaji na kimamlaka zitakazoshughulikia mambo yale kwa ufanisi na kwa haki - kwa haraka.
 
Nilipoiona Ile report nilifurahi Sana, maana niliona jirani yangu hapa Kimara kwisha habari yake maana huyu bwana utadhani ndani kwake Kuna mashine ya hela.
Lakini ndio kwanza mkewe na mtoto ndito ya kuolewa wako Dubai tangu jumamosi iliyopita.
Huu ni wivu binafsi na roho ya kichawi
 
Ofisi ya CAG imetimiza wajibu wake kikamilifu. Ofisi ya CAG ina umuhimu wa hali juu katika kujua kinachoendelea huko kuhusiana na pesa yetu.

Kinachotakiwa kufutwa ni kile kisicho na faida au ambacho kinashindwa kutekeleza wajibu wake.

Pendekezo zuri, ingekuwa kufutwa kwa Bunge hili lisilo na maana yoyote. Hii miaka miwili Serikali ikusanye mapato, ipange na kupitisha matumizi ambayo yatakaguliwa na CAG. Kama kutakuwa na wizi au ubadhirifu, kwa kuwa jinai haina muda, siku tutajapokuwa na Bunge halisi, litaweza kupitia report zote za kipindi ambacho hatukuwa na Bunge.

Hakika kwa hili Bunge la sasa, kuna faida kubwa ya kutokuwepo kuliko uwepo wake. Uwepo wake ni hasara tupu.
 
Kwanza, bunge limeonesha kupambana na ofisi ya CAG. Kwa Sasa bunge haliipi ripoti ya CAG uzito wowote. Ni Bora bunge lijadili azimio la kumpongeza Rais au maadili, lakini kutenga siku tatu kujadili mambo mazito Kwenye ripoti inaonekana ngumu mpaka kurushwa mwezi wa kumi na moja amabpo ushahidi utakuwa umeondolewa na maofisa wa CAG kunyamazishwa.
Changamoto ni kanuni, enzi zile bunge la January ndio lilijadili CAG report kwa Sasa namsikia Tulia anasema ni bunge la November. Na changamoto huwa ni kwamba bunge halijadili ripoti ya CAG mpaka PAC iwe imeipitia na kufikia conclusion zake. So hizo bureaucracy zote ndio zinachelewesha ripoti kufika bungeni.
Pili, serikali kupitia msemaji wake imeishambulia ofisi ya CAG kwa kudai kuwa wafanyakazi wa ofisi hiyo ndio wenye kasoro. Moja kwa moja inaoenekana serikali haiamini ripoti za CAG na kuwashuku maafisa wa CAG kupika takwimu.
Ndio hivyo CAG hafanyi kazi ya serikali Bali kazi ya BUNGE na hata bajeti ya NAO unapangwa na kamati ya bunge. So obviously serikali haiwezi kuwa rafiki ya NAO. Mind you ofisi ya CAG na ukaguzi wote wanaofanya ni baada ya kelele za Zitto na Dr Slaa mwaka 2008 kuwa ofisi hii ianzishwe kukagua pesa za umma. So wanaona kama ni initiative ya upinzani zaidi and so CAG is marginalized.

Sasa Kama bunge na serikali haiiamini ofisi ya CAG basi ni bora tuifute hiyo ofisis ili ufisadi uendelee bila ufuatiliaji, Kuliko kuizodoa na kuikashifu ofisi ya CAG kisa imetoa ripoti yenye kuonesha ufisadi mkubwa.
Nadhani dhaifu ni bunge maana CAG kazi yake ni kutoa taarifa so zingefanyiwa kazi na PAC kwa umakini basi tungeona matunda ya ripoti hii. Tatizo PAC imekua dhaifu tokea mwenyekiti alipokua Mama Kaboyoka na Sasa kamati ipo chini ya mbunge wa CCM so tusitegemee jipya. Ila siku PAC ikiwa na watu serious basi tutaona faida za ripoti ya CAG. Nadhani enzi za kina Zitto kuwa mwenyekiti POAC then PAC walau tuliona faida za ripoti ya CAG maana walikua wanatumbua viongozi wote waliotajwa.
 
Ripoti inasema pesa zilizoibiwa ni zaidi ya bajeti ya nchi ambayo hata utekelezaji wake ni almost 40 % ni mwehu tuu anayeweza iamini hyo ripoti
Accumulated figures, mfano mwaka huu unafanya performance audit Kwenye SGR obviously utakagua Kila kitu sio tu bajeti ya mwaka huu. So kama ulivyoona ufisadi kwenye SGR ni matrilioni sababu ni jumla ya thamani yote ya mradi bila kujali mwaka huu pekee.
 
Back
Top Bottom