Ofisi ya Rais – TAMISEMI Special Thread: Karibu tukuhudumie, tupe Maoni, Maswali, Mapendekezo na Malalamiko

Ofisi ya Rais – TAMISEMI Special Thread: Karibu tukuhudumie, tupe Maoni, Maswali, Mapendekezo na Malalamiko

Joined: 3rd July 2024
Last seen:1st October 2024.

Wastaafu wa toka 2019 bado wanasotea "mapunjo" ya pensions zao halmashauri ya wilaya ya Nzega.

1:Walilipwa lump sum pungufu kutokana na mwajiri kutokupeleka michango yao kikamilifu PSSSF.

2:Wanalipwa monthly pension pungufu hadi leo kutokana na sababu na 1 hapo juu.

Anzisheni "Samia Pensioners Clinic" izunguke huko halmashaurini muongee na hili kundi linapitia changamoto sana kupata stahiki zao.

OR TAMISEMI
 
Wizara ya Tamisemi na Utumishi wa Umma: Watumishi wanaotumikia nchi yetu hawana tena Morali ya Kazi. Wahamishe wakae na familia zao karibu.
 
Wizara ya Tamisemi na Utumishi wa Umma: Watumishi wanaotumikia nchi yetu hawana tena Morali ya Kazi. Wahamishe wakae na familia zao karibu.
Watu wanahama kupitia mfumo kama umetuma maombi na yamefika TAMISEMI Yana zaid ya miezi 5 jaribu kufatilia Kwa mwajiri wako waliopitishiwa maombi kwenye mfumo tangu mwezi wa 5 mwaka jana wamepewa barua wote na barua zimetoka mwaka jana mwezi wa 11
 
Kuna changamoto Kubwa ambayo ipo katika halmashauri nyingi (Ikiwemo Bunda DC); Malipo ya mapunjo ya mshahara.
Unakuta kuna mtu ana madai ya miaka 10 iliyopita, cha ajabu, walio na madai ya hivi Karibuni ndiyo hulipwa, wale walio na madai ya miaka mingi iliyopita wanaendelea kusugua benchi.
Je, utaratibu huu Ni maagizo kutoka kwenu ninyi Tamisemi?
 
Wakurungwa eee wapoleni madaraka ya kuajili sekretarieti hawa jamaaa ni ovyo sana aisee kuita watu interview ni issue sana wanachelewesha sana
 
Nakuja hapa kwa sababu DAWASCO hawana uzi maalum.. Ipo hivi, Kuna msukuma mmoja ana mabwawa ya Samaki hapa Kibamba Hospitali.. Huyu Mwamba amaweka Bomba kuu la DAWASCO ndani ya geti lake kinyume na Sheria ambapo anatakiwa aliache kwa umbali wa mita 7.5.. Amebana barabara inayoelekea Chuo Cha wakorea.. Viongozi ikiwemo Diwani na Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wanamuogopa.. DAWASCO wanamuangalia tu.. Hebu tumeni watu waje washuhudie wizi wa maji anaofanya huyu Msukuma..
 
Wizara hii Tamisemi.
Naomba kuuliza Fedha za Supervison za Miradi ya SEQUIP 2024/2025 ndio Mmegoma kuzitoa ili Watumishi tunaosimamia tutumie mishahara yetu au?
Maana miradi inaisha na Tushatumia sana Mishahara yetu kwenda site na mambo mengine.
 
Ni kweli kabisa kwa Serikali hii tunapoteza muda tu. Huyu Mtendaji ni best wa DED Kinondoni. DED ni best wa Rais. Kesi ya nyani hii
Sasa huu urafiki wao ndio wanatuharibia nchi ; na kama DED ni best wa Samia ndio maana hakai ofisini kushuhurikia matatizo ya Wananchi na bado anadhani Wananchi watampa kura Samia!!! Wanamloga bibi ya watu kwa kutokuwajibika!! Mchengerwa , kama unapita pita humu tafadhali mchukulie hatua huyu mtendaji ama sivyo badala ya kumjenga mnambomoa Samia!
 
Wamefungua account humu July 2024, mwisho ku login October 2024

Labda wana soma juu kwa juu au wanaogopa kujibu

Shame
 
Ndugu wana JamiiForums,

Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), kupitia thread hii, tutapokea Maoni, Ushauri, Malalamiko, Mapendekezo yako Mwananchi. Tunakuhakikishia kuchukua hatua stahiki kwa haraka zaidi kwa kile utakachokiwasilisha kwetu.

Ikumbukwe kuwa tangu Mwaka 1961 hadi sasa Ofisi ya Rais –TAMISEMI imekuwa ni Wizara inayojitegemea na madhumuni ya kuwepo kwa Serikali za Mitaa ni kupeleka Madaraka kwa Wananchi ambapo chimbuko lake ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 Sura ya 8, Ibara ya 145 na 146.

Hadi sasa Nchi ina Mikoa 26, Wilaya 139, Halmashauri 184, Tarafa 570, Kata 3,956, Vijiji 12,319, Vitongoji 64,361 pamoja na Mitaa 4,263.

Majukumu ya Ofisi ya Rais - TAMISEMI
yanatekelezwa katika ngazi ya Makao Makuu, Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kuzingatia Hati ya Rais ya Mgawanyo wa Majukumu (Presidential Instrument) iliyotolewa na Rais Mei 2021, majukumu ya OR-TAMISEMI ni pamoja na:-

i) Kuratibu utekelezaji wa Sera ya Maendeleo Mijini na Vijijini na Upelekaji wa Madaraka kwa Umma (D by D);
ii) Kuratibu huduma mijini kama vile usafirishaji, maji na usafi wa mazingira;
iii) Kusimamia Tume ya Utumishi wa Walimu;
iv) Kuratibu na Kusimamia Tawala za Mikoa ili ziweze kuziwezesha Halmashauri kutekeleza wajibu wake;
v) Kuratibu Usimamizi na Uendeshaji wa Shule za Msingi na Sekondari nchini kupitia Mamlaka za Serikali za Mitaa (MSM);
vi) kusimamia na kuratibu shughuli za utolewaji wa huduma za Afya ya Msingi, Ustawi wa Jamii na Lishe
vii) Kuratibu na kusimamia mifumo na miundombinu ya TEHAMA katika Ofisi za Wakuu wa Mikoa, Mamlaka za Serikali za Mitaa na Taasisi
viii) Kujenga uwezo wa watumishi wa OR-TAMISEMI ili watekeleze majukumu yao kwa ufanisi
ix) Kuratibu shughuli za wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo
x) Kusimamia utendaji wa Mashirika, Taasisi, Programu na miradi iliyo chini ya OR-TAMISEMI

Kupitia JamiiForums.com unaweza kuwasiliana nasi (OR-TAMISEMI) kwa kutuma ujumbe wako kwenye sehemu ya kuweka maoni hapo chini au tutumie kupitia Private Message (PM).

Pia, tunapatikana kupitia:

Instagram @ortamisemi
Twitter @ortamisemitz
Facebook Ofisi ya Rais-Tamisemi
Website www.tamisemi.go.tz
YouTube @ortamisemi
Watssap channel: Ofisi ya Rais - TAMISEMI

Anuani
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
S.l.P 1923 Dodoma - Tanzania,
Telephone: +255 262 321 234
Fax: +255 262 322 116
Email: ps@tamisemi.go.tz
Complain: ps@tamisemi.go.tz

Kituo cha Huduma kwa Mteja
+255 735 160 210 au +255 26 216 0210
Kuanzia saa 1:30 asubuhi mpaka saa 10:30 jioni

JamiiForums





WIZARA YA TAMISEMI NA WIZARA YA ELIMU. NENDENI IFAKARA MKAJIONEE MADUDU​


Kuna walimu wakuu shule za msingi takribani 19 wameenguliwa nafasi zao bila Sababu za msingi.

Jambo la ajabu ni kwamba:-
1. Walimu hao 19 wamepokea barua za onyo mwezi January Mwaka huu. Barua za onyo zinaonekana zimeandikwa na kusainiwa na mkurugenzi tangu mwezi December mwaka jana.

2. Barua za kushushwa cheo nazo wamepokea mwezi huu, lakini barua hizo zinaonekana ziliandikwa na kusainiwa tangu mwez September 2024.

Kwahiyo, kwa kuziangalia tarehe za barua, utaona mwalimu ameshushwa cheo halafu akiwa sio mwalimu mkuu ndio amepokea barua ya onyo.

Boma la ifakara linalalamikiwa sana kwa ukabila (uzawa) inashusha sana morale ya walimu ambao wanasifa mbalimbali lakini sio wazawa wa bonde la Kilombero.

Nyinyi mnauwezo wa kufatilia jambo hili kiundani na kulitafutia ufumbuzi. Mnavyombo vingi vinavyoweza kusaidia upatikanaji wa taarifa kwa kina.
 
Huo usanii wa kutahini walimu mamia kwa mamia halafu wanataka watu hata 20 hawafiki sio kupotezeana muda na gharama?
Watangazetu kwamba hamna ajira. Tangu lini walimu wakafanyiwa usaili
Hivi ni kwa nini hawafanyiwi/walikuwa hawafanyiwi usaili kama ilivyo kwa kada nyingine?
 
Hivi ni kwa nini hawafanyiwi/walikuwa hawafanyiwi usaili kama ilivyo kwa kada nyingine?
Utafanyiaje usaili watu ambao wanahitajika maelfu kwa maelfu? Nimatumizi mabaya ya muda na hela.
Mbona wanaomaliza CCP hawafanyiwi usaili? Hii nchi maigizo mengi. Mkenda nae eti ni profesa
 
TAMISEMI
Ndugu wana JamiiForums,

Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), kupitia thread hii, tutapokea Maoni, Ushauri, Malalamiko, Mapendekezo yako Mwananchi. Tunakuhakikishia kuchukua hatua stahiki kwa haraka zaidi kwa kile utakachokiwasilisha kwetu.

Ikumbukwe kuwa tangu Mwaka 1961 hadi sasa Ofisi ya Rais –TAMISEMI imekuwa ni Wizara inayojitegemea na madhumuni ya kuwepo kwa Serikali za Mitaa ni kupeleka Madaraka kwa Wananchi ambapo chimbuko lake ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 Sura ya 8, Ibara ya 145 na 146.

Hadi sasa Nchi ina Mikoa 26, Wilaya 139, Halmashauri 184, Tarafa 570, Kata 3,956, Vijiji 12,319, Vitongoji 64,361 pamoja na Mitaa 4,263.

Majukumu ya Ofisi ya Rais - TAMISEMI
yanatekelezwa katika ngazi ya Makao Makuu, Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kuzingatia Hati ya Rais ya Mgawanyo wa Majukumu (Presidential Instrument) iliyotolewa na Rais Mei 2021, majukumu ya OR-TAMISEMI ni pamoja na:-

i) Kuratibu utekelezaji wa Sera ya Maendeleo Mijini na Vijijini na Upelekaji wa Madaraka kwa Umma (D by D);
ii) Kuratibu huduma mijini kama vile usafirishaji, maji na usafi wa mazingira;
iii) Kusimamia Tume ya Utumishi wa Walimu;
iv) Kuratibu na Kusimamia Tawala za Mikoa ili ziweze kuziwezesha Halmashauri kutekeleza wajibu wake;
v) Kuratibu Usimamizi na Uendeshaji wa Shule za Msingi na Sekondari nchini kupitia Mamlaka za Serikali za Mitaa (MSM);
vi) kusimamia na kuratibu shughuli za utolewaji wa huduma za Afya ya Msingi, Ustawi wa Jamii na Lishe
vii) Kuratibu na kusimamia mifumo na miundombinu ya TEHAMA katika Ofisi za Wakuu wa Mikoa, Mamlaka za Serikali za Mitaa na Taasisi
viii) Kujenga uwezo wa watumishi wa OR-TAMISEMI ili watekeleze majukumu yao kwa ufanisi
ix) Kuratibu shughuli za wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo
x) Kusimamia utendaji wa Mashirika, Taasisi, Programu na miradi iliyo chini ya OR-TAMISEMI

Kupitia JamiiForums.com unaweza kuwasiliana nasi (OR-TAMISEMI) kwa kutuma ujumbe wako kwenye sehemu ya kuweka maoni hapo chini au tutumie kupitia Private Message (PM).

Pia, tunapatikana kupitia:

Instagram @ortamisemi
Twitter @ortamisemitz
Facebook Ofisi ya Rais-Tamisemi
Website www.tamisemi.go.tz
YouTube @ortamisemi
Watssap channel: Ofisi ya Rais - TAMISEMI

Anuani
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
S.l.P 1923 Dodoma - Tanzania,
Telephone: +255 262 321 234
Fax: +255 262 322 116
Email: ps@tamisemi.go.tz
Complain: ps@tamisemi.go.tz

Kituo cha Huduma kwa Mteja
+255 735 160 210 au +255 26 216 0210
Kuanzia saa 1:30 asubuhi mpaka saa 10:30 jioni
Napongeza juhudi za maendeleo ya teknolojia katika utumishi wa umma. Ushauri wangu kwenu. Mfumo wa Ess Utumishi uwe na sehemu ya Mtumishi kureject maombi ya uhamisho au kuwe na ruhusa ya mtumishi kuomba zaidi ya mara moja. Hii ni kuepusha usumbufu kwenu hasa kwa wale watumishi wanaokuwa wamekosea kwa bahati mbaya kutuma maombi. Itasaidia kumfanya afute aombe upya au hata kama maombi mengine yapo pending na yamekosewa basi aombe tena kwa usahihi. Tunateseka kusubiri yafutwe na katibu mkuu ambaye anamajukumu mengi na inaonekana aingii kwenye mfumo mara kwa mara kuyashughulikia.
 
Back
Top Bottom