Ofisi ya Rais – TAMISEMI Special Thread: Karibu tukuhudumie, tupe Maoni, Maswali, Mapendekezo na Malalamiko

Mradi wa bonde la mto msimbazi unaanza lini!?
 
OR- TAMISEMI mfumo wenu wa TAUSI haupo na uhalisia malalamiko ni mengi lakini hakuna muitikio wowote.Changamoto zilizopo kwenye mfumo wa TAUSI PORTAL;

1.Mfumo wa ufunguaji wa account mpya haufanyi kazi.

2.Kwenye eneo la LAND SALES.Ukiingia kuna muda mfumo unaonyesha viwanja vipo wazi vinarangi ya kijani na kuna muda viwanja hivyo hivyo unakuta vimewekwa rangi nyekundu kuashiri vimeshanuunuliwa.

3.Utaratibu wa kulipia 30% upfront sio rafiki kwakua watu wengi wangependa kuona kwanza sehemu wanayonunua ili kuridhia.Huu utaratibu wa kulipia 30% ya bei ya kiwanja ndio mtu aende halmashauri husika akakione kiwanja unapunguza wateja na kuweka ugumu ikiwa viwanja vitaisha na mtu angependa abadilishiwe eneo.

Mnaweza mkabadili utaratibu kwa kuweka siku za kwenda kutembelea maeneo.Kwa mfano mara mbili kwa mwezi labda Jumamosi mbili kila mwezi katika muda wenu wa GROSS PERIOD.

Njia hii itavuatia watu wengi ambao watafika na kuonana na wataalamu na maafisa ardhi kwa maelezo zaidi na maelekezo ya umiliki wa ardhi katika halmashauri husika.Pia wale wenye changamoto mfano wameshindwa kufungua account na changamoto nyinginezo wangepata usaidizi wa haraka na uhakika kutoka watu husika.

Wahusika mtusaidie maana nimepiga simu mpaka halmashauri husika ila sikupata msaada wa kuridhisha na wakati mwingine simu hazipokelewi.

Mfumo huu ni mzuri kama utakuwa na ufanisi na utasaidia kuondoa vishoka na kuwa na mipango miji mizuri na kupunguza migogoro ya ardhi kwakuwa watu watanunua ardhi sehemu sahihi hivyo ni msaada kwa watu wa hali ya chini.

Pia niwaase muutangaze mfumo ili usiwe unajulikana tu kwa watu wachache.
 
Huo ni utapeli wa kitaasisi uliohalalishwa na serikali.
 
Mfumo huu ni mzuri kama utakuwa na ufanisi na utasaidia kuondoa vishoka
Vishoka wako ndani ya taasisi husika kwa kushirikiana na wataalamu wa mfumo ili kuuchezesha wanapotaka kutekeleza jambo lao.
 
Nilisoma moja ya shule kubwa ya sekondari (yenye form 1 - VI) madasa A,B,C, D kwa kidato
Mwalimu wa phy 1, biology, 1, Chem 2, Hesabu 0 na baadae 1 (wanafundisha hadi wanapata kizunguzungu)
Huku waalimu wa English na Kiswahili wanagombea ili mwalimu asije akasahaulika na kuachwa bila kipindi
LAKINI zikitangazwa ajira utashangaa walio ajiriwa wengi ni wale wale wanaogombea wasikose kipindi.......
Sijui kama na hili linahitaji msaada wa watu wa Marekani ili watusaidie kufikiri ?
 
🙏🙏🙏
 
Ila tamisemi mnazingua Sana, mna mifumo mingiii ila ufanisi wake niwamashaka, mfano ni ESS, mnachangia mazingira magumu Kwa watumishi walio chini yenu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…