Ole Mushi: Watanzania tumejipangaje kuipokea Congo kwenye EAC?

Ole Mushi: Watanzania tumejipangaje kuipokea Congo kwenye EAC?

Linguistic

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2021
Posts
3,669
Reaction score
8,268
DRC imeingia kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki. Imekuja na vitu vifuatavyo:-.

1. Imekuja na Population ya Watu Milioni 92. Idadi hii ya watu itaifanya Jumuiya yetu sasa kuwa na Population ya watu milioni 289. Congo pekee inachangia zaidi ya Robo ya Population yote ya EAC. Inaingiza Asilimia 31% ya population yote.

2. Congo imekuja na ukubwa wa Eneo KM za Mraba 2,345,000 na kuifanya Jumuiya kuwa na eneo la KM za Mraba 4,809,992. Congo pekee inaingiza asilimia 48% ya Eneo lote la EAC.

3. Imekuja na Deposit ya Madini ya Kutosha mengi kuliko ya nchi yoyote kwenye Jumuiya hii.

4. Imekuja na Ardhi yenye Rutuba ya kutosha na ambayo mvua hunyeesha kwa kiwango kikubwa kabisa.

Mambo makubwa yanayoitesa Congo ni mawili.

1. Haina Bandari hutegemea Mombasa na Daresalam kuingiza mizigo yao Congo.

2. Vita za hapa na Pale za kisiasa zimeathiri sana Shughuli za Kiuchumi DRC.

𝙺𝙴𝙽𝚈𝙰 𝚆𝙰𝙼𝙴𝚂𝙷𝙰𝙲𝙷𝚄𝙽𝙶𝚄𝙻𝙸𝙰 𝙳𝙸𝙻𝙸

Kwa Afrika Mashariki, Kenya ni mojawapo ya Taifa ambalo limewekeza kwenye Economic intelligence, tayari kikosi kazi cha Kenya kimeshafika Congo na Kuchambua Fursa zilizopo pale..

Kwenye ripoti yao wameonyesha mambo kadhaa mojawapo ni kwamba imebainika kuwa DRC asilimia 4% tu ya watu wote milion 92 ndio wenye bank account. Bank ya Kenya KCB wameweka mkazo mkubwa sana hapa na tayari wapo Congo kwa ajili ya Mission maalumu. KCB imeambatana na makampuni mengine mawili ya kibiashara ambayo ni Jubilee kampuni la bima na Jambo Net.

Ripoti hiyo pia imeonyesha kuwa Congo inatoa asilimia 70% ya madini yote ya Cobalt Duniani ambayo ndio msingi wa Utengenezaji wa mabetri ya Simu, laptop na kadhalika. Kwa kufahamu hilo tu Kenya wameanza Mpango wa kuja na kiwanda cha Magari yanayotumia Umeme kitakachojengwa DRC.

Ripoti hiyo pia inataja madini ya Copper kuwa Congo pekee inatoa asilimia 50 ya madini yote Duniani hivyo bado wanaendelea kuchakata ni kwa namna gani watatumia fursa hiyo ndani ya East Africa.

Ripoti hiyo pia inataja fursa za mazao ya Misitu, Kilimo, na Ufugaji ambayo Kenya wanazifanyia kazi ya kiuchambuzi zaidi kuona watanufaikaje.

𝙽𝙸𝙽𝙸 𝚃𝙰𝙽𝚉𝙰𝙽𝙸𝙰 𝙸𝙺𝙸𝙵𝙰𝙽𝚈𝙴.

Nimejiuliza sana ila hatupo aggressive sana kwenye mambo ya maana. Mijadala ya Watanzania wengi ni ya mambo rahisi sana kuanzia huku chini hadi juu.

Kwenye East Africa Tanzania ilikuwa giant kwenye mambo mawili. Moja tukikuwa na eneo kubwa kuliko nchi nyingine na tulikuwa na rasilimali nyingi kuliko nchi nyingine.

Nimeangalia Biashara kati ya Congo na Kenya, Uganda, Nikagundua Tanzania bado hatujawekeza sana huko Congo.

Dalili za Congo kuingia EAC zilishaonekana muda Mrefu. Kwa kufahamu hivyo Kenya Rais wake alikwenda Huko mapema mwaka huu kuweka kusaini mikataba kibao. Nitaileta hapa baadaye.

Ole Mushi
071702602
 
Wazo zuri sana, viongozi wetu wanatakiwa kuliona hili na kuwahamasisha wananchi,. Unatakiwa mpango wa kitaifa na sio kuachia kila mwanchi kupambana kivyake.
 
Watanzania tuna bahati mbaya kirithi mfumo wa ujamaa na kuruthishwa kwa lazima chama cha mapinduzi. Ni ukweli kuwa Mifumo ya kizamani ya kidikteta na chama cha mapinduzi ndiyo maadui wa sasa wa taifa.

Serikali mithili ya Tanzania ni ya kilaghai tu. Serikali haina muda wa kuitazama nchi, bali wanatazama zaidi chama chao, masilahi yao, kama kundi na ya wajanja wajanja mmoja mmoja, na namna ya wakubwa kusalia madarakani kwa njia zozote.

Maendeleo ya wananchi, kisiasa, kiuchumi, kiufahamu, na kijamii, yote ni hatari kwa watawala wanaowaza kushikilia nchi kwa maslahi yao.

Hata ukiwasikia wakiongea haya mambo ya faida za muungano wa EAC, tambua kuwa wanajiongelea wao, chama chao na watoto wao. Wananchi wa kawaida mkae tu na maisha duni, mtaabike, kisha mfe haraka haraka ili wao waendelee kuishi kwa amani bila bugudha zenu.

Hofu yangu ni kuwa kuziunganisha nchi zenye wapenda tumbo ni kazi sana. Sudani Kusini ni nchi ndogo, lakini kwa kuwa watawala ni wachumia tumbo zao, nchi imekuwa uwanja wa mauaji kila kukicha na hakuna mtu anayehangaika na hawa wapumbavu.
 
Congo DRC imeingia kwenye Jumuiya ya Africa Mashariki. Imekuja na vitu vifuatavyo:-.

1. Imekuja na Population ya Watu Milioni 92. Idadi hii ya watu itaifanya Jumuiya yetu sasa kuwa na Population ya watu milioni 289. Congo pekee inachangia zaidi ya Robo ya Population yote ya EAC. Inaingiza Asilimia 31% ya population yote...
Uchambuzi mzuri ndio raha ya jf ni madini tuu... Sema kuna watoto wamevamia jukwaa ni matusi muda wote badala ya kujadili mambo ya msingi kama haya
 
TISS wa hapa wanachojua kuubana upinzan na kuiweka CCM madarakan

Linapofika.swala la economic intelligence Hapo hamna kitu n sifur kabisa

Vitu vinapanda Bei hakuna solutions walau bas ushaur

Nchi hii Rais ndye mchumi mkuu anaamua na anongea lolote hakuna wa kumdhibit

Nanukuu kauli yake

"Waambieni ukweli vitu vinapanda Bei sababu ya vita"

Karanga zinazolimwa mtwara zimeathirika na Vita ndyo maana zmepanda Bei

Mchicha unaolimwa bonde la mto msimbaz umepanda Bei sababu ya vita

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
FB_IMG_16487221465824973.jpg
 
Mwezi jana nilifika Burundi fursa zipo nyingi ila hizi nchi zinachangamoto kwenye swala la nishati,mawasiliano na miundombinu hivyo kwa wanaotaka kuwekeza kwenye maeneo haya waweke nguvu kwenye maeneo hayo wasiende na mtazamo wa Dar es Salaam au hata Njombe maana Tanzania imeendelea kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na nchi hizi zilizoathiriwa na vita .
 
..Tz na Drc ni wanachama wa SADC tangu miaka ya 90 au mwanzoni mwa 2000.

..Kwa msingi huo hakuna mabadiliko makubwa yatakayotokea baada ya Drc kujiunga na EAC.

..Kama Watz na Wa-congo hatukuweza kuboresha mahusiano yetu kama wanachama wa SADC sioni kama tutaweza kubadilika baada ya Drc kujiunga na EAC.

Cc Nguruvi3
 
Mkuu pata passport huwezi amini kati ya watu wanaokuwa treated vizuri kongo wakijua wewe ni mtanzania,kongo imeingia kwenye community kwasababu ya tanzania hata kenya wanajua
Treated vizuri ndiyo, lakini tumejipangaje? In the next 5 years malengo yetu ni nini? What about 10 years? Tusijiaminishe kuwa tunakubalika.

Inawezekana US anafaidika zaidi na Kongo kuliko nchi yoyote duniani. Angalia madini ya kongo yanaenda wapi?
 
Congo DRC imeingia kwenye Jumuiya ya Africa Mashariki. Imekuja na vitu vifuatavyo:-.

1. Imekuja na Population ya Watu Milioni 92. Idadi hii ya watu itaifanya Jumuiya yetu sasa kuwa na Population ya watu milioni 289. Congo pekee inachangia zaidi ya Robo ya Population yote ya EAC. Inaingiza Asilimia 31% ya population yote...
Wanasubiri kulaumu serikali na kulalamika 😬😬.

Utasikia serikali haijatusaidia
 
Mkuu pata passport huwezi amini kati ya watu wanaokuwa treated vizuri kongo wakijua wewe ni mtanzania,kongo imeingia kwenye community kwasababu ya tanzania hata kenya wanajua
Kweli 200% niliwahi kuchelewa kutoka uwanja wa Ndjili airport Kinshasa police wa uhamiaji walipoona passport yangu wakaanza kuitana. Kila mmoja alitaka namba yangu. Nilijisikia furaha sana. Wakenya wengi wao ni wakora. Hawaaminiki kiviiile.

Mleta mada umefanya jambo jema sana. Serikali Sasa itoe nafasi Kwa sekta binafsi kufanya ziara za pamoja na serikali yetu na balozi wa DRC Ili kwenda kukamata fursa
 
Congo DRC imeingia kwenye Jumuiya ya Africa Mashariki. Imekuja na vitu vifuatavyo:-.

1. Imekuja na Population ya Watu Milioni 92. Idadi hii ya watu itaifanya Jumuiya yetu sasa kuwa na Population ya watu milioni 289. Congo pekee inachangia zaidi ya Robo ya Population yote ya EAC. Inaingiza Asilimia 31% ya population yote...
Mbona mna-OVERESTIMATE Matarajio namna hii?

Hivi hiyo KCB ilishindwa Nini kufungua matawi ndani ya DRC mpaka isubiri DRC ijiunge EAC? Mbona KCB wana Branches Ethiopia na Malawi ambapo hata sio wanachama wa EAC?

Kuhusu Kujenga Kiwanda Cha Magari ya Umeme!!! MY FOOT Yaani hii hii Kunyaland inayosumbuliwa na Njaa kila mwaka ifungue Kiwanda Cha Magari ya Umeme? Siwezi kuendelea kuongea Chochote.
 
Congo DRC imeingia kwenye Jumuiya ya Africa Mashariki. Imekuja na vitu vifuatavyo:-.

1. Imekuja na Population ya Watu Milioni 92. Idadi hii ya watu itaifanya Jumuiya yetu sasa kuwa na Population ya watu milioni 289. Congo pekee inachangia zaidi ya Robo ya Population yote ya EAC. Inaingiza Asilimia 31% ya population yote....
Mbona mna-OVERESTIMATE Matarajio namna hii?

Hivi hiyo KCB ilishindwa Nini kufungua matawi ndani ya DRC mpaka isubiri DRC ijiunge EAC? Mbona KCB wana Branches Ethiopia na Malawi ambapo hata sio wanachama wa EAC?

Kuhusu Kujenga Kiwanda Cha Magari ya Umeme!!! MY FOOT Yaani hii hii Kunyaland inayosumbuliwa na Njaa kila mwaka ifungue Kiwanda Cha Magari ya Umeme? Siwezi kuendelea kuongea Chochote.
 
Congo DRC imeingia kwenye Jumuiya ya Africa Mashariki. Imekuja na vitu vifuatavyo:-.

1. Imekuja na Population ya Watu Milioni 92. Idadi hii ya watu itaifanya Jumuiya yetu sasa kuwa na Population ya watu milioni 289. Congo pekee inachangia zaidi ya Robo ya Population yote ya EAC. Inaingiza Asilimia 31% ya population yote...
Huyu bwege Ole Mavie kazi kutema mate he doesn't say what he has done or intends to do to explore the due potential of DRC, ushuzi whistle blowing
 
Congo DRC imeingia kwenye Jumuiya ya Africa Mashariki. Imekuja na vitu vifuatavyo:-.

1. Imekuja na Population ya Watu Milioni 92. Idadi hii ya watu itaifanya Jumuiya yetu sasa kuwa na Population ya watu milioni 289. Congo pekee inachangia zaidi ya Robo ya Population yote ya EAC. Inaingiza Asilimia 31% ya population yote....
Tatizo wa Watanzania tunapenda sana kuongelea asali tu. Congo ni nchi ambayo ina vikundi kwa kihasi vingi sana. Kwanza ni kuhakikisha usalama kwa kupeleka wanajeshi wetu kule kulinda watu kama kweli tunataka kufanya biashara. Bila hivyo wazungu ndiyo wataendelea kuiba mali za Congo huko sisi tukibaki kulalamika.

Yaani angalia hapa umeanza kujilingatisha na kenya badala ya kuongelea nchi za ulaya na China wanaochukuwa madini ya mabilioni. Kampuni zinazochimba madini sio za EA lakini umeshaanza kutushindanisha na Kenya wakati hawana kitu. Yaani michanga ya madini inaenda China badala ya kuizuia ili tupeleke walao madini ambayo yamesafishwa na kupata kazi sisi tunafikiria kusafirisha tu.

Hizi ni fikra za kimasikini badala yake madini yote tunaweza kabisa kusafisha wenyewe EA na badala ya kuweka ushindani baina yetu usio na umuhimu tuwatoe kwanza hao wakandamizaji wa kigeni ambao ndiyo wanaleta silaha za kuchochea mapigano.
 
Back
Top Bottom