Ole Sabaya: Doa jeusi kwa utawala wa Hayati Magufuli

Ole Sabaya: Doa jeusi kwa utawala wa Hayati Magufuli

Mpaka mwaka unaisha Bavicha wwtakuwa wanajadili tu ishu ya sabaya
 
Aliyekwenda angekuwepo leo hii Sabaya angekuwa mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro/DSM/Dodoma/Arusha, na kila siku angekuwa anamwagiwa masifa kuwa ni mchapakazi na mzalendo!! Hawa watu wanaopenda kujiita wazalendo wa kuogopa sana
Kabisa. Siku zote anaejinasibu sana kuhusu kuwa mzuri sana kwenye jambo basi ujue ndio kinyume chake. Daima ukiona mtu anatumia nguvu nyingi sana kuaminisha watu kuwa yeye ni mcha Mungu basi ujue hapo ni kinyume chake. Halkadhalika na swala la uzalendo wa kufanya kwa maonyesha siku zote huwa ni ukanjanja tu.
 
Hukumu iliyotolewa jana kwa Ole Sabaya, kuwa alikuwa jambazi la kutumia silaha kupora mali za wananchi, vile vile limeupaka matope utawala wa Magufuli.

Kwamba mteule wa Rais, akafanya mambo kinyume na utawala wa sheria, na mbaya zaidi ujambazi, ni vigumu kueleweka kirahisi kwa nini haya yaliruhusiwa kutokea.

Utawala wa Magufuli mara kadhaa umelaumiwa kutoheshimu haki za binadamu na mali zao, huu mfano wa Sabaya umejitokeza kukubaliana na hoja hizo.

Kwamba kulikuwepo na wasiojulikana, watu kutekwa na baadaye aidha kupotea au kurudishwa na wasiongee yaliyowasibu, hili la Sabaya linathibitisha uhusika wa viongozi fulani, ndani ya Dola, wakiwa na baraka " kutoka juu".

Kwa vyovyote vile Ole Sabaya ni doa jeusi na ambalo si zuri kwa utawala wa Magufuli.

Nafikiri ni ka DAGAA tu kati ya ma KAMBALE! Huyu alikuwa mporaji wa kutumia silaha, ila kuna walio ondoa uhai wa watu kabisa! Kuna walio tumia silaha za kivita hadharani kwa makusudio ya kutoa uhai (mfano swala la Lissu). Kulikoni haka ka DAGAA tu? Ma KAMBALE wanadunda mitaani na wengine bado wako kwenye utumishi wa umma!!! Inafahamamika wazi kuwa huyu DAGAA alimdharau sana RC +Mugwira, pengine dharau hiyo ilikuwa extended pia kwa Makamu wa Rais Samia enzi hizo?
 
Wasiojulikana wote wasakwe waletwe kwa pilato baba yao amekufa hawana Kinga dhidi ya jina.Wasiojulikana wa dikteta Yahaya Jameih wa Gambia wanasota jela.
Jamii inawafahamu iruhusiwe watajwe
 
Silo baada ya kumkamata makonda anamkamata mbowe
 
Nijuavyo Mimi rais huteua akisaidiana/akishirikiana na makamu wake hivyo mamlaka za uteuzi zilizomtuma 7ya kupora kwa silaha tena zamoto Hangaya naye anahusika!!

Kama mhusika namba moja yukoheli huyu nambambili mbona anajikausha?? Aseme anajua nini kuhusu kutuma wavamizi wenye masilaha. Kwakuwa tuko hukohuko walikovamiwa aeleze ilikuwaje watz tusiwe majinga
Kamavp katiba mpya nimuhimu sana ikaundwakuepusha uovu kama juu namingine mingi tuliyoiona na tunayozidi kuiona.
Nb. Godbless Lema ni prophet kuliko maprophet wooote hapa bongo aliona kifo cha mteuzi (jiwe) na yatayomkuta jambazi aloteuliwa (7ya). Bado yasupwika tuendelee kusali sirini watenda mabaya wooote waanguke kwa aibu
 
Mbowe yeye anatuhumiwa kupanga mipango miovu ya kuvuruga AMANI YA nchi.
sasa wewe jiulize mtu anaye taka kuvuruga amani ya nchi unajua madhara yake ni makubwa kiasi gani?! ni hatari kubwa sana na kama akikutwa na hatia anastahili adhabu kali zaidi ili iwe fundisho kwa wanasiasa wengine wanao jaribu kuchezea amani ya nchi
yaani huwezi kulinganisha makosa ya unyanganyi, n.kna makosa ya mbowe ya kupanga njama za kuvuruga amani ya nchi, Amani ya nchi ndio inayo tufanya leo tunafurahia haki kutendeka, amani ya nchi ndio mpango mzima, leo hii Mbowe na Genge lake la kihalifu wanadaiwa kupanga njama za kuvuruga amani ya nchi iliyo tengenezwa na kulindwa kwa zaidi ya miaka 60!!
Amani ya nchi yetu ni ya thamani kubwa sana kuliko mbowe au mtu yeyote yule, atakaye bainika kuchezea amani yetu atashughulikiwa bila huruma.
Utapiga kelele weeee lakini hutafanikiwa kumpakazia Mbowe uongo huo uliotukuka! Mbowe siyo gaidi bali mhanga wa viongozi mafisadi yasiyo heshimu katiba na sheria za nchi!
 
Kabisa. Siku zote anaejinasibu sana kuhusu kuwa mzuri sana kwenye jambo basi ujue ndio kinyume chake. Daima ukiona mtu anatumia nguvu nyingi sana kuaminisha watu kuwa yeye ni mcha Mungu basi ujue hapo ni kinyume chake. Halkadhalika na swala la uzalendo wa kufanya kwa maonyesha siku zote huwa ni ukanjanja tu.
True, wanasema hata wachawi ndiyo wanaopenda kukaa viti vya mbele church
 
Utapiga kelele weeee lakini hutafanikiwa kumpakazia Mbowe uongo huo uliotukuka! Mbowe siyo gaidi bali mhanga wa viongozi mafisadi yasiyo heshimu katiba na sheria za nchi!
vipi kuhusu Gaidi Mbowe ambaye kwa muda mrefu amekitumia chama kama kichaka cha kutekeleza uhalifu, ugaidi, ujambazi wa kuvuruga amani ya Nchi na hata mipango ya kuuwa viongozi?!
kwa muda wote huo alipo kuwa mwenyekiti wa chama, je, unajua katengeneza wahalifu wangapi?
Mbowe anaweza kuwa mtu hatari sana kwa Nchi huenda kuliko hata huyo sabaya.
 
Mbowe yeye anatuhumiwa kupanga mipango miovu ya kuvuruga AMANI YA nchi.
sasa wewe jiulize mtu anaye taka kuvuruga amani ya nchi unajua madhara yake ni makubwa kiasi gani?! ni hatari kubwa sana na kama akikutwa na hatia anastahili adhabu kali zaidi ili iwe fundisho kwa wanasiasa wengine wanao jaribu kuchezea amani ya nchi
yaani huwezi kulinganisha makosa ya unyanganyi, n.kna makosa ya mbowe ya kupanga njama za kuvuruga amani ya nchi, Amani ya nchi ndio inayo tufanya leo tunafurahia haki kutendeka, amani ya nchi ndio mpango mzima, leo hii Mbowe na Genge lake la kihalifu wanadaiwa kupanga njama za kuvuruga amani ya nchi iliyo tengenezwa na kulindwa kwa zaidi ya miaka 60!!
Amani ya nchi yetu ni ya thamani kubwa sana kuliko mbowe au mtu yeyote yule, atakaye bainika kuchezea amani yetu atashughulikiwa bila huruma.
Ni busara kujadili mada iliyopo, doa jeusi linaloiandama Awamu ya Tano.
Kuchanganya haya mawili, aidha mtu huna akili au unajiridhisha kutaka kujipa kiki ya ujasiri ili kuhimili kwa yaliyotokea.
 
Mleta mada usisahau kuwa 90% ya top Govt Officials wa sasa ni wateule wa our beloved The Late Magufuli kuanzia Rais Mamá Samia, Dr Mpango, PM Majaliwa, Jaji Mkuu Prof Ibrahim, DG Tiss, CDF, IGP na wengine wengi

Maamuzi ya kesi ya Sabaya isiihusianishe na mkuu wa Serikali iliyopita ilhali watendaji wakuu wengi kama nilivyowataja wenye influence bado ni wale wale toka awamu iliyopita na ni wenye kiwango kizuri cha kukubalika kwa maana ya utendaji wao ktk nchi yetu

Kama Sabaya alifanya makosa basi acha hukumu imuhusu yeye kama yeye
Ni kweli mbele ya sheria nao wana sehemu ya hilo doa jeusi.
Yakitendeka haya , WALIKUWA WAPI?
Je hako za wananchi na haki za binadamu ni utashi wa mtu/kiongozi?
Iundwe kamati ya klijadili hili ili wananchi wajiridhishe juu ya umakini wa vyombo vyao vya kutetea haki zao.
 
vipi kuhusu Gaidi Mbowe ambaye kwa muda mrefu amekitumia chama kama kichaka cha kutekeleza uhalifu, ugaidi, ujambazi wa kuvuruga amani ya Nchi na hata mipango ya kuuwa viongozi?!
kwa muda wote huo alipo kuwa mwenyekiti wa chama, je, unajua katengeneza wahalifu wangapi?
Mbowe anaweza kuwa mtu hatari sana kwa Nchi huenda kuliko hata huyo sabaya.
Hakuna mahakama yo yote ambayo imethibitisha tuhuma hizi za ugaidi kwa Mbowe. Hayo ni mawazo ya polisi ambao kimsingi imethibitishwa hawajui kanuni za msingi za utendaji wao wa kazi (Police General Orders - PGO)

Kilichothibitishwa mahakamani bila chenga ni kuwa SABAYA NI JAMBAZI LA KUTUMIA SILAHA!
 
Nafikiri ni ka DAGAA tu kati ya ma KAMBALE! Huyu alikuwa mporaji wa kutumia silaha, ila kuna walio ondoa uhai wa watu kabisa! Kuna walio tumia silaha za kivita hadharani kwa makusudio ya kutoa uhai (mfano swala la Lissu). Kulikoni haka ka DAGAA tu? Ma KAMBALE wanadunda mitaani na wengine bado wako kwenye utumishi wa umma!!! Inafahamamika wazi kuwa huyu DAGAA alimdharau sana RC +Mugwira, pengine dharau hiyo ilikuwa extended pia kwa Makamu wa Rais Samia enzi hizo?
Hilo nalo neno!
Mimi si Chadema , ni mtanzania na mzalendo.
Suala la Lissu(pamoja na kwamba sipatani na hoja zake nyingi) lazima ichunguzwe ili wahusika watiwe mbele ya mkono wa sheria.
Tetesi za kwamba Makonda anahusika zisipuuzwe.
 
Back
Top Bottom