Freeman,
(1). Kwanza ni rafiki yangu, na ninajua kuwa ni wachangiaji wawili tu hapa wanaomjua personally, Bob na Jasusi, lakini ninaamini kuwa part yake ya siasa ninaifahamu kuliko wengine wote. Free is a good man na ni visionary man, nimemuona kwa macho yangu akiigeuza Mbowe Hotel kutoka just another Guest house mpaka kuwa Hotel ya kweli, na mpaka sasa Bilicanas. Hata siku moja siwezi kusema Free ni msaliti, hapana! lakini I believe kuwa within his heart Free ni CCM, cham cha marehemu baba yake, na ni kupitia Azimio la Arusha ndipo baba yake aliweza kuinunua hilo jengo kupitia (CCM-TANU), baada ya kazi kubwa ya mzee Haikaeli kumsaidia sana Mwalimu enzi zile.
Katika uchaguzi uliopita CCM kama kawaida yao, waliingia na full gears, lakini toka baada ya Dodoma kulikuwa na wasi wasi mkubwa ndani ya CCM kuwa wananchi walioendelea ni vigumu kumpigia kura mgombea wao, maana hakuwa na record, na mikoa iliyoendelea sio siri inafahamika kuwa ina wananchi ambao sio rahisi kuwadanganya, na sio siri Free aliwika sana kwenye hiyo mikoa, sasa matokeo ya uchaguzi ndiyo yaliyowashangaza sana CCM, kwani hakuna aliyetegemea kuwa Freeman angepata kura chache vile, na mpaka leo hii hakuna anayeelewa exactly what happened? Na hata Freeman mwenyewe haelewi ni nini kilitokea? Sio kwamba angeweza kushinda, no! lakini ilitegemewa kuwa wabunge wengi wangetoka Chadema, ukweli ni kwamba hata mimi binafsi niliamini kuwa bunge lingekuwa nusu kwa nusu, kati ya CCM na Upinzani na hasa Chadema, kwa hiyo yes!, wakati wa uchaguzi Free alikuwa tishio lakini matokeo yalimaliza kabisa nguvu yote ya Free kisiasa kwa maoni yangu, na Chadema itafanya makosa makubwa kumsimamisha tena uchaguzi ujao.
Freeman alikuwa ni a strong candidate kuliko wote waliogombea kwa maoni yangu, na JK alikuwa ni the weakest candidate, Free alikuwa na strong political points kuliko wote, lakini tatizo ni kuwa alikuwa peke yake mtu mmoja, akiwa Songea maana yake ni Chadema nzima iko huko, as opposed to CCM! Halafu vyama vyote upinzani vinaendelea kuwa tatizo moja sugu, nalo ni kwamba wako mijini tu! Hawako vijijini, kura karibu zote za CCM zinatoka vijijini, kama vile kura za Bush kwenye uchaguzi wa mwisho zilitoka vijijini. Halafu Free alisindwa kuzi-simplify point zake ili zieleweke na wananchi wa chini, kwa mfano majimbo ilikuwa ni a very strong one kuliko zote alizokuwa nazo, lakini baada ya kushindwa kuisema vizuri CCM wakai-simplify kuwa ni chanzo cha kuleta ukabila na udini na wananchi wakakubali kuwa ni kweli!
(2). Kufunga magazeti yasiyokuwa na muelekeo ambayo kazi ni kuwapotosha tu wananchi na kupandikiza chuki za bure miongoni mwa wanajamii ni hatua moja muhimu sana katika kufanikisha kuwaelimisha wananchi na taifa na kuwaamsha kisiasa, wewe mwenyewe unajua kuwa tatizo letu kubwa bongo ni wananchi wasioelewa kitu chochote, wakipewa pilau tu wanakuja na kukupa kura! Media ni a very powerful tool ya kuwapotosha wananchi,
ninasema haya magazeti yazungumzie our real problems, kama vile rais kusafiri na wajumbe 50, yaulize EL alikwenda kufanya nini huko Majuu ambalko rais tayari alikuwa huko majuzi tu, magazeti yaulize ni nani aliyeruhusu wabunge kupewa shillingi millioni 40 za magari, badala ya 30 kama ilivyokuwa ni nani aliyeruhusu nyongeza ya millioni 10? Magazeti aulize ni kwa nini tunjenga bunge jipya na wakati tuna Karimjee na Dodoma tayari, wakati hospitali zetu zinatisha kwa uchafu na umasikini? Wananchi wanahitaji kujua ni kwa nini tunagawana umeme? Yapige kelele kuhusu mikataba mbuzi? Wote tumeona jinsi Media ilivyosimama kidete juu ya nyongeza za wabunge mpaka rais mwenyewe akaogopa na kujitoa kuwa yeye hahusiki, sasa kwa nini wasifanya hivyo kwenye issue zote? Badala yake wanakuja kuandika ujinga, I mean NONESENSE! CCM kummaliza Free wanahitaji kukaaa kikao kizima cha CCM?, badala tu ya kumtumia TRA kufunga biashara zake? I mean ukifunga biashara za Free basi na siasa zake zimekwisha kwa sababu aslimia 80% ya shughuli zake za kisiasa Free anatumia hela zake binafsi kwa hiyo akiwa tatizo ni kufunga njia za kuingia pesa zake!
Kwa hiyo mzee kuhusu magazeti, kinyongo changu ni kuwa hayazungumzii real issues ambazo ni muhimu kwa wananchi, na ndio maana hayauzi tena siku hizi, yamebakia kutegemea vikundi vya vyama vya siasa! Isipokuwa kama wananchi kama wewe wanaona kuendelea kuandika ujinga badala ya issues ni sawa, basi yadumu!
(3). Mzee Jasusi,
Swali la mil 40, ninaona mzee Bob amelijibu vizuri, kuhusu sera ni kweli sera almost zote za JK, originally zilikuwa za Free lakini akaweza kuziwahi na kuzigeuza kuwa zake, kama vile Bill Clinton alivyokuwa akiwafanya Republicans, kwa mfano ile issue ya Welfare mwaka 1996, politically sio dhambi ila sasa tatizo linakuja utekelezaji, sasa magazeti yetu yalipaswa kuanza kumuuliza JK vipi zile ahadi za ajira millioni moja kwa mwaka au mwezi?
Kwa kumaliza ninasema kuwa Free alijitahidi, na laifanya kazi nzito na inahitaji kupewa heshima, lakini katika siasa tunaangalia umeangukia wapi sio umeangukaje! Ndio maana huko majuu uchaguzi ukiisha tu, kina Gingrich wanaambiwa wajitoe waingie wengine, huu ni wakati muafaka kwa Free na chadema kuanza kumpromote JJ, na wengine, Free akae pembeni na kuendeleza chama chake, mamboi mengine kama ninavyosema siku zote siwezi kuyaingilia kiundani mno maana tunamuamini Mungu na kufunga milango ya magari yetu!