Mwanasiasa,
Kumjua kwako Free kisiasa na kutomjua kwangu as of your claim, haibadili ukweli kwamba alishindwa vibaya sana katika uchaguzi uliopita na kwamba yeye personal au chama chake, sio tishio kwa CCM, na hasa Mtandao!
Upinzani pamoja na Free na nyinyi wote wa Chadema mna safari ndefu sana mbele yenu, kwa sababu Watanzania ni lini watawachukulia nyinyi kuwa serious! Kitu kidogo tu kama kuungana kinawashinda I mean so far kitu kimoja tu kidogo cha kuwa-convince wananchi hakuna? Unajua you are right sihitaji kuujua upande wa siasa wa Freeman baada ya kuona Helikopta, guess what? Wananchi wamekataa kuwa Helikopta sio hoja, ni afadhali CCM ambao sio perfect lakini hawana helikopta!, ndio maana ya kura za 80%, leo 2006! Aibu!
Ni kweli mimi kama wananchi wengine hatujui the political side ya Freeman ndio maana tumekataa kumpigia kura, hatujui kwa sababu ameshindwa ku-communicate as politician tukamuelewa, yaani point yako inamfanya hata JK aliyekuwa haaahidi tu kuwa na nafuu kuliko asiyeweza kueleweka kabisaaa, maana angalau wananchi walimuelewa JK ingawa utekelezaji ndio hivyo!
CCM as chama kina mikakati na mipango yake, so tuntegemea na upinzani nao wawe nayo sio kulia lia tu where does it stop? Toka vimeanzishwa ni kulia aaaaaaa tu yaani unajua kuna wananchi wameanza kuamini kuwa huenda kulia lia ni moja ya fundamentals za kuitwa chama cha upinzani. Lets say hili gazeti linasema ukweli kama unavyoamini, now kwa nini upinzani nao wasikae kikao na kuanzisha mbinu za kuiua CCM?
Lets say, ni kweli Mzee Jakaya Kikwete rais wa Jamhuri, ameitisha kikao cha NEC, CCM na kuwaomba wajumbe 2,000 msaada wa namna ya kummaliza Freeman na Chadema, aliowashinda kwa kura 80% katika uchaguzi ulioisha karibuni, sasa anawaomba wamsaidie kummaliza ksisiasa maana ni tishio sana katika utawala wake, hebu tuseme kama unavyosema kuwa ni kweli, je kuna sheria ya nchi Tanzania iliyovunjwa?
Unajua na nyinyi upinzani wakati mwingine ni nyinyi wenyewe mnajivunjia heshima mbele ya wananchi, hivi kweli kuna Mtanzania au mbongo anayeweza kuamini kuwa huu ujinga uliondikwa na hili gazeti kuwa ni ukweli? Si kuna maswali ya kujiuliza tena ya haraka haraka, Je kuwa mmaliza BM, JM, SAS, Mangula, Mwandosya, JK alifanya kikao na kumuomba nani msaada? Mbona hli gazeti halikujua? Imekuwaje mpaka likajua hii ya safari hii ya kummaliza mtu na chama alivyovishinda tayari?
I mean CCM sio malaika, na mimi sio mnazi wa kupenda tuu kama mjinga lakini jamani upinzani hebu njooni na issues, real issues, sio huu ujinga, tena ninawatahadharisha kuwa mkifanya mchezo hawa CCM watatawala milele, yes look at your issues? Wabunge wenu wanakuja bungeni na kusema upumbavu usiokuwa hata na miguu, eti viongozi wa CCM wana nyumba SA, get real guys hawa wanaiba hela mbuzi tu za kuweza kujenga Mbezi na kujiuzia nyumba za serikali, za kununua nyumba Madiba au bondeni hawana, labda mmoja tu Yona ambaye ninajua kuwa ana nyumba DC, otherwis eni hadithi za chooni tu!
Nyinyi upinzani kina Mwanasiasa na wenzio kazaneni muimarishe vyama vyenu, hawa wafanya biashara kina Mtei, Ndesamburo, Lwakatare, Slaa, na Freeman wanachotafuta ni masilahi yao tu, toka hivi vyama vianze ninaamini viongozi genuine walikuwa ni Brown Ngwilulupi, Kaborou, na sasa JJ, basi wengine wote ni watafutaji tu kama CCM, kwa hiyo chungeni tena msije kushangaa kuwa wakati mnabishania huu ujingwa wa hlili gazeti wenzzenu walikuwa wanapitisha sheria za mkao wa kula zaidi! Haya magazeti uchawara hayawezi kuwa ndio chanzo cha agenda zenu kisiasa mnahitaji more than this kuwashawishi wananchi, ama sivyo mtakuwa on defensive side daima, kama alivyosema Chadema mwenzio hapo juu jitahidini kuweka mikakati ya kuiweka CCM on the defensive katika issue muhimu, lakini sio hizi issue za kubuniwa kati ya makundi ya CCM na upinzani!
Halafu mumwambie Freeman kuwa aache kukata deal kama ile ya kumuachia Mzee JK, kama angeshindwa CCM au mnafikiri tumesahau, ilikuwaje akakata naye deal si ndio ufanya biashara wenyewe huo? Halafu leo eti huyo JK aliyefanya naye deal kupitia kwa Kingunge, sasa amebadilika anataka kummaliza na mnategemea sisi wabongo ni wajinga sana tuamnini hayo mazingombwe? Acheni filimbi vijana fanyeni kazi za kuimarisha vyama vyenu vibovu na uchwara, kazi kukimbilia Ikulu tu! na kugombea ruzuku, na kuwasaliti wananchi kina Marando!