Man! go home!
(1). Mazingira magumu ya serikali yanawafanya upinzani wasiwe wanavyotakiwa? What a joke? Kule Kenya Moi aliwapa mazingira safi? Kina Mandela walipewa mazingira safi na makaburu? Chiluba alipewa mazingira safi na Kaunda? Mlitegemea CCM, chama kilichotawala for the last 44 years kitawapa madaraka kama kununua samaki sokoni? Je CCM ilimuwekea JK mazingira mazuri? Sasa umafiya ulikuwa wa nini?
(2). Serikali ya nchi yoyote duniani haiwezi kutishwa na agenda za upinzani zisizokuwa na kichwa wala miguu, tena za kuwekwa chini na magazeti kama Mtanzania, ambalo toka lianzishwe ni habari za Freeman tuuuu jinsi alivyo tishio kwa CCM, na walioonewa kwenye uchaguzi wa rais wa CCM Dodoma, basi halina lolote la muhimu kwa wananchi! Rai ndio kabisaaa, wakimnyima tu uraia, na kumtoa kwenye kampeni za rais ndio ananza kuandika hoja muhimu, wakimpa tayari ni kusifu tuuuu, Mengi na IPP ndio hivyo akithubutu tu atalipa madeni yote anayodaiwa na makaburu, na upinzani wenyewe ndio hoi bin taabani, halafu mnashangaa wananchi wanampa JK kura 80%, ni kwa sababu upinzani bado hawajapa sababu ya kuchagua tofauti, sio mazingara magumu, hayo yalianza pale tu upinzani ulipoanzishwa na kumbuka ulianzishwa baaada ya kupewa ok na Mwalimu, muanzilishi wa CCM, sasa mlitegemea nini? Hawa kina Mrema walipokuwa wanakwenda kujikomba kwa Mwalimu, walikuwa wanategemea nini? Kuwa Mwalimu na CCM watawapa tu power bureeee? bila kutoa jasho?
(3). Katiba ya nchi yetu ni mbovu na ndio mwanzo wa upinzani kuishiwa nguvu, great! Je upinzani wamefanya nini kukabiliana na hili tatizo la katiba? Look at CCM kila siku wana mapya ya kuwakandamiza upinzani na kuendelea madarakani, yaani upinzani hamuwezi hata kugomea kupigia kura miswaada mbuzi? Hamuwezi hata kukataa kuongezewa hela bila sababu, shillingi millioni 10 za kununulia magari? Hivi kweli mngezigomea hizi hela si angalau wananchi wangeshituka kuwa na nyinyi mko bungeni?? Hii issue ya nyongeza za marupu rupu ya wabunge imekufa only kwa sababu baadhi ya viongozi wa CCM waliikataa, lakini sio kwa sababu ya upinzani, WHY na hizi ndio hasa issues ambazo tunazisikia dunia nzima zikiwapa upinzani ujiko? Juzi umesikia huko Nepal upinzani walivyoweka mguu chini, mpaka mfalme analia kwenye TV!
((4). Yes, ni mimi niliyesema kuwa sitajiunga na hii forum kwa sababu ni ya Idd Simba, nilisema na baadaye nikajiunga nayo na ninaweza nikatoka wakati wowote kwa nafasi yangu, na sikuvunja sheria ya nchi au ya hii forum? now what is your problem? Sasa wewe mwenye hii forum mbona sijaliona jina lako toka niingie humu? Yaani nyinyi upinzani hamna jipya kazi kulia tuuuuuu, sasa hata unalia eti kwa nini nimeingia hii forum, tena wewe ni mpinzani wapili kuuliza kwa nini nliingia hapa, maana yake ni kwamba kuna mnaotaka hoja za kubembelezana, yaani hamuwezi kuacha hiyo tabia ya kulia lia tu, mimi nilifikiri ungekuwa na shukrani kuwa hii forum ambayo posting zilikuwa kwa siku mbili au tatu sasa ni kwa masaaa, mpaka kwa dakika mpaka wakati mwingine posting zinapandana, sasa nenda huko kwingine amabako hatupo uone, kuna moja niliingia kuchungulia tu yaani posting ya mwisho ilitumwa January! kuwa na shukrani kijana, huwezi malumbano kaa pembeni waachie wengine wanaoweza,
Ukweli utaendelezwa kuwa upinzani bongo ni a big joke, leo 2006 hakuna nchi duniani rais anachaguliwa kwa kura 80%, hata China ambako hakuna upinzani bado rais hapati kura 80%, just simple as that, hakuna! Maana yake ni kwamba upinzani ni hakuna, maana yake ni kuwa viongozi wa upinzani bongo ni CCM watupu na wafanya biashara, Yes! that is exactly what is means! fungeni virago and go homee! Upinzani gani? Hawa kina Morales, Vincente Fox, unajua mambo waliyoyapitia mpaka kuwa marais toka upinzani? Kina Chavez wameshafungwa jela kwanza ndio wakawa rais sio kulia lia tuuu na kulaumu wanabodi wasiokuwa upande wako wanatafuta nini hapa, jibu mapigo kijana hakuna watoto hapa, unafikiri kwa nini BCS ilifungwa, Mzee Mwanasiasa si uliwahi kuuliza kule BCS kuwa hizi forum zitaweza mitulinga ya kina ES?, yes here I am halafu siendi kokote bro, it is tough!