Olympic 2024 France: Maonesho ya Ufunguzi yashutumiwa kuonesha viashiria vya ushetani na upinga Kristo

Walio kuletea hizo dini wala hawalalamiki.

ila wewe mwafrika mtu wa kolomije huko unajifanya kutetea kitu ambacho, Haohao walio kileta wapo comfortable nacho.

Rudi kwenye asili yako na achana na hizo dini za kuletewa.

Sasa wewe unahangaika kubadilisha kitu ambacho uli letewa badala ya kuachana nacho?

Waafrika wengi huko vichwani mwenu kumejaa matope, mna hangaika kutetea imani na dini za kuletewa badala ya kuachana nazo.

Bure kabisa!!
 
Sawa
 
Tuko katika siku za mwisho mwisho kabisa kabla ya tukio la unyakuo wa kanisa la Mungu na kuachiliwa kwa utawala wa mpinga Kristo duniani. Najua humu wengi watabeza lakini kwa wasomaji na wachambuzi makini wa Biblia wanaweza kuelewa unabii wa siku za mwisho unatimia kwa kasi ya ajabu.

Najua hiyo last supper picha ni ya kubuni lakini watu wakiamua kukufuru watatumia chochote mradi ujumbe wa kukufuru umetimizwa na hii sio lazima wanaotekeleza wawe wanaelewa wanachofanya isipokuwa ni maroho machafu yanawavaa.

Miaka ya karibuni sherehe za michezo au festivals kubwa kubwa zimekuwa zikiambatana na maudhui ya kumkufuru Mungu kwa makusudi na watu huchukulia ni jambo la kawaida au labda halihusiani na Mungu.

Uovu ni mwingi sana, kanisa la Mungu duniani na lenyewe liko hoi, wahubiri wa kweli wanapungua na manabii wa uongo wamezuka wengi sana na Yesu alisema; MATHAYO 24:22 Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo.

Kwa wafuatiliaji wa wahubiri wa kweli waliobaki asilimia kubwa ya mahubiri yao ni kuwaandaa watu na kurudi kwa Yesu. Yesu anarudi lakini anakuja kuchukua walio wake kweli kweli, watakaobaki watakutana na kitu kinachoitwa dhiki kuu.
 
Unaongea ujinga ujinga tu.., wewe unaona kila unachokitaka, wengine tunaona clowns na mang’ombe tu hapo, nothing more
 
Matumizi ya watu wa upinde kama

Marastafari kwao upinde ni ishara ya upendo na amani

Katika biblia upinde : inasema: Mwanzo 9:12-15 “Mungu akasema, Hii ndiyo ishara ya agano ninalofanya kati yangu na ninyi, na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, agano la vizazi vyote vijavyo; mawingu, nayo itakuwa ishara ya agano kati yangu na dunia.

Na katika baadhi ya imani Upinde wa mvua angani inasemekana Simba anazaa muda huo

South Afrika alama ya upinde wa mvua ni kauli mbiu ya umoja baina ya raia wa Afrika ya Kusini wenye nasaba ya weusi, chotara, wazungu, wahindi, wachina

Hiyo ni mifano michache kati ya lukuki, sasa kikundi au jamii moja kujimilikisha alama ya upinde wa mvua na kutaka wote tuamaini mambo yao ni upungufu wa maarifa.
 
Badala ya kupambana kutokomeza umaskini, uhujumu uchumi, wizi, ufisadi na ubadhirifu wa mali za umma uliokithiri barani kote Afrika,

Mnahangaika na maisha ya wazungu ambayo hayawasaidii na haisaidii kubadilisha chochote kile nchini kwenu.
 
Wanajua nyakati za mwisho zimekaribia, wanafanya kila wawezalo kumuudhi na Kumkosea Mungu
 
Hapo nimemaanisha watu wa transgender
 
Sijafurahishwa na kitendo hicho, kwani ni dharau na kebehi kwa maudhui yanayo fanana na yale ya Kristo
Hayo mauzui ya kristo uliyoyaona jana yako ukurasa wa ngapi kwenye biblia.maana ata hiyo picha ilichorwa na leonado da vinci kwa mtazamo wake.Sasa waliokuletea hiyo biblia ndio hao hao waliofanya hilo tukio.sasa wewe kinakuuma kitu gani au ndo kusema umekua mkristo kuliko wao?
 
Ndugu yangu wewe fata yako na ya maisha yako tu dunia imekwishaa kwishaaa kabisaa
 
Pia wanajaribu ku mock siku za mwisho kwa kufanya matukio yanayo fanana na siku hiyo... Mfano walionesha tukio hili 👇


Kisha nikaona mbingu zimefunguka, na nikamwona farasi mweupe. Mpanda farasi aliitwa Mwaminifu na Kweli, kwa sababu ni wa haki katika maamuzi yake na kufanya vita
Ufunuo 19:11
 
Hayo mapicha aliyachora Leonardo Da vince ambayo mtaani wanasema alikuwa shoga.Kanisa lioiyaiba na kuyatumia.Hayana uhusiano na Mungu
 

Ni upumbavu wako tu kufikiri kwamba hiyo picha ina uhusiano na Kristo, actually ni kufuru kwa hao waliompa Yesu hiyo picha na huo mwonekano!
 
Mkuu dini zenyewe walituletea wenyewe na ushoga wameleta wenyewe. Kazi yetu sisis waafrica ni kupokea tu maana hatujielewi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…