Olympic 2024 France: Maonesho ya Ufunguzi yashutumiwa kuonesha viashiria vya ushetani na upinga Kristo

Olympic 2024 France: Maonesho ya Ufunguzi yashutumiwa kuonesha viashiria vya ushetani na upinga Kristo

Humu JF kuna mawakala wengi wanaotulazimisha tusiamini uwepo wa Mungu. Kama wao hawaamini, wasitulazimishe sisi tusiamini pia.

Hakuna mwanaume chini ya Jua akiwa na akili timamu ataruhusu kupigwa pumbu au kumpiga pumbu mwanaume mwenzake.

Ushoga ni roho kamili, ni ushetani. Aache mbwembwe anayekutisha kwa hoja za kitoto.
Sasa naelewa kwamba watetezi wa hayo mambo nao ni wahusika pia
 
Umepanick tayari.
Naanzaje kupanick kwa ajili ya wewe kuunga mkono vitendo vya kishoga? Mimi nakusikitikia tu

Jamii tunakemea wewe unasema tunajipendekeza. Nimesikitika sana sikutegemea kuwa wewe ni mtu wa hivyo
 
Shetani yuko tangu enzi za Adamu na Hawa pale bustanini
Unaweza kuthibitisha uwepo wa huyo shetani na si hadithi za vitabuni tu?

Wewe unatetea ushoga ni mtu wa hovyo sana
Wapi nimetetea ushoga?

Shetani hamfanyi mtu awe shoga ila amefanya ushoga uonekane kuwa jambo la kawaida kwa watu kama nyinyi
Wapi huyo shetani amefanya ushoga uonekane kuwa ni jambo la kawaida?

Kama huyo shetani hafanyi mtu awe shoga, Utasemaje huyo shetani amefanya ushoga uonekane ni jambo la kawaida?
 
Wanatambika na kuchinja mbuzi na kumwaga pombe makaburini?
Matambiko yapo ya aina nyingi mkuu. Usidhani kila mtu anatambika kwa kuchinja mbuzi na kumwaga pombe.

Wazo kuu ni matendo yanayofanyika na nia inayokusudiwa.

Kwenye biblia, waisraeli walichinja kondoo, wakapaka damu kwenye milango kwa nia ya kujiepusha na mauaji ambayo huyo Mungu wenu alikuwa anajiandaa kuyafanya.

Hiyo unaona poa ila wachagga wakichinja mbuzi huko makwao unaona ni matambiko mabaya.
Kwanini?
 
Matambiko yapo ya aina nyingi mkuu. Usidhani kila mtu anatambika kwa kuchinja mbuzi na kumwaga pombe.

Wazo kuu ni matendo yanayofanyika na nia inayokusudiwa.

Kwenye biblia, waisraeli walichinja kondoo, wakapaka damu kwenye milango kwa nia ya kujiepusha na mauaji ambayo huyo Mungu wenu alikuwa anajiandaa kuyafanya.

Hiyo unaona poa ila wachagga wakichinja mbuzi huko makwao unaona ni matambiko mabaya.
Kwanini?
Kutambika sio tu kuchinja, ni kuomba na kuabudu mizimu au wafu, kwa upande wa dini wanachinja wanyama lakini hawaombi wala kuabudu mizimu
 
Humu JF kuna mawakala wengi wanaotulazimisha tusiamini uwepo wa Mungu. Kama wao hawaamini, wasitulazimishe sisi tusiamini pia.
Kuna mtu amekulazimisha au alikulazimisha usiamini uwepo wa huyo Mungu?
Hakuna mwanaume chini ya Jua akiwa na akili timamu ataruhusu kupigwa pumbu au kumpiga pumbu mwanaume mwenzake.

Ushoga ni roho kamili, ni ushetani. Aache mbwembwe anayekutisha kwa hoja za kitoto.
Ushoga ni Tabia chafu za mtu binafsi kama ilivyo ulevi, wizi n.k

Hakuna uhusiano wa ushoga na Shetani.

Huyo shetani hajawahi kuwepo, hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.

Muache kutumia dhana shetani kama excuse ya tabia za kibinadamu.

Binadamu ana tabia njema na chafu.

Na hakuna kiumbe yeyote anayefanya binadamu awe mchafu au msafi.

Ni binadamu mwenyewe na maamuzi yake binafsi.
 
Kutambika sio tu kuchinja, ni kuomba na kuabudu mizimu au wafu, kwa upande wa dini wanachinja wanyama lakini hawaombi wala kuabudu mizimu
Bro, unajichanganya sana.
Nimekuonesha kwamba watu wa dini wanachinja kwa kunuia mambo fulani, hilo ni tambiko tayari.

Pia, ukisema watu wa dini hawaombi wafu ilutakuwa unachekesha umma.

Wakatoliki kwa mfano, wanaomba wafu wa kizungu usiku na mchana. Wamepewa jina; watakatifu. Haiondoi ukweli kuwa ni wafu tu a.k.a mizimu.
Wanavaa mpaka masanamu na picha za wafu wa kizungu kama Maria.
Na sasa Kuna mfu mmoja mcheza magemu anakaribia kutangazwa kuwa mtakatifu ili miafrika ianze kumuomba awajalie heri.
 
Nilitaka wanaounga mkono opening ceremony hiyo wajionee vitendo wanavyounga mkono na jinsi walivyo wajinga kukubaliana navyo
Screenshot_20240727-193622_X.jpg
 
Nilitaka wanaounga mkono opening ceremony hiyo wajionee vitendo wanavyounga mkono na jinsi walivyo wajinga kukubaliana navyo
Wewe unaye pinga na yule anayetetea wote mmeangalia mna tofauti gani sasa
 
Ninacho washutumu ninyi ni kuhusisha hayo matendo ya kibinadamu kusema ni ya kishetani ilhali huyo shetani mwenyewe hayupo.

Hakuna uhusiano wa shetani na tabia za wanadamu.
Wewe umesema haumini Shetani yupo.

Sisi tunaoamini Shetani yupo tunajua jinsi alivyo na ushawishi kwenye tabia za watu
 
Wewe umesema haumini Shetani yupo.

Sisi tunaoamini Shetani yupo tunajua jinsi alivyo na ushawishi kwenye tabia za watu
Olympics ilianzia kwa mungu Zeus, kwa nini unaangalia mashindano ya kishetani kwa kuanzia??
 
Back
Top Bottom