Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,771
- 41,027
- Thread starter
- #21
Nyani na Pundi, hoja zenu nakubaliana nazo kabisa. Lakini mnafanya makosa makubwa matatu.
a. Mnachukulia kana kwamba napendekeza tutilie mkazo kujiandaa kwa ajili ya Olympiki na tuache kufanya shughuli nyingine za kijamii na kiuchumi. Nitakuwa sina akili timamu nikipendekeza hivyo. Katika kujiandaa kufikia ndoto yetu suala hili la maandalizi ya olympiki ni sehemu ya shughuli za kijamii na kiuchumi siyo nje yake. Ninachopendekeza ni kwamba pamoja na mambo mengine na miradi mingine tunayoifanya tuongeze mradi huu maalumu wa kujiandaa na Olympiki 2012 kule London.
b. Kwamba napendekeza kiwango kikubwa cha fedha ambacho hatuwezi kukitumia kwenye michazo na kitasababisha dent kubwa kwenye uchumi wetu. Si kweli. Nimependekeza Shilingi bilioni moja kwa mwaka. Hizi shilingi bilioni moja kwa mwaka sisemi zitoke kwenye wizara ya elimu, au zitoke wizara ya afya, au wizara ya ulinzi au wizara nyingine yoyote ile. Hizi ni fedha ambazo zitatoka kwenye wizara ambayo tayari inapewa bajeti na wizara hiyo inaitwa ni WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI NA MICHEZO.
Sasa utaona siyo mimi ambaye ni Mtanzania wa Kwanza duniani kuleta michezo na kutaka itengewe fedha. Hata nchi maskini zinastahili kuwa na michezo. Tukifuata mtiririko wa hoja zenu ina maana tufute wizara ya michezo hadi tuwe na GDP kubwa zaidi na ya kuwa tufute michezo ili tujenge hospitali n.k.
Bajeti ya Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo tayari imeshatengwa na kupitishwa na Bunge ina Shs. Bilioni 21 kati ya hizo Bilioni karibu 10 ni za maendeleo. Sasa katika mipango ya maendeleo ya wizara hiyo tutumie basi angalau 'ka bilioni" moja kwa ajili ya kuanza kujiandaa na Olympiki. Ubaya wa hili ni nini? Kama fedha zimetengwa kwa ajili ya maendeleo ya michezo, kwanini zisitumike kuendeleza michezo?
c. Kosa la tatu ambalo mnalifanya ni kufikiri kuwa hatuwezi kumudu (afford) kutumia bilioni moja kwenye michezo kwa sababu ni nyingi sana na sisi ni masikini tuna vipaumbele vingine. Hoja hii inaweza kuwa kweli lakini ukija kuiangalia kwa karibu utaona haina nguvu sana. Tanzania inapoteza kwa mwaka asilimia 20 ya fedha yake ya fedha ya misaada kwenye ufisadi (corruption) (takwimu za USAID).
Kwa mwaka tunapoteza karibu Shs. Bilioni 400 kwenye manunuzi mabaya, kutofauta taratibu, mikataba mibovu ukosefu wa mapato kutokana ni misamaha ya kodi n.k Fedha zetu nyingi zinavuja kutokana na usimamizi mbaya wa fedha. Kimsingi hatuitaji kuomba fedha hizo bilioni moja kutoka nje au hata kuongeza kodi; tunachohitaji ni usimamizi mzuri wa fedha na kuhakikisha fedha zinazoibwa zinarudishwa na katika hizo tuzitenge kuendeleza michezo na kujiandaa kwa Olimpiki ya London 2012. Hapa kuna tatizo gani?
Shilingi bilioni moja siyo fedha nyingi ukizingatia matumizi yetu ya ajabu na usimamizi wetu wa fedha.
Mimi naamini tukitaka tunaweza. Tukitaka kutenga Bilioni moja kila mwaka kujiandaa kwa Olimpiki ya 2012 tunaweza. Na tukijiwekea lengo la medali 20 ingawa kwa wengine (kama Mtanzania) ni lengo gumu kwangu mimi nasema ni lengo halisia. Tukijiandaa na ikifika Olimpiki hiyo tukapata medali tano tu tutaona fahari kwani tumevuna tulichopanda na itaonesha kujiandaa kunalipa. Hizo medali tano zinaweza kuwa chachu ya sisi kufanya vizuri zaidi 2016.
Hivyo, tuungane mkono kujiandaa kwa Olimpiki 2012 kwa kuboresha mkakati nilioupendekeza hapo juu iili hatimaye Tanzania na yenyewe irudi kwenye medali za Olimpiki. Tukitaka tunaweza.
a. Mnachukulia kana kwamba napendekeza tutilie mkazo kujiandaa kwa ajili ya Olympiki na tuache kufanya shughuli nyingine za kijamii na kiuchumi. Nitakuwa sina akili timamu nikipendekeza hivyo. Katika kujiandaa kufikia ndoto yetu suala hili la maandalizi ya olympiki ni sehemu ya shughuli za kijamii na kiuchumi siyo nje yake. Ninachopendekeza ni kwamba pamoja na mambo mengine na miradi mingine tunayoifanya tuongeze mradi huu maalumu wa kujiandaa na Olympiki 2012 kule London.
b. Kwamba napendekeza kiwango kikubwa cha fedha ambacho hatuwezi kukitumia kwenye michazo na kitasababisha dent kubwa kwenye uchumi wetu. Si kweli. Nimependekeza Shilingi bilioni moja kwa mwaka. Hizi shilingi bilioni moja kwa mwaka sisemi zitoke kwenye wizara ya elimu, au zitoke wizara ya afya, au wizara ya ulinzi au wizara nyingine yoyote ile. Hizi ni fedha ambazo zitatoka kwenye wizara ambayo tayari inapewa bajeti na wizara hiyo inaitwa ni WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI NA MICHEZO.
Sasa utaona siyo mimi ambaye ni Mtanzania wa Kwanza duniani kuleta michezo na kutaka itengewe fedha. Hata nchi maskini zinastahili kuwa na michezo. Tukifuata mtiririko wa hoja zenu ina maana tufute wizara ya michezo hadi tuwe na GDP kubwa zaidi na ya kuwa tufute michezo ili tujenge hospitali n.k.
Bajeti ya Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo tayari imeshatengwa na kupitishwa na Bunge ina Shs. Bilioni 21 kati ya hizo Bilioni karibu 10 ni za maendeleo. Sasa katika mipango ya maendeleo ya wizara hiyo tutumie basi angalau 'ka bilioni" moja kwa ajili ya kuanza kujiandaa na Olympiki. Ubaya wa hili ni nini? Kama fedha zimetengwa kwa ajili ya maendeleo ya michezo, kwanini zisitumike kuendeleza michezo?
c. Kosa la tatu ambalo mnalifanya ni kufikiri kuwa hatuwezi kumudu (afford) kutumia bilioni moja kwenye michezo kwa sababu ni nyingi sana na sisi ni masikini tuna vipaumbele vingine. Hoja hii inaweza kuwa kweli lakini ukija kuiangalia kwa karibu utaona haina nguvu sana. Tanzania inapoteza kwa mwaka asilimia 20 ya fedha yake ya fedha ya misaada kwenye ufisadi (corruption) (takwimu za USAID).
Kwa mwaka tunapoteza karibu Shs. Bilioni 400 kwenye manunuzi mabaya, kutofauta taratibu, mikataba mibovu ukosefu wa mapato kutokana ni misamaha ya kodi n.k Fedha zetu nyingi zinavuja kutokana na usimamizi mbaya wa fedha. Kimsingi hatuitaji kuomba fedha hizo bilioni moja kutoka nje au hata kuongeza kodi; tunachohitaji ni usimamizi mzuri wa fedha na kuhakikisha fedha zinazoibwa zinarudishwa na katika hizo tuzitenge kuendeleza michezo na kujiandaa kwa Olimpiki ya London 2012. Hapa kuna tatizo gani?
Shilingi bilioni moja siyo fedha nyingi ukizingatia matumizi yetu ya ajabu na usimamizi wetu wa fedha.
Mimi naamini tukitaka tunaweza. Tukitaka kutenga Bilioni moja kila mwaka kujiandaa kwa Olimpiki ya 2012 tunaweza. Na tukijiwekea lengo la medali 20 ingawa kwa wengine (kama Mtanzania) ni lengo gumu kwangu mimi nasema ni lengo halisia. Tukijiandaa na ikifika Olimpiki hiyo tukapata medali tano tu tutaona fahari kwani tumevuna tulichopanda na itaonesha kujiandaa kunalipa. Hizo medali tano zinaweza kuwa chachu ya sisi kufanya vizuri zaidi 2016.
Hivyo, tuungane mkono kujiandaa kwa Olimpiki 2012 kwa kuboresha mkakati nilioupendekeza hapo juu iili hatimaye Tanzania na yenyewe irudi kwenye medali za Olimpiki. Tukitaka tunaweza.