Kaangalie kwa mm Australia aliuza hao kondoo hai na kwa nn sasa hivi hauzi wakiwa haiKwahiyo nchi kama Australia wanaosafirisha Kondoo huko ni wajinga ila wewe ndio una akili kuwazidi? Kama hao wahitaji wametaka Ng'ombe hai,wewe tatizo lako ni nini?
2050 hakuna mtalii atakuja tanzania
Tunajilinganisha bado na Australia?Kama Australia waliwapelekea nyama ya kangaroo kwa jina la kondoo
Unafikiri Sisi tutawapelekea nini?
Ila wapo wanaopeleka nyama kutoka Dar na Dodoma pia
Ila nchi nyingi wanapenda wanyama hai wachinje wenyewe nalijua sana hili
Lakini ni mawazo pia ila mwisho wa siku watamalizana wao
Kwa hiyo haya machinjio mliyojenga yatafanya kazi gani?Nchi kama Somali wanasafirisha Mbuzi na Kondoo huko Oman,Australia wanasafirisha Kondoo huko Oman,
Naona badala ya kuchangamkia fursa mmekimbili sijui Twiga mara Tembo!
Bila kubadili hizi fixed mind mentality mtu atajikuta yupo pale pale tu miaka na miaka.
Acha utani
Kwani soko litakua ni Oman tu? Sasa hivi hizo nyama zinauzwa nchi gani na nchi gani?Kwa hiyo haya machinjio mliyojenga yatafanya kazi gani?
Nilidhani mnauza mali zilizichakatwa kumbe sasa hata viwanda havitakiwi,
Malighafi ziwe zinaenda bila kuongezwa thamani?
Kazi ipo bado.
Ni kweli ndiyo maana Australia wanasafirisha wanyama hai baada ya Kulifahamu soko vizuri, na hii husaidia kuikamata fursa vizuri zaidi. Tunaweza kukazia mjadala huu kwa maneno matatu : Mteja Ni Mfalme.
Nani kakwambia kua Australia hauzi Kondoo hai huko Uarabuni? Hivi hua mnajiandikia tu ili mradi na wewe usiachwe nyuma?Kaangalie kwa mm Australia aliuza hao kondoo hai na kwa nn sasa hivi hauzi wakiwa hai
Pili, jiulize tumekosa soko la nyama hadi tuuze ng'ombe wakiwa hai?
Tunajilinganisha bado na Australia?
Tukishindwa kuwa na viwanda vya nyama ili tuuze nje tutakua na viwanda vya aina gani tena? Maana kwenye Teknolojia tulishafeli na hatuwezi.
Kama uwezo wetu upo kwenye kuzalisha ng'ombe , basi duniani tusifike kwa kuwa na viwanda vya nyama vya kisasa kwa kuwa hatuwezi kuwa na viwanda vya magari au simu au computer
Mama angesema mifugo angeeleweka kwa wepesi kuliko alivyosema wanyama mtu akitaja wanyama wabongo wanachojua ni Simba, chui, Nyati, Serikali ilishapiga Marufuku kusafirisha mbuzi na kondoo nje ya nchi, kuna viwanda vya nyama vipo mkuranga, Mama anataka awaambie Wa Omani waje kujenga viwanda vya nyama kuliko kuwapeleka mifugo uko kwa WaarabuKaka acha akili mgando Kama alikuwa nataka kuiba angetangaza ili iweje
Kuna kiwanda cha nyama kipo mkuranga kizuri tu kimetoa ajira kwa wananchi sasa anataka kupeleka wanyama nje wakati ilishapigwa marufuku mbuzi na kondoo kuuzwa kenya tu, na kama ni fursa basi tuwaambie wakenya waje kununua kwetu kama zamaniKwani soko litakua ni Oman tu? Sasa hivi hizo nyama zinauzwa nchi gani na nchi gani?
Badala ya mzungu kuhangaika kuja Tanzania kwanini asiishie hapo Oman tu ambapo ni rahisi kufikika.Kuna wajinga humu wanaona mbuzi na twiga ni sawa, hawaoni kama hao waarabu watachangamkia kile ambacho hawakipati toka mataifa mengine.
Hao mbuzi na kondoo watawahitaji kwa kiasi kidogo kwasababu wanawapata toka nchi nyingine, lakini kwa twiga wetu, na wanyama wengine wa mwituni ndio watamalizwa, na utalii utahamia huko Arabuni.
Hizi fursa zinazofunguliwa na huyu mama ni janga kwa taifa letu na kwa vizazi vijavyo, madini wameyatoa sasa wanatoa na wanyama wetu. Oman wakianza kutangaza vivutio vyao vya utalii na Twiga wetu watakuwepo, sasa hao watalii watatoka wapi kuja kwetu?
Hao Sasa kunakua hakuna maana yoyoteNaunga mkono hoja yako Mkuu
Ila biashara ni makubaliano kwenye soko la nyama tupeleke nyama na wanaotaka wanyama hai wachinje wenyewe sawa pia
Nimekuambia kaangalie kwa nn walizuiaNani kakwambia kua Australia hauzi Kondoo hai huko Uarabuni? Hivi hua mnajiandikia tu ili mradi na wewe usiachwe nyuma?
Nchi Ina watu wengi wajinga hii, Kuna mmoja alikuwa anafurahia Kenya kuruhusiwa kutuletea maziwa huku ya brookside akasema ataanza kunywa hayo ikiwa huku kwetu tuna kila aina ya ngombe. Ila hapohapo wakenya hawaruhusu maziwa ya Asas kule kwaoYaani mnapeleka ajira nje wakati huku kunachangamoto ya ajira.wao waje wawekeze hapa nchini ili tutengeneze ajira hapahapa.mkipeleka wanyama hai tutakuwa tumetengeneza mazingira ya kutorosha maliasili zetu na tutarudishiwa tena kama finished goods kwa bei ya juu.Ifike mahali tubadilishe katiba kuwapa mwaka mmoja wanaopata urais kwa dharura.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kina nani walizuwia? Mpaka leo Australia wanasafirisha Kondoo huko Uarabuni.Nimekuambia kaangalie kwa nn walizuia
Alafu kwa nn tunajilinganisha na Australia? Wao Wana viwanda vya kila aina kuendesha uchumi wao mkubwa, huku sisi uwezo huo hatuna basi kwenye hivi vidogo tunavyomudu kwa nn tusiwekeze kwenye viwanda kwa kuanzisha viwanda vingi vya nyama?
Hapa tusimame kidete tuseme HAPANA!! Tunataka kuhalalisha wizi wa mchana! Ukiruhusu kusafirisha wanyama hai tutabaki na mbuga zisizo na wanyama muda si mrefu!! Hii itakuwa kinyume na kanuni ya utunzaji wa mazingira!! Tutaua utengamano na ulinganifu wa viumbe hai kwenye mbuga zetu (killing the equilibrium balance of the ecosystem in our game reserves), na huo ndio utakuwa mwisho wa utalii!! Huyu mama lazima aambiwe kuwa sasa anataka KWENDA MBALI SANA na HAIVUMILIKI TENA!!Salaam Wakuu,
Rais Samia katika Kongamano la Wafanyabiashara wa Oman na Tanzania, amesema kuna umuhimu Mkubwa wa kuangalia Usafiri wa Majini akimanisha Meli yenye Uwezo wa kusafirisha Wanyama wakiwa hai kutoka Tanzania kwenda Oman.
Watu hapa wasifikilie Wanyama Pori tu, Bali ni Habari njema kwa Wafugaji wa Tanzania kwani sasa Wataanza Kusafirisha Ng'ombe, Sungura, Kitimoto, Mbuzi, Swala, Twiga nk hasa kwa wawindaji wenye Vitaru.
Pia kazungumzia kuhusu meli za Kuvua samaki Bahari Kuu.
Amewataka Oman waje kuwekeza Tanzania ardhi ipo ya kutosha.
Watanzania Kaeni Mkao wa kula.
............................................................................
Rais Samia akiwa kwenye kongamano Kiuchumi nchini Oman, amesema kuwepo kwa vyombo vya usafirishaji vya majini kusafirisha wanyama walio hai na bidhaa mbalimbali kwenda Oman kutaboresha biashara kati ya pande hizo mbili
Pia amegusia japokuwa tuna makubwa ya kuvua, kwa sasa hamna uvuvi wenye tija kwa taifa, amesema “kuna nchi zinakuja Tanzania kuvua na hatuwezi kuwafukuza kwa sababu hatuna vifaa, hivyo wanavua na kuondoka, hili ni eneo lingine ambalo tunaweza kushirikiana kwa pamoja”
Amesema kuwa kongamano la mwaka huu limekusudia kuanngazia namna Tanzania itashirikiana na Oman katika sekta za utalii, kilimo, Uzalishaji (viwanda) mifugo na uvuvi na usafirishaji wa majini.