Omba usishikwe na tumbo la kuharisha ukiwa katikati mjini na hakuna vyoo karibu

Huu uzi nasubscribe kabisaaa ni hatareee....nacheka mwenyewe mpaka naonekana kichaa
 
Mi ilitokea nilipokwenda kwao na mchumba wangu siku hiyo kujitambulisha!
Ile tumemaliza kula tu hali ikagoma nikakimbilia chooni naharisha maji tu.!
Ile namaliza kurudi sebuleni nikabanwa tena safari hii nilijinyea nikiwa mlangoni mwa choo kumsubiri mtu atoke niingie.!
Ilikuwa aibu kubwa ya kufunga mwaka usiniulize kilichotokea baada ya hapo..!
Nnachokumbuka uchumba uliishia hapo kwani sikuwahi kurudi tena wala kumtafuta huyo binti na namba ya simu nilibadiri nikahama na mtaa maana watu wangeinyaka kuwa nilijinyea ukweni ingevuma kuliko ya Bashite na vyeti.
 

Kwa kweli umenivunja mbavu [emoji23][emoji23][emoji23]
Umenikumbusha movie ya zamani ya ki nigeria Usuofia in London!
 
hahahhhh wee hii uongo
 
Show ilinikuta natoka lugalo niko ndani ya dala dala,,hapo nimetoka kumix mivyakula kibao,,sah nikashuka pale ubungo nilitembea kwa speed ya light huku viushuz vidogo vidogo vikisindikiza safari ,,,dah hii sitasahau
 
Aaaa ah mmenikumbusha mbali me nilibanwa na tumbo la kuhara kwenye daradara na palikuwa na foleni naelekea home mana nilibana kiasi kwamba nikinyenyuka kwenye seat mzigo unafuata
Aisee niliona bar moja nilishuka Kimya Kimya lakini tayari nilisha inyea boxer. Nilifika namalizia mzigo uliobaki na kuvaa suluari kavu kavu, boxer nikatia kwenye rambo then nikapeleka dump.
Hii kitu Balaaaa
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Mwaka 2003 Nlikua ndo nimechaguliwa kujiunga kidato cha 5 Mkwawa School.Usiku kabla ya safari maza akaniandalia nyama mkaango na ndizi zilizopakwa ngano.Nilikula kwa uroho sana mana ndo naiaga Life ya home.Nikapanda hood bus Moshi kuelekea Iringa.Tumbo lilikata kuanzia Mwanga hadi nafika Liverpool nilikoma.Afu pembeni nilikaa na Dada mmoja nae akadai anaenda Mkwawa.Jicho lilinitoka mbaya mbovu aseee.
 
Nimecheka kwa sautiiiiii
 
Mkuu wewe hukuharisha ila ulijinyea kabisa!! Dah kazi ipo.
 
Hahaha! Pole sana!!!
Hiyo kitu ikukute chuo alafu ile unakimbilia chooni unakuta majangili washaharibu vyoo vyootee!!! Kudadeki... Huoni ajabu kuachia mzigo juu ya mzigo wa mwingine. I salute uharo aisee!!
Ahsante sana, japo ni miaka mingi iliyopita lakini bado tukio halifutiki kichwani mwangu....
 
Nilikuwa nasafari yakutoka Dodoma kwenda Dar asubuh nimegonga kiporo cha wali maharage swafi njian kuelekea stand tumbo likakoroga nikajikaza mpaka stand ya shabiby choon kuzama nikashusha mzigo mzito nikatoka kukaa dakika tano kitu tena dooh nikazama tena hapo naomba basi lisiondoke nikarud tena trip ya tatu sink likajaa nafkir lilikuwa limeziba kuingia kwenye basi siti za nyuma nyuma viti vya watu watatu me Niko katikati nitumbo kukoroma Kama radi nkaseme kufedheheka ndo huku nikajikaza likiyumba na Mimi nmeyumba kaza kalio mpaka jasho sizungumzi nikafanikiwa kufika Moro kushuka brake yakwanza toi nilishusha mzigo wa kutosha hapo cjala kitu mpaka nafika Dar chamoto nilikiona na sikutumia dawa yoyote nilipona tuu na nikafunga choo Kama siku nne
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…