"Ombeni Mtapewa", "Tafuteni Mtapata", "Bisheni Hodi Mtafunguliwa" Je, Wajua Kuna "Kauli" na "Kauli Umba" Ambazo Huumba? Shuhudia

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,

Leo nimepata tena fursa kuendelea na zile makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa, ila makala ya leo ni abstract topic, kuielewa mtu ni lazima uwe na levels fulani za uelewa!

leo nikizungumzia kitu kinachoirwa "kauli umba". Kuna hii misemo "Ombeni Mtapewa", "Tafuteni Mtapata", "Bisheni Hodi Mtafunguliwa" Je Wajua Kuna "Kauli" na "Kauli Umba" Ambazo Huumba?. Shuhudia jinsi kauli umba zinavyoumba!

Lengo la mada hii kuhusu kauli umba, ni kuwalenga viongozi wetu, wasijiinue kupitiliza, wajishushe na wawe wanasikiliza hata kauli za watu wadogo, insignificant na wa kawaida kama akina sisi, baadhi ya watu wadogo hawa na insignificant, baadhi yao, japo they are nobodies lakini baadhi yao wana "kauli umba" baadhi ya kauli zao ni very powerful, wakisema jambo linatokea, usikute ni kauli za watu wadogo hawa na insignificant hawa ndio zimekufikisha hapo ulipo kiuongozi bila ya wewe kujijua! Ukiweza kujitambua, kusikiliza na kuzingatia kauli umba za wadogo hawa, sio tuu zitawasaidia sana, bali pia zinaweza kuwaepusha na mengi na kulisaidia sana taifa letu kwa kuliumbia mema, kwa kauli umba zao, kwasababu kauli za baadhi yao zina posses the real powers za uumbaji na wakilisema jambo, wanakuwa wameliumba na jombo hilo kuumbika na kutokea kweli kutokana na kuumbwa na kauli umba hizo ambazo huumba!

Siku za Jumapili nitakuwa nikipandisha threads za mambo ya powers za imani, kauli na wishes ili kuwajengea watu uwezo wa kutumia nguvu iliyo ndani yao kufanya mambo huku tukiikamilisha Easy Sunday, at easy kwa kuainisha baadhi ya kauli umba ambazo ni very powerful zenye powers za uumbaji ndani yake, zilizotolewa humu jf, kuzungumzia jambo fulani, na baada ya muda, jambo hilo lililozungumziwa, likaja kutokea kweli kwa jinsi ile ile iliyozungumzwa. Baada ya jambo hili kutokea, kwa vile wengi hawakuwahi kujua kuwa kabla jambo hilo halijatokea, kuna kauli umba ilitolewa kabla, powers za kauli umba hiyo, ndizo zikaja kuliumba hilo jambo, hivyo hilo jambo linakuwa ni limeumbwa kwa kauli umba za watu hao ambao ni nobodies kabisa na very insignificant ordinary people!.

Nawashauri viongozi wetu, wawe wanazisikiliza kauli za watu hawa wenye kauli umba, zitawasaidia na kulisaidia taifa!.

Mada hii ni abstract ya vitu vya kufikirika, vikasemwa na vikaja kutokea kweli. Lengo la kuileta mada hii ni tusidharau watu, wala tusidharau kauli za baadhi ya watu, zina nguvu ya kuumba!.

Kwa sisi Wakristu, kuna mahali Bwana wetu Yesu Kristo, ametufundisha "Ombeni Mtapewa", Tafuteni Nitapata", "Bisheni Hodi Mtafunguliwa"

Hivyo ukiwa na kitu unakihitaji unapaswa kukitafuta ili ukipate, ukiwa na mahitaji unaomba ili upewe na ukienda mahali ukakuta milango imefungwa, bisha hodi utafunguliwa. Na ukibisha hodi usipofunguliwa au mlango mmoja ukifungwa, mlango mwingine unafunguka. Ili mtu ufanikiwe ni lazima utafute.

Bwana Yesu anaendelea kufundisha kuwa jambo lolote utakalo omba kwa Baba yangu, kwa jina langu, utapewa, lakini kwa sababu jf ni ukumbi wa dini zote, naomba kuwajulisha kuwa Mungu sio wa dini yoyote, Mungu hana dini, wala hakuna Mungu wa Wakristo, Mungu wa Waislamu, miungu ya Wahindu, Wapagani na wengine wote, Mungu ni mmoja tuu, omnipotent, omnipresent, na omniscience.

Kuna watu waliaminishwa na mafundisho ya dini zao kuwa Mungu yuko juu mbinguni, ameketi kwenye kiti chake cha enzi huko mawinguni, na kwamba mbinguni au peponi ni juu mawinguni. Hivyo wakisali na kuomba, wanatazama juu!. It's not true, Mungu ni omnipresent yupo pote!

Mungu yuko ndani yetu ndani ya kila binadamu haijalishi ni wa dini gani, baada tuu ya kuumbwa kwa udongo Mungu alitupulizia ile pumzi ya uhai, pumzi ile, life force, ndio yenye Umungu ndani yake.

Hivyo sii kweli mbinguni ni kule juu, mbinguni na duniani ni hapa hapa, ila hii dunia tuliyopo sasa ni ulimwengu wa mwili, na kuna ulimwengu wa Roho, huko ndiko mbinguni, peponi na motoni.

Hivyo ili kuomba chochote kwa Mungu, unaweza kutazama popote sio lazima juu, na unaweza kuomba chochote kwa Mungu bila kulitaja jina lolote na ukapewa!

Hii maana yake, Mungu ni msikivu sana, ukiwaza tuu kuwa unataka jambo fulani, Mungu tayari anakuwa amesikia, hivyo kuomba kwa kauli hata kwa kuandika tuu popote, kwenye simu, kwenye SMS, kwenye mitandao ya kijamii, etc, huko ni kuliongezea tuu nguvu hilo jambo lako.

Ushuhuda wa Pasco Mayalla Kuumbiwa Ajali ya Pikipiki Kwa Kauli Tuu ya Mtu!

Je, wajua kuwa baadhi ya watu kauli zao zina nguvu ya kuumba?Niulize mimi! Mimi kazi yangu ni mwandishi wa habari, kazi ya uandishi inakutaka ufike kwenye tukio haraka, na kuwahisha habari newsroom kwa haraka. Hivyo usafiri most convenient kwa sisi waandishi wa habari, ni usafiri wa pikipiki. Hivyo kati ya miaka yangu 32 ya uandishi wa habari, miaka 18 usafiri wangu ulikuwa ni piki piki!

Mwezi June mwaka 2008, kuna mtu alipandisha uzi humu JF, kuhusu uendeshaji wangu wa piki piki, kwenye uzi huo, kulitolewa kauli mbaya kuhusu uendeshaji wangu wa pikipiki na kuhusishwa na ajali!, huwezi amini mwezi uliofuata, mwezi Julai, nilikula mziga wa kwanza, na mwezi August nikala mziga wa pili wa haja!. Lile bandiko la mwanzo kuhusu uendeshaji wangu wa pikipiki, likafutwa ndipo bandiko la ajali yangu ya pikipiki likapandishwa
Pascal Mayalla apata ajali..... hivyo huu ni uthibitisho kuwa kuna baadhi ya watu, kauli zao huumba!. Nimeanza kuendesha pikipiki 1993, hivyo hiyo 2008 ni miaka 15!, huo ndio ulikuwa uendeshaji wangu na sikuwahi kipata ajali!. Ila baada ya watu wenye kauli za kuumba, kuandika humu JF kuwa naendesha mbio pikipiki nitapata ajali, kauli hizo ziliniumbia hiyo ajali na kweli nikapata ajali!

Hivyo amini usiamini kauli huumba? Angalia baadhi ya kauli hizi ziliumba nini?. Laiti wahusika waliotajwa kwenye kauli hizi, wangezingatia haya yaliyosemwa, yaani kauli umba hizi zingesikizwa, labda by now, matokeo yangekuwa ni mengine.

Sisi binadamu tuna mtindo wa kuheshimu hoja zinazotolewa na watu fulani fulani tuu, watu muhimu kwenye jamii au watu wakubwa!, viongozi, na kudharau watu wadogo ambao ni nobody!. Kwa vile kauli hizi zilitolewa na mtu ambaye ni nobody, no one paid any attention kwa kauli hizi, mpaka pale kauli hizi zilipoumba ndipo baadhi tuu ya watu angalau wakafahamu, lakini very unfortunately, walengwa wa kauli hizo, never paid any attention kwa kauli za makapuku!. Laiti kama wangezingatia hoja za kauli hizo, you never know, labda baadhi yao, tungekuwa nao hadi leo, yaani wangeliwepo!

Naomba nianze na tukio la hivi karibuni.
Mfano Spika JYN, baada ya kuusoma uzi huu Voices from within: Nimesikia sauti, Dr. Tulia Ackson ndiye Spika ajaye! Sauti hiyo imenieleza Ndugai, japo atatamani aendelee lakini... Iwapo JYP angesoma bandiko hilo na kuamua kutogombea Uspika Kwa term nyingine, angeondoka Uspika kwa kuagwa kwa heshima na sio kwa fedheha kama alivyoondoka!

Hata sasa Spika Tulia, anaweza asijue kuwa usikute yeye kupata Uspika huu alionao sasa ulitokana na kauli ya kwenye bandiko hilo!
Kauli umba ni hii
mara ghafla nikasikia sauti from within, ikiniambia kuwa "Spika ajaye ni Mhe. Dr. Tulia Akson. Sauti hiyo ikaniambia japo Mhe. Ndungai, atakuwa anatamani sana kuendelea kuwa Spika, lakini Ndugai hatakuwa kwa sababu fulani,
Paskali
Mwaka 2014, humu JF, kulipandishwa bandiko hili
Elections 2015 - Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli, by that time, JPM wala hakujua kuwa atakuja kugombea urais.
Kauli umba ya kumuumbia JPM urais wa JMT ni hii
Muda wa kuchukua fomu za urais CCM ulipowadia JPM alijitokeza kuchukua fomu kwa ku beep tuu, simu ikaitika!

Hivyo JPM alikuja kuupata urais wa JMT akijijua ni yeye ndiye aliye u beep urais akaupata, bila kujua kuna watu waliishamtolea kauli za kumuumbia urais wa JMT!

Hata hoja ya udikiteta, baadhi yetu bila kujijua kumuita mtu fulani ni Dikiteta, kumbe ndio tumemuumbia huo udikiteta!
Kauli huumba! Je, ni kweli Magufuli ni dikiteta? Kama ni kweli, ni kosa la nani kati yake na aliyetoa kauli hii?

Amini usiamini, baada ya kupindua kauli, kiukweli kabisa JPM alinza kubadilika, Magufuli is Getting Better and Better, He is Changing for The Better!. Hongera Sana!

Hivyo nikarejea humu JF na kuwaeleza watu humu Trends, Visions: Watanzania msitatizwe na kauli zake kuhusu Katiba, baada ya Nyerere, ni Magufuli ndiye ataacha legacy kubwa ikiwemo Katiba Mpya!.
Baadae Rais Magufuli, so far, is the best president this country has ever had. Msikivu, ana upendo na huruma. Atabarikiwa sana. Tanzania itabarikiwa!

And by the time anatwaliwa from huu ulimwengu wa Mwili kwenda ulimwengu wa Roho, he was almost a saint! Voices From Within: Je, wajua yuko Peponi, Mbinguni, Kwa Baba yake? Why kumshutumu, kumsakama na kumsimanga? Aachwe apumzike kwa amani

The same applies to urais wa Samia, hakuna mtu yoyote alijua kuwa kuna siku rais wa JMT anaweza kufa akiwa madarakani!, hivyo siku zote Makamo wa rais alikuwa anateuliwa tuu bila kumhesabia anaweza kuja kuwa rais wa JMT kwasababu hakuna aliyewahi kufikiri rais wetu anaweza kufa!.

Hivyo naamini hata wakati Samia ni Makamo wa JPM, hakuwahi kuwaza kuwa kuna siku JPM anaweza kuitwa kwa Baba yake na yeye kuwa rais wa JMT!, hivyo ilivyotokea JPM akaitwa Baba yake na Samia kawa rais, watu wote wanajua imetokea tuu, ni mipango ya Mungu, lakini hakuna watu wanaojua kumbe kuna watu, walitoa kauli zenye nguvu ya kuumba, waliomuomba Mungu, wakamuumbia urais wa JMT ili Samia awe rais na kweli Mungu akasikia hivyo kauli hizo zikamuumbia Samia urais, hivyo usikute hata Samia mwenyewe anajihesabu amekuwa rais wa JMT kwa kudra tuu za Mwenyeenzi Mungu, kumbe hajui sio kudra tuu, kuna watu waliomba, na wakapewa!.

Kwanza anza kuangalia ni lini watu walianza kumspot Mama Samia, mimi nilimspot 2010 New Cabinet: Baadhi ya Majina ni Haya Hapa!.
Bandiko hili ni la 2010, angalia hiyo 2010 tulisema nini kumhusu Samia, na nini kilikuja kutokea... mkiambiwa baadhi ya kauli zinaumba, mjue ni kweli kauli huumba!.

Kisha 2015 Siku ya Wanawake Duniani: Je, tuna Wanawake wenye sifa za Presidential Material?
Kauli Umba ya kuunda VP mwananke kwa Tanzania
Tanzania ilipata VP, mwanamke kwa mara ya kwanza, baada ya uchaguzi wa 2015, kuna wengi wanadhani ilijitokea tuu, Tanzania kuwa na VP mwanamke!, hawajui kuwa huo u VP wa mwanamke, kuna watu wenye kauli zenye powers za kuumba, walitoa kauli za kutaka tupate VP mwanamke, toka Machi 8, 2015!.

Then Siku ya Wanawake Duniani: VP Samia Suluhu: "Womanly, Genuine, Humble, Simple na Down To Earth!”
Hii ni kauli umba ya kumuumbia mtu urais wa JMT.

na hili "Watu waachwe Huru kuujadili Muungano"- VP, Samia Suluhu Hassan. Huyu mama anaongea vizuri kwa Unyenyekevu mpaka raha. Huchoki kumsikiliza
Angalia kwa makini hii kauli umba hapa iliumba nini?
Hapa kuna mtu ameumbiwa urais wa JMT kwa kauli tuu!.

Naamini kama JPM angesoma hapa, halafu akaamua tangu ile ile ,2020 angempisha Samia, you never know by now labda...

Hitimisho
Kulikamilisha bandiko na kukuacha na burudani ya easy Sunday, naomba nikuache na kibao hiki cha DDC Mlimani, wana Sikinde ngoma ya ukae, kiitwacho "Utu ni Tabia Njema na Wala Sio Pesa"'
Mtunzi ni Shabani Dede, Mwimbaji ni Cosmas Thobias Chidumule, baadhi ya maneno ya wimbo huo ni
"Nimekumbuka yangu Dunia"
"Maneno Baba alio niambia"
"Fukara Hapendezi mbele za watu hata kidogo"
" Lolote asemalo wao watacheka"
"Na kumuona bure tena hayawani"
Sasa nini maana watadharau na kupuuza"
Chorus
"Utu ni Tabia Njema na wala sio pesa" X 2
Haja ya Mja hunena muungwana ni kitendo
"Dharau Haifai na tena mbaya sana"
"Mtu muone kama mtu sio mpaka awe na kitu"

When you are nobody, hata ukisema kitu, hakitiliwi maanani, natoa wito kwa viongozi wetu, lisemwalo lipo, kama halipo linakuja, mkishauriwa kitu hata na mtu mdogo, ambaye ni nobody,
hakuna ubaya, sio lazima kufuata kila ushauri, ila ni muhimu kuuzingatia ushauri wowote wenye logic ndani yake, unasaidia, unalisaidia taifa na besides everything, unaokoa na unaponya!.

Wasalaam

Paskali.
 
Labda ni kweli angempisha 2020 angekuwepo bado lakini who knows? Isitoshe yote haya ya nini wote tu safari moja Magufuli ameenda, Mzee Mkapa ameenda, Mwalimu Nyerere ameenda hata Mrema nimesikia kwamba pia ameenda, hivyo tu safari moja hata wanajiona leo ni Miungu watu na kutoa lugha za kebehi sijui hamia Burundi mara kazikwe naye Chato ipo siku yao pia, Binadamu tu wasahalifu sana, kama alivyosema WM Majaliwa siku moja kwamba hakuna ajuaye nani atakuwa raisi unaweza kujiandaa na kufanya kila kitu lkn bado ukaukosa mfano Lowasa au hata Raila, …
 
Hivi wewe mzee hunaga kitu kingine unawaza kufanya kutokana na fani yako kwani lazima uwe mwanasiasa, kama watakuona unafaa watakuchukua acha kulambalamba watu miguu kisa vyeo vya kidunia, infact kwa umri wako huo kalee wajukuu na kumrudia muumba wako!

Nyie wazee mnabidi muwe mifano kwa kizazi cha sasa na kijacho ila kutwa kucha kazi kisifia na kuabudu, ona sasa umevuka mipaka unajipa cheo cha utabiri😁😁😁😁 ulafi unakudhalilisha wewe mzee huna cha voice from within wala nn ww ni tapeli kama matapeli wengine wanaotaka kufaidika na kupata utajiri kwa mgongo wa siasa, wewe mzee jiheshimu bwana embu uwe unaridhika, umesoma sheria ili iweje nyie ndo mnasoma ili muwe na title kubwa na hizo elimu hamzitumii, hiyo pesa ungesomesha watoto wenye uhitaji ungeonekana wa maana na ungekuwa mfano wa kuigwa, acha tamaa ww mzee ujiheshimu!
 
Asomaye na afahamu. CC. Singida Big Star.
 
Konyagi na k vant hazijawahi kumuacha mtu salama
Licha ya yote ya kutukumbushia hizo konyagi nakukumbusha ahadi Yako ya kuniua kwa kuwaibia TV chogo black and white 1988. You must finish me off bcoz letting me continue living like this with this tozo stuff everywhere in our country is not fair.

This is the last time am reminding you, next time I will ambush you at a knife point and blades will be held against your throat till you fulfil your promise.

 
Aliyesoma akamaliza anipe sammary 😆😆
 
Kipindi upo vizuri ulishawahi kinijibu kwa shit humu jukwaani kuwa hauhitaji uteuzi ,hivi ni kweli bado au umebadili msimamo?
 
Mwa

Mwaka mmoja kabla ya Uchaguzi nilimuuliza JPM kama atagombea urais. Hakujibu, yaani, swali lilikuwa kama embarrassment, kwa vile CCM hawatakiwi kusema 'afortime. Ilikuwa nimeuliza swali mbele ya watu wengi.
 
Mkuu, sisi waafrika tunapenda sana ushirikina, mambo yasiyoonekana yasiyo na uthibitisho, mythologies na vitu vya namna hiyo. Embu tuanze kuwa objective tujishughulishe na vitu vya ukweli vyenye kufanyika na kuthibitika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…