Ombi kwa Mohammed Said kuhusu Saigon Club

Kamanda Chiko Nilihudhuria Mazishi yake pale Kisutu...
 
Tatizo la Saigoni ukikaa ukianza kuzungumzia Siasa watu wote wanatimka...
 
Tatizo la Saigoni ukikaa ukianza kuzungumzia Siasa watu wote wanatimka...
Mlaleo,
Hilo sina hakika ila ninachojua si watu wa kupenda siasa kwa kiwango
cha majadiliano lakini sidhani kama inavunjwa baraza kwa ajili ya siasa.

Nilichokuwa na uhakika nacho ni mazungumzo ya mpira yanapendwa
mno hata kwenye Dar es Salaam Saigon Group mazungumzo mengi ni
ligi ya Uingereza na Simba na Yanga.

Kila watu wana mila yao.
 
Nimefurahi kusoma historia lakini pia mjadala wa kistaarabu mno usio na matusi na kejeli kama mijadala mingi humu jf. Asante kwa historia nzuri
 
Haya yanayopitika Saigon hivi sasa ni urithi kutoka kwa wazee wetu.[/QUOTE]

Mzee Mohamed Said, nafahamu wewe ni mwenyeji hapa Dar es Salaam. Lakini wakumbuka namna Saigon ilivyotumika kumzuia Marehemu Dr Lutta Nelson kugombea Uongozi Chama cha Soka Dar es Salaam DRFA miaka ile ya 90? Mwanachama mwenzenu Ukiwaona Mzuzuri alisema mtu asiyeijua Saigon na ambaye tongotongo hazijamtoka hawezi kuongoza DRFA. Kwa nini tusiseme mlikuwa mkileta aina fulani ya ubaguzi?
 
Inna li Llahi wa Inna Ilayhi Rajiun.

Hussein amefariki?

Kuhusu Chico nilipata habari, Allah amrehemu yeye na aturehem nasi pia.

Kuna siku Nyani Ngabu alikambia msalimie Zomba, ukamjibu Inna li Llahi wa Inna Ilayhi Rajiun. Unataka kusema Zomba alifariki? kama ni hivyo basi poleni na Mwenyezi Mungu amrehemu
 
dah...Garincha marehemu? masikini my old friend.

Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un..
 
Kuna siku Nyani Ngabu alikambia msalimie Zomba, ukamjibu Inna li Llahi wa Inna Ilayhi Rajiun. Unataka kusema Zomba alifariki? kama ni hivyo basi poleni na Mwenyezi Mungu amrehemu

Inna li Llahi wa Inna Ilayhi Rajiun, mwaka jana.
 
Dah... Hivi lengo kuu la Saigon kwa nyakati hizi ni nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…