Ombi la kurejeshwa kwa mada maalum ya waliotekwa ama waliopotea

Ombi la kurejeshwa kwa mada maalum ya waliotekwa ama waliopotea

Will due respect
Naomba uongozi wa JF utafakari tena uamuzi wa kuifuta mada husika niliyoiweka hivi karibuni
Ni mada inayohusika na uhai wa watu .. Kwenye dunia hii hakuna kitu cha thamani kama uhai kwakuwa hakuna vipuri vya uhai
Naomba with all due respect mada husika iweze kurudishwa ili JF ionekane ni sehemu ya kuunga mkono dhidi ya udhalimu wa utekaji na mauaji yanayoendelea nchini
Naamini kati ya wengi waliotekwa, kupotea ama kuuliwa wamo pia wanachama, wapenzi na wafuasi wa jukwaa letu pendwa la JF

JF ina watu wa kila aina na wenye habari za kila aina kwenye kila kitu .. Na ndio maana kwasasa inachukuliwa kama chanzo cha uhakika cha taarifa nyingi (credible source)
Naamini kwa dhati ya moyo mada husika ingeachwa hewani zingekuwa zimeshapatikana taarifa nyingi na pengine nyeti juu ya hali tuliyo nayo kwasasa kuliko kila wakati kuwa na mada nyingine mpya
Waliotekwa, waliopotea, waliopotezwa na waliouawa ni sehemu ya JF kwakuwa JF ni ya wote.. Naomba sana tuitoe kifungoni mada husika kuonesha support yetu kwa hao wahanga wote wa natukio tajwa
Kwa heshima na tadhima
Kwa uhai na ustawi wa JF
Naomba ikuwasilisha

Ndimi mjoli wenu
Mshana Jr
Kilingeni Msata
September 12 2024
Natamani ungeliondoa neno KILINGENI!

Ila pole sana mkuu. Najua mada zako huwa si za kitoto, na huna kawaida kutukana. Halafu inatumia verified id! Kwa nini wamefanya hivyo? Wanahofia usalama wao? JF ina maslahi na mada uliyoiandika? Baadhi ya "wahariri" wa JF nao wanahitaji kutazamwa.

Ukiweza, andika tena. Wakiifuta , unaiandika tena na tena mpaka wachoke kuifuta!
 

Mshana huna baya...usitekwe
WAEFESO 4:31-32

³¹ Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matukano yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya;

³² tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.

HILO NDILO NENO LA MUNGU
 

Natamani ungeliondoa neno KILINGENI!

Ila pole sana mkuu. Najua mada zako huwa si za kitoto, na huna kawaida kutukana. Halafu inatumia verified id! Kwa nini wamefanya hivyo? Wanahofia usalama wao? JF ina maslahi na mada uliyoiandika? Baadhi ya "wahariri" wa JF nao wanahitaji kutazamwa.

Ukiweza, andika tena. Wakiifuta , unaiandika tena na tena mpaka wachoke kuifuta!

Natamani ungeliondoa neno KILINGENI!

Ila pole sana mkuu. Najua mada zako huwa si za kitoto, na huna kawaida kutukana. Halafu inatumia verified id! Kwa nini wamefanya hivyo? Wanahofia usalama wao? JF ina maslahi na mada uliyoiandika? Baadhi ya "wahariri" wa JF nao wanahitaji kutazamwa.

Ukiweza, andika tena. Wakiifuta , unaiandika tena na tena mpaka wachoke kuifuta!
Asante sana mkuu wangu.. Wakati naandika hii mada nilikuwa pale Msata kilipokuwa kilinge changu enzi zile za kiza
 
Will due respect
Naomba uongozi wa JF utafakari tena uamuzi wa kuifuta mada husika niliyoiweka hivi karibuni
Ni mada inayohusika na uhai wa watu .. Kwenye dunia hii hakuna kitu cha thamani kama uhai kwakuwa hakuna vipuri vya uhai
Naomba with all due respect mada husika iweze kurudishwa ili JF ionekane ni sehemu ya kuunga mkono dhidi ya udhalimu wa utekaji na mauaji yanayoendelea nchini
Naamini kati ya wengi waliotekwa, kupotea ama kuuliwa wamo pia wanachama, wapenzi na wafuasi wa jukwaa letu pendwa la JF

JF ina watu wa kila aina na wenye habari za kila aina kwenye kila kitu .. Na ndio maana kwasasa inachukuliwa kama chanzo cha uhakika cha taarifa nyingi (credible source)
Naamini kwa dhati ya moyo mada husika ingeachwa hewani zingekuwa zimeshapatikana taarifa nyingi na pengine nyeti juu ya hali tuliyo nayo kwasasa kuliko kila wakati kuwa na mada nyingine mpya
Waliotekwa, waliopotea, waliopotezwa na waliouawa ni sehemu ya JF kwakuwa JF ni ya wote.. Naomba sana tuitoe kifungoni mada husika kuonesha support yetu kwa hao wahanga wote wa natukio tajwa
Kwa heshima na tadhima
Kwa uhai na ustawi wa JF
Naomba ikuwasilisha

Ndimi mjoli wenu
Mshana Jr
Kilingeni Msata
September 12 2024
Nlitaka kunukuu majina ya watu zaidi ya mia mbili waliopotea au kuuwawa kama ilivyoandikwa kwenye kitabu cha Sheikh Ponda ila naota nitapoteza muda tuu hapa.
 
CHADEMA KUWAPA USHIRIKIANO POLISI NI USALITI NA MZAHA KWA ROHO ZA WALIOTEKWA, KUPOTEA NA KUUAWA.

1.Nimetaarifiwa kuwa Jana Jumanne 10 September 2024 jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni kupitia RCO Kinondoni waliwapigia simu mawakili wa CHADEMA kwamba wanamuhitaji Katibu Mkuu John Mnyika kwa mahojiano.

2.Kama John Mnyika na CHADEMA watatoa Ushirikiano kwa Jeshi la Polisi Tanzania kufuatia kitu kinaitwa kamati ya uchunguzi watakuwa kuwa wamefanya mzaha mkubwa juu ya sisi wanachama wao tunotekwa, kuuawa na kupotea kwa kukubali kuwapa ushirikiano watuhumiwa namba moja wa matukio hayo.

3.Jeshi la Polisi halina uhalali wa Kimaadili Kufuatia kupotea kwa watu zaidi ya 100 na sita wakiwa ni wanachama wa CHADEMA huku mmoja akiokotwa akiwa ameuawa maeneo ya Ununio

4.Viongozi wa CHADEMA wakae vikaoni watoke na msimamo mmoja wa chama kuhusu wapi watapeleka ushahidi wao na maelezo wanayo yajua kuhusu watekaji na wauaji

•Taarifa ambazo CHADEMA wanazo na wana uhakika nazo isipokuwa hawana mamlaka inayoaminika na yenye nia ya dhati ya kushughukikia madai yao.

5.Jeshi la Polisi Tanzania halina mpango wa kuchukua hatua wala kukomesha utekaji na mauaji ya wananchi au makada wa CHADEMA bali wanalenga kutaka kujua CHADEMA wanajua nini kuhusu tuhuma zao ili watumie nafasi hiyo kuficha ukweli na kuharibu ushahidi.

6.Jeshi la Polisi Tanzania lilimsikia Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe 22 August 2024 kufuatia tuhuma kwa Jeshi la Polisi, akimtuhumu ZCO Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam, ACP FAUSTINE MAFWELE kuhusika katika kuratibu na kusimamia vikundi vinavyoendesha utekaji ndani ya Jeshi la Polisi, wakiwa na makao yao nyuma ya Kituo cha polisi Chang'ombe maarufu kama Tembo 7.

7. Jeshi la Polisi pamoja na Kusikia tuhuma za Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe za 22 August 2024, Hawakuwahi kujitokeza hadharani kukanusha tuhuma hizo.

•Hawakuwahi kumuhitaji Freeman Mbowe kumuhoji na kutaka kujua ukweli wa tuhuma hizo.

•Hawakuwahi kumfungulia mashtaka Freeman Mbowe juu ya upotoshaji au uchochezi kama tulivyo wazoea.

•Hawakuwahi kuhabarisha umma kuwa tuhuma za Freeman Mbowe zilikuwa zinafanyiwa kazi

8.Jeshi la Polisi Tanzania walichofanya ni kwenda kuvunja maskani ya kikosi kazi kinachotuhumiwa na Freeman Mbowe, kuendesha shughuli za utekaji na mauaji nyuma ya kituo cha Polisi Chang'ombe maarufu kama "TEMBO 7" na sasa wamehamia sehemu mpya ya maeneo ya Mpingo House.

•Huku askari waliotajwa na Freeman Mbowe walifuta akaunti zao katika mitandao ya kijamii kama alivyofanya Afande Semageni Shabani mmoja wa watuhumiwa katika kikosi kazi cha Polisi Chang'ombe (Tembo 7)

9.Kama Jeshi la Polisi Tanzania wangekuwa wana nia ya dhati ya kushughulikiia tuhuma za Mwenyekiti wa CHADEMA huenda Kifo cha Kiongozi wake wa Sekretarieti ya CHADEMA Taifa Bwana Ali Muhammad Kibao kisingetokea.

10.Tarehe 07 September 2024 majira ya Saa 6: 00 mchana, Wakati Katibu Mkuu wa CHADEMA John Mnyika anafamya kikao na Waandishi wa Habari kulitaka Jeshi la Polisi lijitokeze kusema alipo Kiongozi wake Ali Muhammad Kibao

•Tayari Jeshi la Polisi lilikuwa limeshauchukua Mwili wa Ali Muhammad Kibao kutoka Ununio na kupeleka hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kinondoni ya Mwananyamala

•Siku hiyo tarehe 07 September 2024 Msemaji wa Jeshi la Polisi DCP David Misime akitoa taarifa yake kuhusu kufanyia kazi tuhuma za John Mnyika tayari Jeshi la Polisi ilikuwa limeshaokota Mwili wa Ali Muhammad Kibao kwa zaidi ya saa 8 zilizopita tangu saa 1:00 Asubuhi baada ya Wakulima wa mchicha wa Ununio kujulisha mamlaka kuhusu kukutwa kwa mwili wa binadamu eneo la jirani la vitalu vyao vya mchicha.

11.Wakati wote huo Jeshi la Polisi lilikuwa linajua Mwili huo uliookotwa eneo la Ununio ndiyo Mwili wa Kiongozi wa CHADEMA anayetafutwa

•Badala ya jeshi la Polisi Kuwajulisha CHADEMA wao waliwazunguka CHADEMA na kuwatafuta ndugu wa Marehemu Ali Muhammad Kibao na kuwataarifu wafike hospitali ya Mwananyamala siku hiyo hiyo ya Tarehe 07 September 2024 majira ya mchana

•Na hata ndugu walipoutambua mwili wa marehemu Ali Muhammad Kibao Jeshi la Polisi lilificha taarifa isiwafikie CHADEMA na kuwaomba Wanafamilia Msiba uwe siri na usiwe wa kisiasa kwa kuwaondoa CHADEMA wasiwe sehemu ya msiba.

Na hata CHADEMA na mawakili wao walipofika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kinondoni ya Mwananyamala sehemu ya kuhifadhia maiti polisi waliwazuia CHADEMA kuingia ndani ya chumba cha Autopsy

•Hii pia inathibitishwa na taarifa ya Jeshi la Polisi ya tarehe 07 September 2024 kupitia kwa Msemaji wake DCP David Misime ambapo alisema kuwa wapo tayari kushirikiana na familia tu huku wakikwepa kutaja CHADEMA katika taarifa yao pamoja na kujua marehemu ni Kiongozi wa CHADEMA

•Je, leo Jeshi la Polisi ndiyo limegundua linahitaji Ushirikiano na CHADEMA..? Huu kwa lugha rahisi tu, tunaweza kuita ni unafiki wa kiwango cha juu sana na hatutakiwi kuufumbia macho.

11.kuanza kutafutwa leo na Jeshi la Polisi ni unafiki mkubwa. Jeshi la Polisi liliwapuuza CHADEMA likaziba masikio na kuacha kufanyia kazi tuhuma za CHADEMA kwa askari wake wanaotajwa kuendesha Operesheni za kuteka na kuua watu. Badala yake watuhumiwa hao wapo maofisini wanaendelea na kazi chafu wanazotuhumiwa nazo.

Baada ya kuona Rais Samia anatoa pole kwa familia na CHADEMA na Kulaani mauaji ndiyo Jeshi la Polisi likaanza kujifanya linafanya uchunguzi au kuongeza Polisi Wengine kuchunguza tukio la kutekwa Ali Kibao na kuuwawa.

12.CHADEMA wasiingie katika mtego huo wa kuhojiwa na Polisi tena na RCO ambaye yupo chini ya Usimamizi wa Boss wake ZCO Faustine Mafwele ambaye CHADEMA wamemtuhumu hadharani kuhusika na mutekwa na Kupotea kwa watu Dar es saalam ikiwemo Godwin Mlay, Deusdedith Soka na Frank Mbise.

Badala yake CHADEMA waandae ushahidi na mashahidi wao kwenda kutoa taarifa na maelezo kwa tume huru ya kijaji kama ilivyokuwa kwa Jaji Kipenka Mussa katika mauaji ya Wafanyabiashara wa Mahenge, Morogoro itakayokuwa huru kukusanya taarifa, kuhoji wahusika na mashahidi pamoja na kutoa mapendekezo juu ya kila tuhuma za mtuhumiwa.

Boniface Jacob
Ex-Mayor
0712 239 595
The voice of the silenced Majority
 
1.Unamteka mtoto wa kike kwa mtutu wa bunduki

2.Kundi la wanaume saba wakatili mnakubali kwenda kumteka, kumdalilisha, kumnyanyasa na kutweza utu wa mwanamke kwa ujira wa fedha?

3.Mnafunga kitambaa usoni mwanamke kisha mnamtoa nyumbani kwake Kibiti mnamsafirisha hadi mapori ya Kisarawe kwenda kumnyanyasa na kumfanyia ukatili

4.Mnajitambulisha kuwa ni maafisa wa chombo cha dola kisha mnatumia gari la kodi za wananchi, pingu na bunduki zilizonunuliwa kwa kodi zetu.

5.Mnachana nguo za mwanamke aliyefunzwa kujistiri kwa dini yake safi ya kiislamu tangu utotoni na kumuacha utupu.

6.Mwanamke mmoja anashirikiana na wanaume saba kumshambulia na kumdhalilisha mwanamke mwenzake kwa ujira wa pesa tu

7.Mmemaliza kumfanyia ukatili Mwanamke mnamtekeleza maporini mnaondoka na kujiona wajanja... mnajiona mmeyapatia maisha kweli.

8.Nawakumbusha yupo Mungu juu anayeona kila kitu muda wote na sehemu zote. Ipo siku kabla hamjazikwa na kufukiwa na udongo huu mnaotumia kumwaga damu, mtakumbushwa kila tukio moja mlilotenda.

9.Nawaonea huruma ninyi watekaji na wauaji, kwa kuwa najua hamjui watu makatili kama ninyi mwisho wenu unakuwaga vipi.

10.Lakini niwahakikishie akili za upinzani na harakati hazizimwi kwa mtutu wa bunduki na kufuli la Jela tulifikiri mmejifunza kwa Hayati Magufuli

Hamtoweza kuua watu wote,wapo watakaobaki nyuma yetu,wao watatulipia visasi vyetu.hilo mnatakiwa kulielewa siku zote.

Hakunaga Jambo linafanywa na watu zaidi ya wawili likabakia kuwa siri.
Credit: Boni yai Twitter
20241023_051623.jpg
 
8.Nawakumbusha yupo Mungu juu anayeona kila kitu muda wote na sehemu zote. Ipo siku kabla hamjazikwa na kufukiwa na udongo huu mnaotumia kumwaga damu, mtakumbushwa kila tukio moja mlilotenda.
Wala haya maneno hayawatishi
 
Will due respect
Naomba uongozi wa JF utafakari tena uamuzi wa kuifuta mada husika niliyoiweka hivi karibuni
Ni mada inayohusika na uhai wa watu .. Kwenye dunia hii hakuna kitu cha thamani kama uhai kwakuwa hakuna vipuri vya uhai
Naomba with all due respect mada husika iweze kurudishwa ili JF ionekane ni sehemu ya kuunga mkono dhidi ya udhalimu wa utekaji na mauaji yanayoendelea nchini
Naamini kati ya wengi waliotekwa, kupotea ama kuuliwa wamo pia wanachama, wapenzi na wafuasi wa jukwaa letu pendwa la JF

JF ina watu wa kila aina na wenye habari za kila aina kwenye kila kitu .. Na ndio maana kwasasa inachukuliwa kama chanzo cha uhakika cha taarifa nyingi (credible source)
Naamini kwa dhati ya moyo mada husika ingeachwa hewani zingekuwa zimeshapatikana taarifa nyingi na pengine nyeti juu ya hali tuliyo nayo kwasasa kuliko kila wakati kuwa na mada nyingine mpya
Waliotekwa, waliopotea, waliopotezwa na waliouawa ni sehemu ya JF kwakuwa JF ni ya wote.. Naomba sana tuitoe kifungoni mada husika kuonesha support yetu kwa hao wahanga wote wa natukio tajwa
Kwa heshima na tadhima
Kwa uhai na ustawi wa JF
Naomba ikuwasilisha

Ndimi mjoli wenu
Mshana Jr
Kilingeni Msata
September 12 2024
Nilikua nasikiliza C2N

Aisee madhila ya docta ulimboka aisee alisimulia mpaka nilisisimka anasema alipigwa Kama kitenesi pigwa n'golewa kucha tolewa meno pigwa Sanaa

Mpaka leo kina SOKA na wenzake hawajulikani walipo.

Siku izi hata mwenyekiti wa bavicha taifa Dogo pambalu kakaa kimya kabisa simsikii akizungumza.
 
Back
Top Bottom