One incredible vs stereo

One incredible vs stereo

The impeccable u cant criticize, they got ill skills dont you feel these guyz, they bring one hit that they can kill twice

Impeccable
 
Kwenye kilinge mbinde tight mic na kiganja, panga vina kama lebo kwenye shati la kiranja, usiende kuwanga kisa kocha hakupi namba, ukiwa boss tu jamaa watasema safi tu hata ukijamba
Hapa mwenye usongo najieleza nawapakaza choo nachimba natoboa nachukia ubishoo zaidi ya hata mimba mnazotoa mimi ndo Chunda boy nadindisha kila mboko huwa sizami chaka kusaka na jibwa koko, tega masikio wakueleze wenzio kila zikigonjwa ngoma zenu wanazima radio

Stereo (Let it be)
 
Chunda badi dudu killer nakemea pepo kwa flow kama mchungaji tila nafanya mashambulizi natuliza ball lango limejaa walinzi zangu shoot mbili goli
Wabaya watakupa hadi sumu huku kitaa vibabu vinavuta hadi ndumu mabitozi wanakwepa majukumu hali ngumu
Verse tamu kama sukari ya mtibwa nagombania midundo kama pilau ya msiba, nawagonga bila mchele wa kuhonga, vina na tungo zao ni mitutu ya kuchonga
Stereo (Tungo)
 
Niko simple kama shaolin moka,bench humuoni mess hii ni shaolin soccer, shaolin coca ,kata kiu nipige mbiu misitari inatema sumu kama shaolin nyoka(stereo swahili)
 
We mwenyewe hapo kwene simu yako una ngoma za kina sholomwamba manfongo na kina shilole.hapa jukwaani unajifanya mgumu*
Haki ya Mungu sijawahi kuweka nyimbo ya shilole na wala sina nyimbo za singeli labda bongofleva na RnB Benpal, Diamond, kiba Belle9, Maua sama, Jux maana mimi sio mgumu
 
Yaaan kayumba mno.nadhani kaanguka kabida.nas na j .z wa kitambo sana.ni sawa na useme humsikii dugu au proffesor j.
Hawa watoto shule zifunguliwe warudi kusoma.nas na jzee uwafananishe na waimba viduku as marekani kina tyga?huku no kukomaa adabu :
 
Unajua hawa machalii wanaswaga zile za East Coast wakimwiga zaidi Nas kuanzia delivery, wordplay etc.... kiukweli wana skills kwenye mic lakini wote wana lyrical content mbovu.
Mkuu ukipata muda fafanua statement yako
 
"Maisha yangu yana ubora mwenzangu ana ubora gani hata nikiwa bora nani atakuwa bora nami sina roho ya upinzani nina roho ya ushindani..mwenyezi anibarikie kesho bora yenye amani" one the incredible (Kesho Yetu)
Haya maisha ni safari na hili gari ni bovu, hii hali ya hatari na sirikali ina uovu, dereva ni mkali ilihali ni kipofu, ila mwisho ni jeneza ndo mahali pa wokovu, baba sali sana muumba akupe mema acha hali ya kujuana kayumba asome vyema, nasali sana ila sio mwenye dhambi anione mwema, .....kesho ya jana isiwe kesho ya leo, maisha yamekua mchezo na uwezo ni matokeo, mzazi mjali mkeo sio kimeo, kesho itafika vp hili taifa likifa leo..
 
Back
Top Bottom