wewe unadhani unapenda kumbe ndo unachunwa
we unadhani unapanda kumbe ndo unavunwa
.....
ile ngoma kali sana ilikuwa aifanye mbishi peke yake umeme ukazingua kesho wenzake kusikia beat wakaipenda kila mtu akataka atupie verse.. duke kakubari
Sizungumzi na mwana, nazungumza na mzazi, huu uzungu wa kuuzana kama ruzuku ya jambazi, kumbuka, wema watoto wakwepe mkosi, baba ana nyumba ndogo kigezo kubwa haitoshi, anazuga anakupa support, yuda eskariot, pochi inashinda kwa mchumba bi mkubwa ale karoti, ona vijana wanakosa malezi kisa mama hana uwezo baba yupo kwa mpenzi lisa, ama baba hana uwezo na mama haiwezi shida, ezi zimepita kisa ana mpenzi wa kumridhisha, kumbuka haya maisha safari, pole kwetu waliokufa wamemaliza tayari, wasifu was sifa sio sifa jijari, njoo upate maarifa hii taarifa ya habari, Ona watoto wanaomba wanakosa wana njaa kwa sababu wazazi wameponzwa na tamaa, hili janga la jamii sio janga la jamaa, binti mwenye kilanga kalamba dume la mtaa, hii ni kwako wewe rafiki yangu jihami kama huwezi kuwa mwema siwezi kuwa jirani, sina imani nawe usiwe na imani nami, kama sote ni wanyama mi ni simba we ni nyani, ....
Kuwa na imani ili amani ipate nafasi, mchunge mwana wa jirani asidanganywe na fataki....
[HASHTAG]#HISIA[/HASHTAG], hii ngoma noma