donlucchese
JF-Expert Member
- Mar 23, 2011
- 17,128
- 21,885
Mnamo mwezi December 1992, raisi wa Marekani wa wakati huo Georgw H.W Bush alitoa amri kwa majeshi ya marekani kuungana na umoja wa mataifa katika operation ya pamoja iliyoitwa 'operation rejesha tumaini (operation restore faith)' na dhumuni la msingi ilikua kurudisha amani na 'order' katika nchi ya Somalia.
Kipindi hiko nchi ya Somalia ilikua imeharibiwa kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe na njaa kali kutokana na kutawaliwa na faction leaders (nimekosa tafsiri iliyo rasmi) na kwa miezi mingi iliyofuata hali ilizidi kutetereka.
Mnamo tarehe 20 January 1993, rais aliefuata baada ya Bush, Bill Clinton alichukua ofisi.
Mwezi May 1993, vikundi vyote vilivyokua vikihusika na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe vilikubaliana kukaa kikao na kusitisha mapigano ambapo kikao hicho kiliongozwa na Mohamed Farrah Aidid.
Kikao jicho kilipelekea kuanzishwa kwa muungano wa kisiasa uliojulikana kama The Somali National Alliance (SNA) mwezi wa sita 1993.
Muunganiko huo ulihusisha vikundi mbali mbali ambavyo vyote vikawa chini ya utawala wa Aidid, baada ya Aidid kujitangaza kua raisi wa Somalia.
Wakati huo huo raia wengi wa Somalia walipinga shughuli za majeshi ya Marekani nchini mwao ambapo watu wengi hususan wanawake na watoto walijitokeza na kukamata silaha kupambana dhidi ya majeshi ya Marekani wakati wa mapambano katika mji wa Mogadishu.
Tarehe 5 June 1993, moja ya mashambulizi mabaya zaidi kutokea kwa vikundi vya majeshi ya umoja wa mataifa (UN) nchini somalia lilitokea na kupeleka vifo vya wanajeshi 24 wa Pakistan walifanyiwa 'ambush' na kuuawa katika eneo lililokua chini ya utawala wa Aidid.
Matumaini yeyote ya kumaliza mgogoro kwa njia ya amani yalitoweka rasmi na ndipo baraza la usalama la UN ( UN Security council) lika-issue kitu kilichoitwa "Resolution 837".
Hili lilikua ni tamko rasmi kuhusu kusakwa hadi kukamatwa na kuhukumiwa wale wote waliohusika na shambulizi lile.
Ndege za Marekani na majeshi ya UN yakaanza mashambulizi katika ngome za Aidid lakini bwana Aidid akabaki kua mkaidi na mashambulizi kati ya wasomali na vikundi vya majeshi ya umoja wa mataifa yakashamiri kwa hali ya juu.
Itaendelea.......
Kipindi hiko nchi ya Somalia ilikua imeharibiwa kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe na njaa kali kutokana na kutawaliwa na faction leaders (nimekosa tafsiri iliyo rasmi) na kwa miezi mingi iliyofuata hali ilizidi kutetereka.
Mnamo tarehe 20 January 1993, rais aliefuata baada ya Bush, Bill Clinton alichukua ofisi.
Mwezi May 1993, vikundi vyote vilivyokua vikihusika na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe vilikubaliana kukaa kikao na kusitisha mapigano ambapo kikao hicho kiliongozwa na Mohamed Farrah Aidid.
Kikao jicho kilipelekea kuanzishwa kwa muungano wa kisiasa uliojulikana kama The Somali National Alliance (SNA) mwezi wa sita 1993.
Muunganiko huo ulihusisha vikundi mbali mbali ambavyo vyote vikawa chini ya utawala wa Aidid, baada ya Aidid kujitangaza kua raisi wa Somalia.
Wakati huo huo raia wengi wa Somalia walipinga shughuli za majeshi ya Marekani nchini mwao ambapo watu wengi hususan wanawake na watoto walijitokeza na kukamata silaha kupambana dhidi ya majeshi ya Marekani wakati wa mapambano katika mji wa Mogadishu.
Tarehe 5 June 1993, moja ya mashambulizi mabaya zaidi kutokea kwa vikundi vya majeshi ya umoja wa mataifa (UN) nchini somalia lilitokea na kupeleka vifo vya wanajeshi 24 wa Pakistan walifanyiwa 'ambush' na kuuawa katika eneo lililokua chini ya utawala wa Aidid.
Matumaini yeyote ya kumaliza mgogoro kwa njia ya amani yalitoweka rasmi na ndipo baraza la usalama la UN ( UN Security council) lika-issue kitu kilichoitwa "Resolution 837".
Hili lilikua ni tamko rasmi kuhusu kusakwa hadi kukamatwa na kuhukumiwa wale wote waliohusika na shambulizi lile.
Ndege za Marekani na majeshi ya UN yakaanza mashambulizi katika ngome za Aidid lakini bwana Aidid akabaki kua mkaidi na mashambulizi kati ya wasomali na vikundi vya majeshi ya umoja wa mataifa yakashamiri kwa hali ya juu.
Itaendelea.......