Elections 2015 Operesheni Zinduka: Uamuzi Sahihi 2015

Elections 2015 Operesheni Zinduka: Uamuzi Sahihi 2015

Mi hua najiuliza, why not Lowasa? Sielewi, why nguvu nguvu kubwa hivi inatumika? Sielewi, hivi kama lowasa mwizi si wamkamate tu yaishe? Sielewi, kuna experiment kubwa sana ya kufanya, why not vote for him ili nigundue? Duh huyu lowasa ni binadamu wa aina yake. Mara fisadi, mara mgonjwa, mara mlutheri, mara mkaskazini duh, nimezindukaaaaa

Wahenga walisema usichezee shilingi chooni.
 
NB: Video Inafuata

Operesheni Zinduka imeanza kama nilivyoahidi (jana haikuwezekana kwa sababu moja tu ya heshima ya Mch. Mtikila na haihusiani na mipango ya watu wengine). Nitajitahidi kuwa na onesho hili kila siku (ukiondoa mwisho wa Juma) na nitazungumzia mada mbalimbali. Wiki hii ya kwanza zaidi nitagusia hoja nyingi zilizoibuliwa kutushangaa tunaomkataa Lowassa kama mgombea Urais kwa tiketi ya upinzani.

La pili nitajitahidi hasa wiki ile inayokuja kutoa nafasi kwa wagombea wa CHADEMA kwenye Ubunge (ambao tutaweza kuwafikia) ili wajiuze kwani ninaamini Bunge lenye nguvu lililoundwa na watu waliolelewa na kukomaa katika upinzani na wenye kuelewa hasa ajenda ya upinzani ndio chachu ya kweli ya mabadiliko tuyatakayo. Hivyo, wiki ile inayokuja tutatoa nafasi hii kwa wote tutakaoweza kuwapata.

Tatu, kwa vile nina uhakika wapo wengi ambao hawajakubaliana na uamuzi wangu huu (ambao naamini ni sahihi) basi nitatoa nafasi pia kwa watu wengine kutoa hoja zao dhidi ya ninachosema (sikiliza onesha hili juu ya 'mashart kuzingatiwa'). Kwa barua pepe anuani yangu ipo chini na namna nyingine ya mawasiliano nitawajulisha siku chache zijazo.

Nitajitahidi kuweka shows zote kwenye uzi huu huu kila siku, na video zitafuata chini toka ya zamani zaidi hadi mpya zaidi.

Mwisho, ninaamini na nina uhakika kuwa kwa atakayeamua kunisikiliza kuanzia sasa hadi kuamkia Uchaguzi Mkuu hatoweza kumpigia Lowassa kura ya Urais. Ni kwa sababu hiyo wale ambao tayari wameshaamua kuwa haijalishi nini kitasemwa juu ya Lowassa nawaomba au kuwashauri wasisikilize mada hizi wasije kujikuta wanabadili mawazo. Mada hizi ni kwa wale tu ambao bado hawajaamua au wale ambao wameamua lakini bado wanajikuwa wanavuta na upepo wa 'nyomi' kiasi kwamba bado hawajathibitika katika msimamo wao.

"Uamuzi Makini, Uamuzi wa Lazima, Uamuzi Sahihi"

MMM

ONESHO 1. "Baada ya Kelele Sauti za Hoja Zitashinda"


ONESHO 2. "Makosa 2 ya Dr. Slaa na 1 la Mbowe - Jumatano Oktoba 7, 2015)

<strong>




  1. Kuna Haja Gani Ya Kuendelea Kushabikia Vyama (CHADEMA, TLP n.k.) Wakati Havina Misimamo Bali Vinaburuzwa na Wanaoviongoza?
  2. Wengine Tulishasema Siku Nyingi Kuwa Tatizo la CHADEMA Ni Mbowe, Je Ni Kwa nini Wafuasi Wengi Wa CDM Ikiwa ni Pamoja na Mkuu Mwanakijiji Hamlioni Hilo?
  3. Je Vijipesa Vya Mbowe Kuwapatia Waliokaribu Yake, Ikiwa ni Pamoja na Dr. Slaa (Nyumba), JamiiForum.com (kulipia host), MMJJ (???) n.k. Ndio Vilivyotufikisha Hapa pa Kuyumbishwa na LOWASSA?
 
Last edited by a moderator:
NB: Video Inafuata

Operesheni Zinduka imeanza kama nilivyoahidi (jana haikuwezekana kwa sababu moja tu ya heshima ya Mch. Mtikila na haihusiani na mipango ya watu wengine). Nitajitahidi kuwa na onesho hili kila siku (ukiondoa mwisho wa Juma) na nitazungumzia mada mbalimbali. Wiki hii ya kwanza zaidi nitagusia hoja nyingi zilizoibuliwa kutushangaa tunaomkataa Lowassa kama mgombea Urais kwa tiketi ya upinzani.

La pili nitajitahidi hasa wiki ile inayokuja kutoa nafasi kwa wagombea wa CHADEMA kwenye Ubunge (ambao tutaweza kuwafikia) ili wajiuze kwani ninaamini Bunge lenye nguvu lililoundwa na watu waliolelewa na kukomaa katika upinzani na wenye kuelewa hasa ajenda ya upinzani ndio chachu ya kweli ya mabadiliko tuyatakayo. Hivyo, wiki ile inayokuja tutatoa nafasi hii kwa wote tutakaoweza kuwapata.

Tatu, kwa vile nina uhakika wapo wengi ambao hawajakubaliana na uamuzi wangu huu (ambao naamini ni sahihi) basi nitatoa nafasi pia kwa watu wengine kutoa hoja zao dhidi ya ninachosema (sikiliza onesha hili juu ya 'mashart kuzingatiwa'). Kwa barua pepe anuani yangu ipo chini na namna nyingine ya mawasiliano nitawajulisha siku chache zijazo.

Nitajitahidi kuweka shows zote kwenye uzi huu huu kila siku, na video zitafuata chini toka ya zamani zaidi hadi mpya zaidi.

Mwisho, ninaamini na nina uhakika kuwa kwa atakayeamua kunisikiliza kuanzia sasa hadi kuamkia Uchaguzi Mkuu hatoweza kumpigia Lowassa kura ya Urais. Ni kwa sababu hiyo wale ambao tayari wameshaamua kuwa haijalishi nini kitasemwa juu ya Lowassa nawaomba au kuwashauri wasisikilize mada hizi wasije kujikuta wanabadili mawazo. Mada hizi ni kwa wale tu ambao bado hawajaamua au wale ambao wameamua lakini bado wanajikuwa wanavuta na upepo wa 'nyomi' kiasi kwamba bado hawajathibitika katika msimamo wao.

"Uamuzi Makini, Uamuzi wa Lazima, Uamuzi Sahihi"

MMM

ONESHO 1. "Baada ya Kelele Sauti za Hoja Zitashinda"


ONESHO 2. "Makosa 2 ya Dr. Slaa na 1 la Mbowe - Jumatano Oktoba 7, 2015)

<strong>


Mkuu Mzee Mwanakijiji

Ambao hawakuelewa Operesheni Zinduka (OZ) wakati ule, bila shaka wakati huu wamepata nuru ya nini hasa ilikuwa hoja zako dhidi ya aliyekuwa mgombea wa CHADEMA. Hongera tena kwa kutuletea OZ
 
Back
Top Bottom