Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hakuna mtendaji yeyote wa serikali aliyewahi kuwa makini kiasi hicho. Wizi wa kura kwa kutumia michakato ya ki IT unahutaji uzoefu, umakini na efficiency ya hali ya juu. I am 100% sure kuwa grave miscommunications zitatokea kati ya uongozi wa juu wa tume, makamishna, na wasimamizi majimboni. Ukijumlisha na pressure ya umma watanzania na mataifa mbalimbali, watachanganyikiwa mapema sana...
Kuiba wataiba, lakini utakuwa wizi wa mchana, yaani kila detail ya wizi itakuwa wazi.
u-salva rweyimumuMM Kwanza nikuombe uweke maslahi yako wazi,wewe kama mwandishi wa riwaya mimi kama mwandishi wa vitabu na makala tunatofautiana sana pale unapojificha chini ya uvungu wa jambo fulani na kupaza sauti,Mwanzo nilijaribu kuelewa mantiki ya makala zako sikuweza ila sasa nafahamu huyu anae jiita mzee mwanakijiji ni nani? kumbe ni mganga njaa kama wale mitume kumi na mbili wa ufisadi, Natumaini nilipokuwa naandika huku elewa nilikuwa nasemea nini ila Mwenye enzi Mungu hamfichi mnafiki tukawaona wanapewa vyeo na kunyamaza,Enzi zile za rai tuliandika baada ya watu kumpamba mtu matokeo yake walipewa cheo.Swali wewe umeahidiwa cheo gani?Karibu mwalimu forum tunaposema ukweli kwa ajili ya mama yetu Tanzania na sio uchonganishi kwa watanzania.Mungu ibariki Tanzania
Nyie watu acheni unafki nilini mlianza kujua kuwa Lowasa ni Fisadi mayowe haya mnayopiga Yanatudhihirishia bila shaka mmekwiba sana kwenye hii NCHI sasa mnaona huyo jamaa akiingia madarakani Atawafanya vibaya huyo MM yuko kzn so Lazima atimize wajibu wa waliomtuma lkn asidhani km kuna MTU asietumia Utumbo kufikiri ataweza kuMbadilisha kwa hizo Ngano....zake wengine tulishaikataa CCM tangu 1995 sasa kuja na blah blah kama hizi nikupoteza Muda wengine tunazipitia hizi thread kwaajili yakuona Watu wazima wanavyojitoa ufahamu sababu Njaa.......[/QUOT
Sio kila asiyemkubali Lowassa ni CCm.
Mimi ni Chadema,Chadema ile iliyokua ikihubiri kuwa Lowassa ni Fisadi.
Sijui tunaelewana lakini?
Kila chama kina malengo yake....hasa kushika DOLA labda wenzetu nyie mnapenda tuwe na Vyama vya kudumu vya Upinzani Jambo ambalo aliweza kufanya mchgj Mtikila manake ilikuwa ni ngumu kumuelewa anasimamia nini... Sikiliza Rafiki nikwambia siwote tunaomchagua LOWASA nikwamba labda tunakubaliana nae sana NO..ila kwakuwa tunaamini ataweza kutusaidia kuvunja Mgongo wa hili JOKA linaloitwa CCM that Y tutamchagua hata km maendeleo hayatakuwa na kwa kasi km tunavyotamani lkn hali haitakuwa hii tuliyonayo leo Tunataka kila baada 5yrs chama kinachotakuwa Madarakani kisiwe nauhakika wakurudi madarakani km kimedanganya km CCM zaidi ya 50yrs hadi wanatoa Ahadi Tuta...Tuta ..badala ya Tumefanya...huu in Upuuzi KENYA hawapo pale kwa Bahati mbaya.....waliamua kusogeza Mbele nchi yao....Hebu niwaulize nyie Hater's wa EL hivi kwa uchaguzi wa Mwaka huu ulivyo taiti SLAA au LIPUMBA angetia KWATO? acheni ndg zangu tunajua wengi maisha yenu yamefungamana na CCM so hatushangai Nitashanga MTU Riz 1 atakubali kusema CCM ni Mbaya
Nitalijibu hili swali vile vile... stay tuned. Hatari sasa hivi ni zaidi ya CCM!
Haya bana; ila umewahi kuona watu wanasubiria mvua jangwani?
Ahahahaaa daaah!
Nadhani nilipatwa na 'brain fart' nikashindwa hata kufikiri vizuri.
Lakini kwa upande mwingine ni vizuri zaidi kuuliza na kupata jibu kuliko kusadiki.
Sasa nimekuelewa vyema kabisa, Operesheni Zinduka nayo inaingia akilini [hata kama sikubaliani nayo] na kuanzia sasa nitakuwa nazisubiri tu hizo episodes.
Uchaguzi utakuwaje wa huru na haki wakati tume nzima imeundwa na mwenyekiti wa CCM ambaye chama chake pia kitashiriki huo uchaguzi?
Waache kutusi akili za watu.
Uchaguzi utakuwaje wa huru na haki wakati tume nzima imeundwa na mwenyekiti wa CCM ambaye chama chake pia kitashiriki huo uchaguzi?
Waache kutusi akili za watu.
Nani ambae hayupo kwenye payroll ya CCM now?
CCM wanazidi onesha walivyo na uthubutu wa kumkamata yeyote 'ahamie' kwao
kuna thread ilisema Yericko nae kapewa milioni 72 ahamie CCM....it could be uwongo but you can imagine
Mkuu Uteuzi Kufanywa na Mwenyekiti Wa Chama Haiharalishi Uwepo wa Mbinu Za kupora Ushindi. Kumbuka Licha ya makamishinda Kuteuliwa na Mwenyekiti wa Chama lakini katika Mioyo Yao Inawezekana Kukawa na Utofauti Wa Kimsimamo na Rais. Siku Zote Kutanguliza neno kushindwa Katika Mapambano ni kujikatisha tamaa mapema.... Time will tell
Ameen!
Kuna mambo mengi natofautiana na Mwanakijiji, lakini katika hili, nakubaliana nae moja kwa moja. Ni hvibaya kuona ndugu zetu walikuwa brain washed in the name of mabadiliko, bila kujali mabadiliko wanayoahidiwa na hasi au chanya.
Hiyo contradiction wao hawaioni kabisa na hawawezi kuiona kwa sababu zilizo wazi. Na mimi hapa bado sijasema "mpigieni kura Magufuli". Miye ninachosema ni kile kile nilichokisema miaka nane sasa. Lakini naonekana nimebadilika!
Unachosema ni kweli.
Lakini ni kweli pia kuwa, mwenyekiti wa CCM kuunda tume ya taifa ya uchaguzi halafu CCM nayo ni mshiriki wa chaguzi kunaleta mgongano mkubwa sana wa kimaslahi.
Na mtu huhitaji kuwa jiniasi kuuona huo mgongano.
Pia, hata ingekuwa mimi ndo mwenye mamlaka ya kuunda hiyo tume, ni wazi ningeweka watu ambao naamini watakuwa wanashabihiana nami kimtazamo na ambao wataweza kulinda maslahi yangu/ ya chama changu.
Ndo maana sehemu zingine wameamua kuwa na tume huru za uchaguzi.
Duh Mzee Mwanakijiji what a waste of time....mbona hukuenda direct to the point? 12 minutes na hujaongea lolote bado. Dah!
Hivi ni lini wewe uliwahi kuwa upinzani...lini? Ni lini wewe ulitaka mabadiliko?
Dakia 5:24 "wengi ambao hawajui, miaka 20 sasa nimekuwa kwenye harakati hizi..."
Dakika 5:51, "..tuliunga upinzani wakati ule na tumeendelea kufanya hivyo. Pamoja na kwamba tuliamini kwamba labda kwa kufanya hivyo chama ambacho kilikuwa kimeleta uhuru Tanzania kingeweza kubadilika lakini hakijabadilika jinsi ambavyo tulikuwa tumetarajia. Labda safari hii kinaweza kikabadilika "
- Mzee wangu, kwa miaka zaidi ya 50 tumekuwa tukisema hayo hayo unayoyaongea, "labda safari hii kinaweza kikabadilika..." labda..labda..labda...na hakuna siku wamewahi kubadilika!
- Ubaya wa Lowassa ni upi huo ambao mlipokuwa naye mlimuunga mkono kuliko watangaza nia wote waliokuwa kwenye kinyang'anyiro ila sasa amekuwa mbaya kuko Hashim Rungwe (no offence intended)?
- Unataka tena kuja hapa baada ya miaka mitano kutueleza ni kwa namna gani tumejaribu jaribu kuleta upinzani na mwaka 2015 tuliona LABDA watabadilika?
MWISHO: kwenye video zako zitakazofuata tafadhali tafuta mtaalamu akusaidie kwenye speech yako..punguza maneno yasiyo na mantiki. hizi ""eeh" "aaah"! Ninaamini ulijiandaa na uliiandaa speech kabla ya ku-rekodi. Inapoteza ladha kusikiliza! Inakaa kama unawaza kwa kadri unavyozidi kuongea. Go straight to YOUR point..!
Nashukuru.
Usilete pumba hapa watu wameshaamua mabadiliko Mimi na umri wangu wote nmekua kada wa ccm nmekubali mabadiliko nakushangaa ww kijana
mzee hatukutishi bali tunakuambia ukweli msijaribu kucheza na mabomu ambayo alarm imeshaanza kutowa mlio!
kama mlikuwa mnasikia kwa majirani sasa alarm inalia hapa kwetu ole wenu ole wenu vijana hatutarudi nyuma na hamtaweza kuturudisha nyuma me mwenyewe moyo wangu unakaribia kupasuka kwakuona unacho jaribu kutaka kutuaminisha kitu ambacho hakina faida na TANZANIA !!
NN kuna jambo umesema kuhusiana na tume nitaandika baadaye kidogo uone kwanini bapo awali nilosema safari hii tume ni kisingizio siyo sababu ya upinzani kushindwa.