Duh Mzee Mwanakijiji what a waste of time....mbona hukuenda direct to the point? 12 minutes na hujaongea lolote bado. Dah!
Hivi ni lini wewe uliwahi kuwa upinzani...lini? Ni lini wewe ulitaka mabadiliko?
Dakia 5:24 "wengi ambao hawajui, miaka 20 sasa nimekuwa kwenye harakati hizi..."
Dakika 5:51, "..tuliunga upinzani wakati ule na tumeendelea kufanya hivyo. Pamoja na kwamba tuliamini kwamba labda kwa kufanya hivyo chama ambacho kilikuwa kimeleta uhuru Tanzania kingeweza kubadilika lakini hakijabadilika jinsi ambavyo tulikuwa tumetarajia. Labda safari hii kinaweza kikabadilika "
- Mzee wangu, kwa miaka zaidi ya 50 tumekuwa tukisema hayo hayo unayoyaongea, "labda safari hii kinaweza kikabadilika..." labda..labda..labda...na hakuna siku wamewahi kubadilika!
- Ubaya wa Lowassa ni upi huo ambao mlipokuwa naye mlimuunga mkono kuliko watangaza nia wote waliokuwa kwenye kinyang'anyiro ila sasa amekuwa mbaya kuko Hashim Rungwe (no offence intended)?
- Unataka tena kuja hapa baada ya miaka mitano kutueleza ni kwa namna gani tumejaribu jaribu kuleta upinzani na mwaka 2015 tuliona LABDA watabadilika?
MWISHO: kwenye video zako zitakazofuata tafadhali tafuta mtaalamu akusaidie kwenye speech yako..punguza maneno yasiyo na mantiki. hizi ""eeh" "aaah"! Ninaamini ulijiandaa na uliiandaa speech kabla ya ku-rekodi. Inapoteza ladha kusikiliza! Inakaa kama unawaza kwa kadri unavyozidi kuongea. Go straight to YOUR point..!
Nashukuru.
Aisee nimemsikiliza huyu mtu nikaamini kweli kuna watu wanaakili za kushikiwa.
Hivi Tanzania ilipofika bado kuna kijana mwenye nguvu ya kumpinga mgombea wa upinzani hata angekua ni panya?
Hivi hata Mzee Kingunge anauchungu kuliko vijana ambao wana years ahead???
Ivi Wa Tanzania tuko serious kabisa tunashabikia CCM? Kwa lipi?
MMM unahisi kwa kumpinga Lowasa unamsapoti nani? Kwalipi? Na kwa faida ya nani?
Unaposema Watanzania wamenyimwa mgombea sahihi, halafu unasema hauna tatizo Na uongozi/Mbowe, huoni ni unafiki?
Nani amewanyima? Ulitaka awe nani? Vita yako unamuelekezea nani?
Tanzania iko pabaya, maybe kwavile wewe ni mwanaume hauingii chumba cha uzazi, hujui adha tuipatayo wanawake, maybe ndio maana unaujasiri wa kuongea unayoyaongea.
Jamani, tuwe realistic, wa Tanzania tunateseka...we need change ya mfumo, Na huweziujua unless umeupa nafasi.
UKAWA is all I need! Hope you Know what that means.
MMM acha ujinga.
Gudluck!
Last edited by a moderator: