Orodha ya Nchi zinazoongozwa Kidini au Dini inanguvu ya ushawishi

Orodha ya Nchi zinazoongozwa Kidini au Dini inanguvu ya ushawishi

Mhaya

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2023
Posts
1,831
Reaction score
5,489
Hapa kuna orodha ya nchi zinazoongozwa kwa sera za kidini au ambazo dini ina ushawishi mkubwa kwenye serikali na sheria za kitaifa. Nimezipanga kulingana na dini husika:

1. Uislamu (Nchi za Kiislamu)

Nchi hizi zinafuata sheria za Kiislamu (Sharia) kikamilifu au kwa kiwango kikubwa katika mfumo wa serikali:

Saudi Arabia – Nchi inaongozwa kwa sheria za Uislamu wa Sunni (Madh'hab ya Hanbali)

Iran – Nchi inaongozwa kwa sheria za Uislamu wa Shia (Jamhuri ya Kiislamu)

Pakistan – Jamhuri ya Kiislamu (Nchi ina mchanganyiko wa Sharia na sheria za kiraia)

Afghanistan – Nchi inaongozwa kwa Mfumo wa sheria za kiisilamu (Sharia) chini ya Taliban. Wanasimamia misingi mikali ya uislamu.

Sudan – Sheria za Kiislamu (Sharia) zina ushawishi mkubwa kitaifa.

Mauritania – (Sharia) sheria za Kiislamu ni msingi wa sheria zote nchini.

Yemen – Mfumo wa sheria za kiisilamu (Sharia) unatekelezwa kikamilifu.

Maldives – Uislamu wa Sunni ndio dini ya serikali.

Somalia – Sheria kiislamu (Sharia) zinatumika kwa kiwango kikubwa.

Nchi nyingine zisizochini ya sheria ya kiislam ila zina ushawishi wa Sharia au Uislamu:

Brunei – Inafuata sheria za kiisilamu (Sharia) kwa baadhi ya masuala, hasa ya kijamii na ya maadili.

Indonesia – Ingawa ni nchi ya kidemokrasia, sheria za Kiislamu zinaathiri baadhi ya mikoa kama Aceh.

Bangladesh – Uislamu ni dini rasmi ya taifa, na baadhi ya sheria za kidini hutumika.

Kuwait – Sheria ya kiislam (Sharia) zinaathiri mfumo wa mahakama.

Qatar – Inafuata sheria za kiisilamu (Sharia), ingawa kuna sera za kisasa.

United Arab Emirates (UAE) – mfumo wa sheria za kiisilamu (Sharia) zinatumika hasa kwa masuala ya familia na maadili.

Nigeria – Sehemu za kaskazini zinafuata sheria za kiisilamu (Sharia), ingawa taifa lote ni la dini mchanganyiko.

Egypt – Uislamu ni dini rasmi, na Sheria ya kiislam (Sharia) inaathiri mfumo wa sheria.


2. Ukristo (Nchi za Kikristo)

Ingawa nchi nyingi za Kikristo ni za kidemokrasia, baadhi zina dini rasmi ya serikali au ushawishi mkubwa wa Ukristo:

Vatican City – Nchi ya Kikatoliki (teokrasia ya Papa)

Greece – Orthodoksi ya Kigiriki ni dini ya taifa. Dhehebu la Orthodoksi ndio mhimili wa taifa.

Denmark – Kanisa la Denmark la Kilutheri (Lutheran) ni la taifa. Dhehebu la Kilutheri ndio linashikilia miiko ya Nchi.

Norway – Kanisa la Kiinjili la Kilutheri ni dini ya serikali.

Iceland – Kanisa la Kilutheri ni dini ya taifa.

England (Uingereza) – Kanisa la Anglikana (Anglican) ni dhehebu rasmi la taifa, lakini serikali ni ya kidemokrasia na kifalme.

Nchi nyingine za kawaida zenye ushawishi mkubwa wa Ukristo

Poland – Kanisa Katoliki (Catholic) lina ushawishi mkubwa kwenye siasa, ingawa ni nchi ya kidemokrasia.

Malta – Katoliki (Catholic) ni dhehebu rasmi la taifa, na sheria nyingi zinategemea mafundisho ya Kanisa la kikatoliki.

Armenia – Kanisa la Armenia Apostolic Church lina ushawishi wa kijamii na kisiasa.

Costa Rica – Katoliki (Catholic) ni dhehebu rasmi, ingawa kuna uhuru wa kidini.


3. Uyahudi (Nchi ya Kiyahudi)

Israel – Ingawa ni demokrasia, Israel inajitambulisha kama "nchi ya Kiyahudi" na ina sheria fulani za kidini, hasa kuhusu ndoa na utambulisho wa taifa.


4. Dini za Kiasia (Buddhism, Hinduism, na Confucianism)

Nepal
– Ingawa ni nchi ya kidemokrasia, ina ushawishi mkubwa wa dini ya Hindu (hapo awali ilikuwa Himaya ya Kihindu).

Bhutan – Buddhism ya Tibetan ndio dini ya taifa, na Sheria za Buddha zinaathiri utawala mzima.

Myanmar – Ingawa serikali si rasmi ya kidini, Buddhism ina nafasi kubwa katika siasa na maisha ya kila siku ya raia.

Sri Lanka – Buddhism ya Theravada ina ushawishi mkubwa, na katiba inatambua nafasi maalum ya Buddha.

Nchi nyingine zisizo chini ya sheria ya Kibudha au Kihindu ila zenye ushawishi wa kidini katika siasa au sheria za kibudha na kihindu:

Thailand – Buddhism ya Theravada ni dini ya taifa, na mfalme hutambulika kama mlinzi wa Buddha.

Cambodia – Buddhism ni dini rasmi na ina ushawishi mkubwa katika siasa.

India – Ingawa India ni nchi ya dini mchanganyiko, imani ya Hindu inaathiri baadhi ya maamuzi ya kisiasa.

5. Dini za Kikristo na kiislamu Tu

Eritrea
– Serikali inatambua dini rasmi mbili tu (Ukristo na Uislamu; ambapo kwenye Ukristo ni madhehebu ya Orthodoksi, Katoliki, na Lutheran tu ndio upewa kipaumbele), huku dini nyingine zikikandamizwa.



HITIMISHO
Japo kuna nchi nyingi za zinaidadi kubwa ya watu ambao ni waumini wa Dini fulani lakini hii orodha inazingatia nchi ambako dini ina ushawishi mkubwa kwenye Mamlaka za uongozi au ni rasmi katika sera za kitaifa.
 
Dini za watu kuziita za kiasi maana ake ni nini? Au ndipo uelewa wako ulipo ishia
 
Saudi Arabia moja kati ya nchi tamu Sana kwa biashara na good time tatizo udini mingi.

Recently Warussia & Waingereza wengi zaidi wamevamia Dubai kuanza life "fresh start" & kuinvest hope mapema siku zijazo udini utapungua .

Tho Kuchomoa life pale Dubai ni more easy kuliko huku dunia ya tatu, Nauli yako tu.
 
nakurebeshia list, Maelezo utayakuta

1. UISLAMU
2.HINDUISM (Dini kuu ya India)
3. ---
4. ---
5. Ukristo

HINDUISM

Naomba nikusahishe, Namba mbili weka dini ya wahindi inayoitwa Hinduism, wana miungu mingi lakini imekusanyika kwa dini hiomoja, Hao watu wana itikadi kali sana za kidini waweke namba mbili, waislam na wakristo wengi sana wanauwawa,kubakwa, kubaguliwa huko india, Dini ina matabaka ya watu ukizaliwa tabaka flani imeaminishwa umezaliwa kuteseka na kutumikishwa, Kuna kampeni ya HINDUTIVA yenye lengo la kuifanya nchi iongozwe kwa misingi ya dini,

UISLAM

Tunarejea dini ya nchi za kiislam hawa ni shida, ni nchi zinazokandamiza dini nyingine na waislam wanaotoka nje.

Nchi kama Saudi Arabia, Afghanistan, Sudan, Iran, n.k. ukiwa muislam ukitangaza umebadili dini sheria zipo wazi UNAUWAWA, nchi kama Malaysia kubadili dini uende mahakama ya mashehe kuomba kibali cha kubadili dini, Utasubiri sana !! Lakini ukiwa mkristo ukibadili dini hutapata usumbufu wowote

Waislam wakijaa nchi flan ni ngumu sana dini nyingine kupata haki zao, Tusiende mbali sana angalia Zanzibar hawaruhusu mkristo aoe Muislam, Mfungo ukifika wakristo hawaruhusiwi kuendelea na ratiba zao za kula, ukikutwa unapigwa sana na kufungwa,

Nchi za kiislam nyingi zina vikundi vya kuua wasio waislam, Hapa Afrika kwa mfano Nigeria wakristo wanawindwa kama wanyama.

UKRISTO

Ukija kwenye nchi za kikristo dini nyingine zipo huru huwezi kusikia mtu kabadili dini apate kibali, apigwe, kufungwa au kuuwawa, Watu wa dini nyingine hawaitwi majina ya ajabu mfano kafir, dini nyingine wengi wanapewa vyeo na kazi kwenye nafasi za uongozi na taaluma, n.k
 
Ndio shida ya kutoroka shule wakati wenzako wanafundishwa... Kwanza sio Kiasi ni Kiasia neno linalotokana na bara la Asia.

Ujinga wako wa miaka kadhaa nyuma unatugharimu na sie
Ahahah
 
Saudi Arabia moja kati ya nchi tamu Sana kwa biashara na good time tatizo udini mingi.

Recently Warussia & Waingereza wengi zaidi wamevamia Dubai kuanza life "fresh start" & kuinvest hope mapema siku zijazo udini utapungua .

Tho Kuchomoa life pale Dubai ni more easy kuliko huku dunia ya tatu, Nauli yako tu.
Saudi Arabia inaanza kuchachuka , miji ya kiimani zaidi ni Mecca na Madina ila huku kwengine bata zipo.Dubai jiji la kisasa lile
 
Saudi Arabia inaanza kuchachuka , miji ya kiimani zaidi ni Mecca na Madina ila huku kwengine bata zipo.Dubai jiji la kisasa lile
Yessir, bata zipo na udini upo, Asilimia kukwa ya waarabu Wana ubaguzi unaosababishwa zaidi na dini, just udini ukipungua just kwa 30% itakua unyama Sana.
 
nakurebeshia list, Maelezo utayakuta

1. UISLAMU
2.HINDUISM (Dini ya tatu kwa watu wengi)
3. ---
4. ---
5. Ukristo

HINDUISM

Naomba nikusahishe, Namba mbili weka dini ya wahindi inayoitwa Hinduism, wana miungu mingi lakini imekusanyika kwa dini hiomoja, Hao watu wana itikadi kali sana za kidini waweke namba mbili, waislam na wakristo wengi sana wanauwawa,kubakwa, kubaguliwa huko india, Kuna kampeni ya HINDUTIVA yenye lengo la kuifanya nchi iongozwe kwa misingi ya dini,

UISLAM

Tunarejea dini ya nchi za kiislam hawa ni shida, ni nchi zinazokandamiza dini nyingine na waislam wanaotoka nje.

Nchi kama Saudi Arabia, Afghanistan, Sudan, Iran, n.k. ukiwa muislam ukitangaza umebadili dini sheria zipo wazi UNAUWAWA, nchi kama Malaysia kubadili dini uende mahakama ya mashehe kuomba kibali cha kubadili dini, Utasubiri sana !! Lakini ukiwa mkristo ukibadili dini hutapata usumbufu wowote

Waislam wakijaa nchi flan ni ngumu sana dini nyingine kupata haki zao, Tusiende mbali sana angalia Zanzibar hawaruhusu mkristo aoe Muislam, Mfungo ukifika wakristo hawaruhusiwi kuendelea na ratiba zao za kula, ukikutwa unapigwa sana na kufungwa,

Nchi za kiislam nyingi zina vikundi vya kuua wasio waislam, Hapa Afrika kwa mfano Nigeria wakristo wanawindwa kama wanyama.
Umeelezea vizuri sana, ila mimi sikupanga kwa Idadi ya waumini wa Dini.... Nimepanga ambazo zinaongozwa waziwazi kwa sheria za kidini, bila kujali dini hiyo ina waumini kiasi gani wa dini fulani

Siku nyingine nitakuja na orodha ya dini zenye wafuasi wengi
 
Saudi Arabia inaanza kuchachuka , miji ya kiimani zaidi ni Mecca na Madina ila huku kwengine bata zipo.Dubai jiji la kisasa lile
Saudi Arabia ni nchi inayoongozwa kwa sheria za kiisilamu za Kisunni (Wasali Sunna) Nchi nzima)

Dubai haipatikani katika Nchi ya Saudi Arabia, Dubai inapatikana kwenye Nchi ya United Arab Emirates (UAE) yani umoja wa falme za kiarabu. Dubai ni mji wa kibiashara, Mji mkuu ni Abu Dhabi.

Saudi Arabia ni nchi tofauti kabisa na UAE, pia mwambao huo huo kuna Nchi inaitwa Qatar ambao mji wake mkuu ni Doha
 
Nchi nyingi zinazoongozwa kwa misingi ya imani fulani hapo ni mtihani sana kuishi, achilia mbali wageni..hata wao kwa wao tu.
 
SIJAONA SIS WALOKOLE
Makanisa ya Kilokole yalianza miaka ya juzi juzi tu huko Marekani ukilinganisha na madhehebu mengine yalianza kipindi cha wanafunzi wa Yesu au karne za mwanzo baada ya Yesu, ambayo kwa asilimia kubwa yalipewa nafasi kubwa kwenye jamii. Walokole ambao kwa kwa kimombo yanajulikana kama Evangelical au Born-Again Christians.

Dhehebu hili lilianza katika harakati za uamsho za Kikristo huko Marekani na Ulaya mwishoni mwa karne ya 19 na mwanzoni mwa karne ya 20.

Katika Afrika Mashariki, harakati ya Walokole ilianza kusambaa sana katika miaka ya 1930 na 1940, ikianza na uamsho wa Balokole huko Uganda na baadaye kuenea Tanzania, Kenya, na maeneo mengine ya Afrika. Kipindi ambacho Nyerere anapigania uhuru
 
Nchi nyingi zinazoongozwa kwa misingi ya imani fulani hapo ni mtihani sana kuishi, achilia mbali wageni..hata wao kwa wao tu.
Lakini kuna baadhi ya Nchi hasa ulaya uwezi kupata changamoto... Hata ubaguzi ni mdogo, labda hasa wakubague kwa rangi, lakini si kwa udini... Nchi kama Ugiriki, denmark, Norway, uingereza zote zina misingi ya kidini, ila watu wanaishi fresh
 
nakurebeshia list, Maelezo utayakuta

1. UISLAMU
2.HINDUISM (Dini ya tatu kwa watu wengi)
3. ---
4. ---
5. Ukristo

HINDUISM

Naomba nikusahishe, Namba mbili weka dini ya wahindi inayoitwa Hinduism, wana miungu mingi lakini imekusanyika kwa dini hiomoja, Hao watu wana itikadi kali sana za kidini waweke namba mbili, waislam na wakristo wengi sana wanauwawa,kubakwa, kubaguliwa huko india, Kuna kampeni ya HINDUTIVA yenye lengo la kuifanya nchi iongozwe kwa misingi ya dini,

UISLAM

Tunarejea dini ya nchi za kiislam hawa ni shida, ni nchi zinazokandamiza dini nyingine na waislam wanaotoka nje.

Nchi kama Saudi Arabia, Afghanistan, Sudan, Iran, n.k. ukiwa muislam ukitangaza umebadili dini sheria zipo wazi UNAUWAWA, nchi kama Malaysia kubadili dini uende mahakama ya mashehe kuomba kibali cha kubadili dini, Utasubiri sana !! Lakini ukiwa mkristo ukibadili dini hutapata usumbufu wowote

Waislam wakijaa nchi flan ni ngumu sana dini nyingine kupata haki zao, Tusiende mbali sana angalia Zanzibar hawaruhusu mkristo aoe Muislam, Mfungo ukifika wakristo hawaruhusiwi kuendelea na ratiba zao za kula, ukikutwa unapigwa sana na kufungwa,

Nchi za kiislam nyingi zina vikundi vya kuua wasio waislam, Hapa Afrika kwa mfano Nigeria wakristo wanawindwa kama wanyama.
Sema wanyama mwitu!
 
Back
Top Bottom