SHIVA MAINA
JF-Expert Member
- Jan 9, 2015
- 293
- 42
Haiwezekani watu tumejaza form chuoni kuomba maeneo tunayoweza kupangiwa halafu ninyi mfanye tofauti kabisa na makadirio. kwa mfano mtu umetumia anuani ya dar, umeomba dar, moshi then unajikuta umepangiwa rukwa, hivi mashariki na magharibi wapi na wapi. mbona mikoa jirani na hiyo iko mingi. au zile form hazikua na maana? chakushangaza zaidi mtu mwingine ameomba upande huo huo wa rukwa una mleta mashariki tena kwa masomo hayo hayo. Hivi haya si ni makusudi kabisa. Na hii inasababisha matumizi ya kiasi kikubwa cha pesa za nauli zinazolipwa na serikali pamoja na kero za baadae za watu kubadilishana vituo kiholela bila kujali uhitaji wa wasomo husika. Naomba tatizo hili lijumuishwe kwenye marekebisho yanayoendelea ya walimu ngazi ya shahada na stashahada.
Mimi niliomba Mwanza, Geita na Morogoro nikitumia anwani ya Geita bt nimepangwa Mtwara