Orodha ya wasanii wenye majina makubwa lakini kiuhalisia hawana vipaji

Orodha ya wasanii wenye majina makubwa lakini kiuhalisia hawana vipaji

Tatizo ni pale unapong'ang'ania maoni yako yawe facts. Binafsi sijawahi kumpenda Sugu lakini kusema hana kipaji sio sahihi. Haiwezekani mtu akatoa wimbo ukahit nchi nzima na shoo akafanya halafu useme hana kipaji, kama sio kipaji ni nini?

Nyakati zao waliokua wanajaribu ni wengi lakini waliofanikiwa ni hao wachache mpaka tunawajadili hapa. Ni wangapi walitamani kufika level ya Mike Tee na hawakufika?
Ni Maajabu watu waimbe Nchi nzima tuwasikie na kuwaelewa halafu aseme hawana Kipaji sijui nini.... Tena Enzi ambazo hakukua na Digital platforms kama sasa.
 
Unajua ku criticize ni rahisi sana, maana hutumii nguvu nyingi.

Hisia zinaniambia ni kama vile hao wasanii uliowataja, wengi wao hukupata nafasi ya kuwasikiliza pindi wakiwa bado kwenye game. Lakini hata ukiwa sikiliza now as throw back, still kuna vibe fulani utalipata.

Sugu - Moto Chini
Temba - Nimekubali
Soggy - Kibanda Cha simu
Kala Pina- Mstari wa mbele
Mike T - Nakupenda.

Nimechagua baadhi ya nyimbo, Toka kwa baadhi ya wasanii uliotaja.

Moja kati ya ugomvi mkubwa ambao ulishawahi kutokea kati ya sisi watoto kipindi tunakua pale nyumbani, ni pale sister yetu aliporekodia igizo la radio, kwenye Kanda ya album ya Solo Thang, Kima Cha chini.

Mkuu, hujui ukisemacho. Penda unachopenda, ila usichokijua usikiongelee
Hahaha sister alizingua pakubwa sana, yaani KCC inarekodiwa akina Mama Muyaone! Haikiwa haki kabisa.
 
Unataka aweje ili umuone ana kipaji
Nikusaidie kwa mazingira ya zaman ilikua ni ngumu sana kutoa nyimbo na ukavuma ni tofauti na sasa hivi

Chujio la zaman ni gumu sana kama huna kipaji tofauti na sasa hivi mafanikio ya msanii yako revolve around kick
Hao uliowataja ni wachache kati ya wengi waliopambana kujulikana ki-music na wakashindwa ukweli ni kwamba watoto wa sahivi mnachukulia mambo kirahis sana kabisa unasimama unasema sugu au temba hana kipaji hivi unayajua mazingira ya 2000 kurudi nyuma huko
Ebu nikuulize una miaka mingapi
Mtoa mada ni moja ya wapumbavu wachache wanao jiona wajuaji,kwanza hawajui wasanii na sanaa yenyewe ilivyo,siku za nyuma mziki ulikuwa mgumu sana tofauti na sasa.

Mr 2 sio mtu wa kumkebehi hata kidogo katika tasinia ya muziki
 
Mtoa mada ni moja ya wapumbavu wachache wanao jiona wajuaji,kwanza hawajui wasanii na sanaa yenyewe ilivyo,siku za nyuma mziki ulikuwa mgumu sana tofauti na sasa.

Mr 2 sio mtu wa kumkebehi hata kidogo katika tasinia ya muziki
Oya jiheshimu , mpumbavu ni wewe unayejibu kimhemko
 
Kalapina,

Huyu jamaa mbali na kuwa na harakati nyingi akiwa pamoja na kundi lake la Kikosi cha mizinga .ukweli ni kwamba hana kipaji cha music. Alipata umaarufu coz ametoka kipindi wasanii ni wachache

Sugu

Huyu jamaa ana majina kibao kama Mr two, jongwe, too proud na sasa anajiita Taita licha ya kuwa na heshima kama moja ya waasisi wa music wa hiphop tanzania , ukweli ni kwamba hana kipaji cha music

Jaffarai

Huyu ni moja ya member wa wateule alitamba na wimbo wa niko bize .lakini hakuweza kudumu kwenye game kwa muda mrefu kutokana ukweli hana kipaji

Mchizi mox

Huyu pia ni member mwingine wa wateule ngoma zake zilizowahi kupata airtime ni mambo vp na chupa nyingine . lakini uwezo wake ni wa kawaida sana

Mike tee mnyalu

Huyu jamaa alipata airtime miaka ya zamani kwa ngoma zake lakini ukimskiliza ni wazi hana uwezo kabisa. Ni moja kati ya wasanii ambao huwa wanaandikiwa

Soggydog hunter

Huyu jamaa bora angebaki kwenye u presenter tuu huku kwenye music aliforce tuu hana uwezo kabisa ana ngoma nyingi ila iliyopenya ni kibanda cha simu pekee yake

Bou nako

Huyu alikua member wa N2N lakini tangu hakua na uwezo kabisa .nafkir wana walimbeba tuu kutokana na love .ila kwenye music jamaa hana kipaji

Fido vato

Huyu member wa vatokoko soldiers ni empy kabisa , analazimisha fan tuu ila ukweli anaujua kuwa hana uwezo wowote ule zaidi ya kujikuta gangstar

Kr mulah

Huyu ndio founder wa style ya kucheza Mapanga . ameanza sanaa muda mrefu sana lakini ukimskiliza utagundua jamaa hana uwezo wowote kwenye music kwa kifupi hana kipaji

Mh temba

Huyu ni member wa TMK wanaume family mwanzoni alibahatisha ngoma kama tatu zikaenda mjini, baadaye akaja kuungana na chege wakatoa hadi album..ila ukimfuatilia vizur jamaa hana
uwezo kabisa

Rich one

Huyu pia ni member wa TMK alitamba na ngoma moja aliyomshirikisha Juma nature inaitwa hatuna kitu.baada ya hapo hajawai kutoa hitsong tena, Jamaa anasifika kwa utapeli wa kuandaa show na wasanii fake huko mkoani afu anapiga hela

Dudu baya

Huyu jamaa aliotea ngoma kama tatu tuu ambazo zilimtambulisha vyema kwenye game .lakini alipata jina kwakua kipindi anatoka hapakua na upinzani mkali kama ilivyo sasa

Dark master

Huyu ndo muhasisi wa Chamber squard Nampa heshima kubwa sana kwa kuweza kuiweka dodoma kwenye ramani ya muziki , Lakini tukiongelea uwezo binafsi .jamaa anauwezo wa kawaida sana

John mjema,

The late John mjema alitamba na wimbo wa wachumba 30. Na ngoma zingine alizofanya kwenye kundi lao aliokua na kina the late steve 2k na buibui .lakini tukimzungumzia binafsi kimuziki jamaa hana kipaji cha muziki

Maujanja suppliers

Hawa jamaa nawakubali kwa harakati zao za street lakini kwenye music watupishe hawana vipaji .lakini wao wamekua wanalalamika wanabaniwa kitu ambacho sio ukweli

Kama unafuatilia music wa bongo fleva utakua unakubaliana na mimi hawa jamaa hawana talent za music kabisa
Umemuacha KI THE THE
 
Soggy Doggy hunter? Ameonewa, kibanda cha simu pamoja na story ya soggy ni ngoma zinazothibitisha ubora wake!

Kala Pina a.k.a Nabii koko? Hapana, mstari wa mbele ni moja kati ya ngoma kali za bongo hip hop za muda wote!

Mike T mnyalu? Inawezekana style yake haikukuvutia. Mike T wa "je utanipenda" na "hata kama Mnyalu" huwezi kumuweka kwenye kundi la watu wasio na vipaji.

Sugu? Pengine flow yake haikukuvutia, ila mafanikio yote aliyonayo, chimbuko lake ni mziki alioufanya. Sugu ndio mtu wa kwanza kuanzisha vita na mainstream media (chini ya Ruge) na akasurvive. Wa pili ni Lady Jaydee a.k.a Komando!

Jaffarai na Temba, sijawahi kuvutiwa na muziki wao kabisa. Ila wanazo hit songs, na mashabiki wengi waliwakubali. Siwezo kusema hawana vipaji.

DUDU BAYA a.k.a KONKI MASTA! Hapa mzee nimekosa cha kutetea. Mimi binafsi, mpaka leo sijaweza kuelewa kama dudu baya alikua anaimba au anarap. Maana kama ni kuimba, basi mwamba yuko na sauti mbaya. Na kama ni kurap, basi jamaa hajui nini maana ya vina.

Shilole a.k.a Shishi Trump. Kuna vitu vimempa umaarufu, sio muziki. Hata yeye anajua huku kwenye muziki anafosi tu. Kuna Shishi, Amber Lulu na Giggy money, wako kundi moja japo Giggy kidogo yuko na nafuu!

Nilitaka kusema kitu kuhusu AY, ila ngoja niishie hapa!
 
Yaani Unasema Soggy hana Hit Song baada ya Kibanda cha Simu?? Nilikaona Mwaka jana na Stori umeziimba wewe mpaka zikawa Hit song?? Bila Kuisahau KURWA NA DOTO nayo ilikua Hit song.

Sugu mpe Heshima yake, Ni kweli wakati wa sasa si Kama Zamani ila Heshima yake na Mashairi yake kamwe usiyabeze na kuyafananisha na hawa watoto wa 2000. Sugu Ni Msanii wa Hip Hop aliyethubutu kuikosoa serikali kuanzia enzi hajawa mbunge wala Hana matarajio ya kuwa mbunge, Kiufupi ni msanii aliyeiwakilisha mitaa (jamii) na matatizo yake.

Ni Msanii mwenye Album nyingi zilizosheheni Jumbe mbalimbali na Burudani. Kama

Ni Mimi (1995)

Ndani ya Bongo (1996)

Niite Mister II (1998)

Nje ya Bongo (1999)

Millennium (2000)

Muziki na Maisha (2001)

Itikadi (2002)

Sugu (2004)

Coming of Age-Ujio Wa Umri (2006)

VETO (2009)

Antivirus Mixtapes

Moja Kati ya wimbo wake niliokua nikiuimba sana na Kuupenda ni Mikononi mwa Polisi (1999) aliouimba kwa ajili ya Kijana mwanafunzi Michael Sikupya aliyeuawa na Polisi jijini Mbeya shuleni Iyunga Sekondari.

Kimsingi Sugu ni Legend, G.O.A.T.



Kuna Wengine umewaonea tu hapo, wale ambao walitoa Wimbo mmoja ukawa hit na hatukupata kuwasikia tena kama

°Rich One na Hatuna Kitu
°Fidovato huyu kwenye hii list sijui umemuweka wa nini hakupaswa kuwapo hapa kwa maana hakuna alichofanya katika muziki wa hip hop.
°Kr Murah Jibaba mziki mnene cd 700 njoo kichwa kichwa ule za uso.... Huyu mwamba hana chochote Kama Solo zaidi ya kazi za Kundi ulipaswa usimuweke hapa pia.


Mike Tee pia unamuonea, Ameacha game kwa heahima kubwa. Alitoa ma dude yaliyokua mikito ya Taifa wakati ule kama

1. Kama ft Jay moe
2. Nampenda nani ft Juma Nature
3. Ni beep baby
4. Je Utanipenda ft Mad Ice
5. Sivainogela
6. Hodi
7. Niacheni ft Banana Zoro
8. Sintobadilika ft Q Chief
Yaani ukisikiliza sintobadilika..utajua mtoa mada kazingua kwa mnyalu
 
Soggy Doggy hunter? Ameonewa, kibanda cha simu pamoja na story ya soggy ni ngoma zinazothibitisha ubora wake!

Kala Pina a.k.a Nabii koko? Hapana, mstari wa mbele ni moja kati ya ngoma kali za bongo hip hop za muda wote!

Mike T mnyalu? Inawezekana style yake haikukuvutia. Mike T wa "je utanipenda" na "hata kama Mnyalu" huwezi kumuweka kwenye kundi la watu wasio na vipaji.

Sugu? Pengine flow yake haikukuvutia, ila mafanikio yote aliyonayo, chimbuko lake ni mziki alioufanya. Sugu ndio mtu wa kwanza kuanzisha vita na mainstream media (chini ya Ruge) na akasurvive. Wa pili ni Lady Jaydee a.k.a Komando!

Jaffarai na Temba, sijawahi kuvutiwa na muziki wao kabisa. Ila wanazo hit songs, na mashabiki wengi waliwakubali. Siwezo kusema hawana vipaji.

DUDU BAYA a.k.a KONKI MASTA! Hapa mzee nimekosa cha kutetea. Mimi binafsi, mpaka leo sijaweza kuelewa kama dudu baya alikua anaimba au anarap. Maana kama ni kuimba, basi mwamba yuko na sauti mbaya. Na kama ni kurap, basi jamaa hajui nini maana ya vina.

Shilole a.k.a Shishi Trump. Kuna vitu vimempa umaarufu, sio muziki. Hata yeye anajua huku kwenye muziki anafosi tu. Kuna Shishi, Amber Lulu na Giggy money, wako kundi moja japo Giggy kidogo yuko na nafuu!

Nilitaka kusema kitu kuhusu AY, ila ngoja niishie hapa!
Kila mtu ana taste yake..hapo kwa AY na Mimi simkubali Sana.. lakini siwezi kusema Hana kibaji wakati anangoma nyingi zilivuma Sana..Kama Zigo..Leo..n.k
 
Jamaa kwa harakati za music tunampa heshima yake .lakini tukibaki kwenye ukweli ni kuwa hana kipaji cha music..
Ndo maana hajapewa heshima ya Godfather wa bongo fleva ila proffessor jay kapewa
Ukweli mchungu ,japo anapambana sana
 
Soggy Doggy hunter? Ameonewa, kibanda cha simu pamoja na story ya soggy ni ngoma zinazothibitisha ubora wake!

Kala Pina a.k.a Nabii koko? Hapana, mstari wa mbele ni moja kati ya ngoma kali za bongo hip hop za muda wote!

Mike T mnyalu? Inawezekana style yake haikukuvutia. Mike T wa "je utanipenda" na "hata kama Mnyalu" huwezi kumuweka kwenye kundi la watu wasio na vipaji.

Sugu? Pengine flow yake haikukuvutia, ila mafanikio yote aliyonayo, chimbuko lake ni mziki alioufanya. Sugu ndio mtu wa kwanza kuanzisha vita na mainstream media (chini ya Ruge) na akasurvive. Wa pili ni Lady Jaydee a.k.a Komando!

Jaffarai na Temba, sijawahi kuvutiwa na muziki wao kabisa. Ila wanazo hit songs, na mashabiki wengi waliwakubali. Siwezo kusema hawana vipaji.

DUDU BAYA a.k.a KONKI MASTA! Hapa mzee nimekosa cha kutetea. Mimi binafsi, mpaka leo sijaweza kuelewa kama dudu baya alikua anaimba au anarap. Maana kama ni kuimba, basi mwamba yuko na sauti mbaya. Na kama ni kurap, basi jamaa hajui nini maana ya vina.

Shilole a.k.a Shishi Trump. Kuna vitu vimempa umaarufu, sio muziki. Hata yeye anajua huku kwenye muziki anafosi tu. Kuna Shishi, Amber Lulu na Giggy money, wako kundi moja japo Giggy kidogo yuko na nafuu!

Nilitaka kusema kitu kuhusu AY, ila ngoja niishie hapa!
Mkuu kuhusu AY hebu funguka kidogo
 
1.Baba levo(Anapiga kelele nyingi)
2.Niki wa pili na Kaka yake johmakin(Hawa hawana kipaji ila wanabebwa kwakua wana connection kwenye kundi lao la weusi anaejua ni G warawara tu )
3.Darasa ( huyu aliotea maisha na mziki Basi Hadi leo anaimba kwa staili ileile ni kama anarudia nyimbo moja kila siku)
4.Best naso
5.Abdu kiba
6.Wakazi
7.Hbaba
Nimecheka huyo namba 3 [emoji16] [emoji16]
 
Back
Top Bottom