Padre afariki akiendesha Ibada ya Mazishi Mtwara

Padre afariki akiendesha Ibada ya Mazishi Mtwara

"Mmoja wa madaktari wa Hosptali hiyo ya Ndanda ambaye hakupenda jina lake litajwe kwenye vyombo vya Habari (Dr Venance Chingwile) amethibitisha kupokelewa mwili wa Mchungaji Milanzi"
Kazi kweli kweli, yaani Dr. Venance Chingwile hakupenda Jina lake litajwe kwenye vyombo vya habari!
 
Kombora hilo dadekii

Tatizo hawa watawa wakishapangiwa majukumu ya kiroho ktk kanda husika

Huwa wanajisahau sana

Waruhusiwe kuoa tu
 
Wengi wameshangaa lakini nadhani ni kwamba hilo si jina lake sahihi huyo dokta, ndio wakalieka kwa mabano ila amesahau kuandika kwamba sio jina lake
 
"Mmoja wa madaktari wa Hosptali hiyo ya Ndanda ambaye hakupenda jina lake litajwe kwenye vyombo vya Habari (Dr Venance Chingwile) amethibitisha kupokelewa mwili wa Mchungaji Milanzi"
😂😂😂😂
 
Kama kafia makaburini wangemzika tu hapo hapo yaishe. Mawazo ya pombe
 
Wengi wameshangaa lakini nadhani ni kwamba hilo si jina lake sahihi huyo dokta, ndio wakalieka kwa mabano ila amesahau kuandika kwamba sio jina lake
Sasa kuna haja gani ya kuandika jina ambalo sio sahihi?

Kwani angesema tu hakutaka jina lake litajwe kuna shida gani?
 
Makamu wa Askofu wa Jimbo katoliki la Mtwara amekanusha hiyo habari.
"Ni upuuzi,upotoshaji na kukosa weledi. Mpaka sasa na tarehe tajwa hakuna Padri wa Jimbo la Mtwara aliyefariki. Aidha hakuna Padri mwenye jina la Laurence Millanzi katika jimbo la Mtwara.Ni taarifa inayomfurahisha mwandishi mwenyewe na aibu yake. Lakini pia ni chukizo kwa wapendao ukweli.
Vicar General, Mtwara."
 
Mchungaji wa Kanisa Katoliki kijiji cha Liputu, Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara, Laurence Milanzi amefariki Dunia maeneo ya makaburini alipokuwa akishiriki mazishi ya mwanakijiji mwenzao aitwae Daudi Veno

Untitled-3_0.jpg

Mashuhuda wa tukio hilo wanasema mchingaji huyo alianguka ghafla wakati akiwaasa watu kutosusia misiba kwa mtu asiyehudhuria Nyumba za Ibada.

Kifo cha Mchungaji huyo kimetokea kwenye Kijiji hicho Julai 19 mwaka huu, saa 5:00 asubuhi kwenye eneo linalotumika mahususi kwa mazishi ya watu wanaofariki dunia.

Mwili wa Mchungaji huyo umehifadhiwa katika Hosptali ya Mission ya Ndanda, Wilaya ya Masasi ukisubiri taratibu za mazishi yanayotarajiwa kufanyika Kijiji hapo, baada ya kukamilika kwa taratibu zote.

Baadhi ya mashuhuda walioudhuria mazishi ya Daudi Veno, wameeleza kwamba, Mchungaji Milanzi amekutwa na umauti huo, alipokuwa anatoa sala na kuwasihi viongozi wenzake wa Dini kuacha tabia ya kutohudhuria mazishi kwa Binadamu mwenzao asiyeshiriki masuala ya Ibada.

Mchungaji Milanzi alisema kitendo cha kususa kumuombea marehemu kwa kuwa hakuwa anashiriki kwenye Nyumba za Ibada, Kanisani na misikitini ni kwenda kinyume na maagizo ya mwenyezi Mungu alivyoagiza mtu anapofariki ni muhimu akazikwa na sio kumuacha kwani uharibu hali ya hewa kutokana na harufu mbaya kutoka kwake.

“Baada ya kueleza hayo, tukamuona mwenzetu akidondoka chini kisha kupoteza fahamu” Walieleza Joseph Michael na Samwel Chindonga. Aidha,mashuhuda hao wamesema kwamba baada ya Mchungaji huyo kudondoka chini walimchukuwa na kumkimbiza Hosptali ya Ndanda na kuelezwa na madaktari kuwa alishafariki

Mmoja wa madaktari wa Hosptali hiyo ya Ndanda ambaye hakupenda jina lake litajwe kwenye vyombo vya Habari (Dr Venance Chingwile) amethibitisha kupokelewa mwili wa Mchungaji Milanzi, na kuhifadhiwa chumba cha maiti (Mochwari) ukisubiri taratibu za mazishi.

Chanzo: EATV
Ni Mchungaji au Padre mbn haieleweki?
 
Inasadikika kuwa huyu mchungaji aliliponda Kanisa kwa kukataa kuendesha ibada ya kumzika marehemu kwani alikuwa hashiriki kikamilifu; so katikati ya ibada ya mazishi, huyu mchungaji yakamkuta yaliyomkuta.
 
Mchungaji wa Kanisa Katoliki kijiji cha Liputu, Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara, Laurence Milanzi amefariki Dunia maeneo ya makaburini alipokuwa akishiriki mazishi ya mwanakijiji mwenzao aitwae Daudi Veno

Untitled-3_0.jpg

Mashuhuda wa tukio hilo wanasema mchingaji huyo alianguka ghafla wakati akiwaasa watu kutosusia misiba kwa mtu asiyehudhuria Nyumba za Ibada.

Kifo cha Mchungaji huyo kimetokea kwenye Kijiji hicho Julai 19 mwaka huu, saa 5:00 asubuhi kwenye eneo linalotumika mahususi kwa mazishi ya watu wanaofariki dunia.

Mwili wa Mchungaji huyo umehifadhiwa katika Hosptali ya Mission ya Ndanda, Wilaya ya Masasi ukisubiri taratibu za mazishi yanayotarajiwa kufanyika Kijiji hapo, baada ya kukamilika kwa taratibu zote.

Baadhi ya mashuhuda walioudhuria mazishi ya Daudi Veno, wameeleza kwamba, Mchungaji Milanzi amekutwa na umauti huo, alipokuwa anatoa sala na kuwasihi viongozi wenzake wa Dini kuacha tabia ya kutohudhuria mazishi kwa Binadamu mwenzao asiyeshiriki masuala ya Ibada.

Mchungaji Milanzi alisema kitendo cha kususa kumuombea marehemu kwa kuwa hakuwa anashiriki kwenye Nyumba za Ibada, Kanisani na misikitini ni kwenda kinyume na maagizo ya mwenyezi Mungu alivyoagiza mtu anapofariki ni muhimu akazikwa na sio kumuacha kwani uharibu hali ya hewa kutokana na harufu mbaya kutoka kwake.

“Baada ya kueleza hayo, tukamuona mwenzetu akidondoka chini kisha kupoteza fahamu” Walieleza Joseph Michael na Samwel Chindonga. Aidha,mashuhuda hao wamesema kwamba baada ya Mchungaji huyo kudondoka chini walimchukuwa na kumkimbiza Hosptali ya Ndanda na kuelezwa na madaktari kuwa alishafariki

Mmoja wa madaktari wa Hosptali hiyo ya Ndanda ambaye hakupenda jina lake litajwe kwenye vyombo vya Habari (Dr Venance Chingwile) amethibitisha kupokelewa mwili wa Mchungaji Milanzi, na kuhifadhiwa chumba cha maiti (Mochwari) ukisubiri taratibu za mazishi.

Chanzo: EATV
Hii taarifa mbona ina mkanganyiko! Maana Kanisa Katoliki lina Mapadre/Makasisi! Na siyo Wachungaji.

Lakini pia makao ya Padre, au utambulisho wake ni Parokiani! Padre fulani wa Parokia ya...., Jimbo Katoliki la....!! Na wala siyo Kijiji cha.....!

Sasa huyu Mchungaji wa Kanisa Katoliki, Kijiji cha.......! Mbona taarifa inachanganya.

Anyway, Rest in peace Mchungaji wa Kanisa Katoliki Kijiji cha Liputu huko Mtwara.
 
Back
Top Bottom