TANZIA Padre Paul Ignas Shewiyo wa Kanisa la Msimbazi afariki Dunia

TANZIA Padre Paul Ignas Shewiyo wa Kanisa la Msimbazi afariki Dunia

Wiki iliyopita tulimzika Kaka yake Stephen Ignas Shewiyo alikua mfanyakazi wa TCAA Kwa corona tena alifariki KCMC. Leo tena Paul ameenda?! Halafu kuna mashetani yanasema hakuna Corona.
Kwa hiyo korona imekuwa busy na familia hii
 
Kipindi hiki kila kifo ni corona. Magonjwa nyemelezi, kansa, stroke, na mengineyo yanaonesha sasa yameacha kuua watu.
Nkupe maarifa kidogo tu, ukiwa na hayo magonjwa na ukakutana na bwana Corona lazima usepe. Wakati zamani ungeendelea kudunda kwa muda mrefu tu. Ukipata malaria na kama uko na ukimwi wajua chance ya kufa ni kubwa sana, je ukifa unakuwa umekufa kwa ukimwi au malaria?
 
Corona corona, unapotutembelea usisite kupiga hodi pale Magogoni ya Dodoma, ukifanya hivyo utakuwa umetenda haki
 
AJABU SANA NAOMBA KUJUZWA HIVI MTU YEYOTE ANAYEFARIKI KATIKA NYAKATI HIZI CHANZO CHA KIFO CHAKE HUWA NI KORONA NAOMBA TUJUZANE HILI KWANZA LINANITATIZA SANA
Kuna kwown cases na ni nyingi kuliko magonjwa mengine. Hii ya leo ni confirmed na yuko hospital wiki plus or so. Hivyo siyo kila jambo ni kupinga. Aliyeleta hii allert ni ndugu yake wa damu. Inauma unapoteza ndugu wawili wa damu within a week kwa ugonjwa unaofichwa na kubadilisha majina. Sad Tanzanians.
 
Huyo anayedanganya watanzania kuwa hakuna Corona bali ni Pneumonia ninaomba hiyo Pneumonia impate yeye na kizazi chake na asibakie hata mmoja. Leo hii kwenye makundi niliyopo ni msiba mingi na yote ni Pneumonia maana wanaogopa kutaja Corona. Mtu kama kwako hujapigwa na Corona bado kaa kimya. Corona ipo kwa Wingi mno. Wanaugua wanapona na wengine wanakufa. Tusimkebehi Mungu kwa maneno ya uongo ya kutunga. Tanzania siyo Makao Mkuu ya Mungu.
nami naomba iwapige kweli kweli akina Jiwe na Gwajima wanaosema hakuna corona, wafe wke zao, watoto zao halafu warudi watwambie hakuna corona
 
Kwa hiyo korona imekuwa busy na familia hii
Ohhh Mungu wangu. Ninafikiri wewe utakuwa ni kisiwa kisichofikika. Hivi unawezaje kuandika hivi wakati wenzako wanahuzunika. Wapo wengi wamefariki bila kuletwa humu maana siyo maarufu au public figure. Sad indeed.

Wanasema marehemu tu ndiye asiyeweza kuamka na kupata ya DUNIANI. Ila tulio hai tujiangalie maana siku zipo, wiki zipo, miezi ipo na miaka ipo. Waliougua Corona hawakujua kama itawapata. Waliokufa kwa Corona hawakujua kama watakufa. Kesho yetu hatuijui.
 
Wiki iliyopita tulimzika Kaka yake Stephen Ignas Shewiyo alikua mfanyakazi wa TCAA Kwa corona tena alifariki KCMC. Leo tena Paul ameenda?! Halafu kuna mashetani yanasema hakuna Corona.
Exactly, nimewasiliana na ndugu yake muda si mrefu analia tu.Ni Corona ni corona.

Tz is the HELL
 
Kwanini korona imeshamiri sasa kuliko kipindi cha nyuma. Najiuliza sana lakini sipati jibu. Na kitu gani ilipunguza wakati mtindo wa maisha ya watanzania haujabadilika . Nina maswali mengi ambayo nakosa majibu. Poleni sana kwa wafiwa wote . Na Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema
 
Kwanini korona imeshamiri sasa kuliko kipindi cha nyuma. Najiuliza sana lakini sipati jibu. Na kitu gani ilipunguza wakati mtindo wa maisha ya watanzania haujabadilika . Nina maswali mengi ambayo nakosa majibu. Poleni sana kwa wafiwa wote . Na Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema
Second wave imekuja kitofauti sana. Nahisi ni kali sana na dalali zake hazijitokezi haraka. Zikijitokeza means imeshakutafuna. Hivyo ukiwa na kinga dunia basi inakuzidia. Ndiyo new strain hiyo ni mbaya pia na Tz imetajwa kama nchi mmojawapo yenye new strain na tuko kiwango cha 4 ambacho ni kibaya. Mungu tusaidie.
 
Kwanini korona imeshamiri sasa kuliko kipindi cha nyuma. Najiuliza sana lakini sipati jibu. Na kitu gani ilipunguza wakati mtindo wa maisha ya watanzania haujabadilika . Nina maswali mengi ambayo nakosa majibu. Poleni sana kwa wafiwa wote . Na Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema
Hujasikia kuna wimbi la pili(second wave) la korona duniani?
 
Wiki iliyopita tulimzika Kaka yake Stephen Ignas Shewiyo alikua mfanyakazi wa TCAA Kwa corona tena alifariki KCMC. Leo tena Paul ameenda?! Halafu kuna mashetani yanasema hakuna Corona.
Pole Mkuu, nashauri wale wanaosema hakuna bora wakae kimya sababu hawawezi / hawajapima kila mtanzania..., kwa kufanya hivyo inakuwa dhihaka kwa wanaofiwa..., ingawa technically na wewe watakwambia uliwapima ? , Nadhani hizo sintofahamu zimeletwa na hizi ficha ficha, jambo ambalo kwa sasa hatuaminiani na itapelekea kuacha kuwaamini hata wataalamu....
 
Poleni kwa msiba,
Walale salama marehemu wote, Jumanne tumemuaga Padre Paroko Benedict wa parokia ST MARTIN WA PORES
Tunamshukuru Mungu kwaajili ya zawadi ya uhai wao hapa duniani
Atleast leao umekubali kwamba kuna CORONA na mwenyekiti wa ccm anawadanganya watanzania.
 
Amehusika sana kwenye ujenzi wa kanisa la Nyasubi kahama
Mungu amlaze pema peponi
 
UKITENDA MEMA DUNIANI UTAKUMBUKWA DAIMA. SOMENI WASIFU WA MAREHEMU KAKA NA NDUGU YETU PADRE PAUL IGNAS SHEWIYO KAMA NILIVYOUPOKEA KUTOKA KWA KIONGOZI WA PAROKIA MOJA ALIYOHUDUMU DAR ES SALAAM.

PUMZIKA KWA AMANI KAKA.ULIKUWA MMOJA WA WANASEMINARI WANYOOFU SANA KIPINDI HICHO UKIWA SEMINARI.
***********^^^^^^^^^^*****

Bado natafakari, nayastaajabu matendo Makuu na ya ajabu ya Mwenyezi MUNGU! 🙆🏾‍♂

Ni kama siamini ninachokisoma au kusikia. Ni kama naota mchana..... lakini la hasha, ni kweli, naona Baba Shewio hatunae tena! 😭

Pole sana Baba Paroko, Baba Paroko Msaidizi, Waumini wote na zaidi kwa Kanisa kwa ujumla! 🙏🏾

Nimemfahamu Baba Shewio tangu huko Moshi muda mrefu sasa, hakika nimemfahamu kama Baba mwenye mapenzi mema sana kwa Kanisa na jamii ya Waumini wote! Tumepata pigo na pengo ambalo MUNGU Baba Mwenyezi pekee ajua siri na mpango wake.

Baba Shewio alikuwa Mcheshi, mwenye furaha na tabasamu toka rohoni! Alijaa upendo wa dhati, alipenda Yatima na wenye shida! Aliwakumbuka walemavu na wenye uhitaji...na hakika, alisikia raha na faraja alipoweza kutenda jambo la huruma kwa wahitaji! 🙏🏾

Leo hatunae, ametangulia. Tuhuzunike lakini tufurahi kwa bahati ya kupata fursa ya kuishi na Baba Shewio. Kila mmoja wetu amuenzi Baba Shewio kwa kuishi "Upendo" na kuyaendeleza yale mambo makuu aliyoyaishi hapa Duniani! 🙏🏾

Baba Shewio, natazama picha zako, nakumbuka maneno yako, nakukumbuka sana! Natokwa machozi, machozi ya simanzi ya kutuacha...lakini pia ya furaha kwa matumaini makubwa kuwa umeenda kwa Baba Mbinguni! 🙏🏾

Buriani Baba Shewio, hakika kuishi kwako ni KRISTO na hata kifo chako naamini ni faida kwako, Starehe kwa Amani Baba Shewio! Nakumbuka jinsi ulivyoendesha Misa ya Marehemu Baba yako Mzazi na jinsi ulivyokuwa shupavu, mwenye furaha na Imani.....na hasa maneno yako ya faraja na Imani. Ulimshika Kristo haswa, pumzika! 🙏🏾

Umekuwa Jemedari mnyenyekevu, Askari mpole wa YESU,.... Rubani mwenye Hekima kwetu Waumini Wasafiri hapa Duniani, Baba aliejaa Upendo kwa Kanisa lote bila ubaguzi na Mchungaji Mwema uliyekuwa kimbilio la wengi, hakika tutakukumbuka sana! 🙏🏾

Kwaheri Baba Shewio, japo umezimika ghafra kama Mshumaa barazani! Safari yako ni somo kwetu, naam, kwetu tuliosalia.... tuwe tayari, tuishi kwa Upendo na kumtumaini Bwana, kwani hatujui siku wa saa!

Tulikupenda Baba Shewio, tunakupenda, na tutakuenzi daima! Ukiweza, tuombee Baba Shewio, tuombee kama ulivyofanya hapa Duniani. Nasi tutakuombea mara kwa mara! Wana Upanga, tutakukumbuka! 🙏🏾

Starehe kwa amani Baba Shewio, pumzika Baba Shewio! Vita umevipigana, mwendo umeumaliza na hakika, Imani umeishika! Mwanga wa Milele ukuangazie, upumzike kwa Amani, Ameeen! 🙏🏾🙏🏾🙏🏾😔😭😔
 
Back
Top Bottom