Zogwale
JF-Expert Member
- Jul 10, 2008
- 15,295
- 10,928
TANZIA.
Shirika la Watawa wa Mtakatifu Benedicto Abasia ya Ndanda, iliyopo Jimbo katoliki Mtwara, wanatangaza kifo cha Baba Abate wa Abasia ya Ndanda Padre Plasidius Mtunguja OSB, kilichotokea alfajiri ya tarehe 02/03/2021, katika hospitali ya Rufaa Ndanda- Masasi.
Mazishi yatafanyika Jumanne ya Tarehe 9/3/2021 saa tano kamili asubuhi, huko Abasia ya Ndanda.
Habari ziwafikie, watawa wote wa shirika la Mtakatifu Benedicto ndani na nje ya nchi, mapadre, Maskofu, watawa wakike na wakiume, waamini Walei, ndugu jamaa na Marafiki na wote wenye mapenzi mema.
Raha ya Milele umpe ee Bwana, na mwanga wa milele umuangazie; apumzike kwa amani. Amina.
Shirika la Watawa wa Mtakatifu Benedicto Abasia ya Ndanda, iliyopo Jimbo katoliki Mtwara, wanatangaza kifo cha Baba Abate wa Abasia ya Ndanda Padre Plasidius Mtunguja OSB, kilichotokea alfajiri ya tarehe 02/03/2021, katika hospitali ya Rufaa Ndanda- Masasi.
Mazishi yatafanyika Jumanne ya Tarehe 9/3/2021 saa tano kamili asubuhi, huko Abasia ya Ndanda.
Habari ziwafikie, watawa wote wa shirika la Mtakatifu Benedicto ndani na nje ya nchi, mapadre, Maskofu, watawa wakike na wakiume, waamini Walei, ndugu jamaa na Marafiki na wote wenye mapenzi mema.
Raha ya Milele umpe ee Bwana, na mwanga wa milele umuangazie; apumzike kwa amani. Amina.