Biblia inasema wazi huwezi kutumikia MABWANA wawili
Daah, Kati ya vitabu ambavyo, huwenda waliowahi kuvielewa vyema Kwa asilimia zote ni hao hao walioviandika,
Na hiki mkuu, ulichokoti kutoka Kwa Biblia, huwenda ndicho shetani anakitumia ili kuhakikisha mamlaka zote za serikali zinaongozwa na watu wake, na ndiyo maana Dunia inashuhudia mauwaji kutoka kila Kona yakisababishwa na viongozi pandikizi wa shetani
Na Shetani kazi yake ni kuangamiza na kufanya mauwaji kama Dunia inavyoshuhudia kuwa na viongozi katili wasiojali ubinadamu
Mungu Wakati anakutana Ibrahimu, moja ya Ahadi aliyompa, alisema, na wafalme (watawala) watatoka kwako!
Mkuu, Hilo Andiko ulilonukuu, shetani amelitumia vya kutosha ili kukandamiza watu na kuwafanya mateka wake
Kwanza, ieleweke kwamba, kila mtu Kwa kazi anayoifanya, iwe ya kwake kabisa, hata kazi ya ubunge, Uraisi n.k zote ni utumishi wa kumtumikia Mungu, kazi yako halali haiwezi kuitwa ni kazi ya Kishetani, kazi zote halali zinamwakilisha Mungu, iweje ukiwa kazini kwako kugeuke na kuwa sehemu ya bwana mwingine? Ila ukiwa kanisani au msikitini tu ndio kuwe Kwa Bwana muumbaji? Ni Sawa na kusema, utakatifu utaufanya ukiwa maeneo ya Ibada pekee
Binadamu wote, ni mawakili wa Mungu, haijalishi unafanya kazi gani, siku ya mwisho hiyo kazi yako ndio itakuwa sababu ya kukuingiza peponi au motoni
Tafsiri ya Neno Hilo, ni mtu kuwa mtumishi wa Mungu na Wakati huohuo anamtumikia shetani,
Kazi ya ubunge,Uraisi na biashara halali n.k sio kazi za shetani buana!
Watu wa Mungu, ombeni nafasi za Uongozi, kwani hata nafasi hizo zinamwakilisha Mungu
Watumishi wa Mungu pekee wenye hofu ya Mungu wakiwa ndio viongozi wa juu, Dunia nzima itakuwa sehemu salama na Amani