Padri Kitima: Bunge letu linafikiri kichama. Upeo wa kuchambua masuala ya nchi yetu umeshuka

Padri Kitima: Bunge letu linafikiri kichama. Upeo wa kuchambua masuala ya nchi yetu umeshuka

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Katibu Mkuu wa TEC, Padri Dkt. Kitima akiwa kwenye mahojiano na The Chanzo amesema kuwa ule uwezo wa kuchambua masuala ya kitaifa umeshuka.

' Ule uchambuzi, kuchambua masuala, kupembua wa watu wa kawaida umeshuka. Wewe angalia sasa hivi watu wana miaka saba hatujawaongelea juu ya haki zao za msingi za kujitawala.

Hatujawaongelea uzuri wa kuwa na kitu kinachoitwa Katiba ambayo ni sheria mama ambayo kila mtu anapaswa kuwajibishwa nayo.

Hata ungewaambia watu kuwa, sasa jamani tutakuwa tuna vitabu viwili tu vinavyotawala nchi hii Quran na Biblia, ambavyo vimewekwa na muumba wenu, bado Watanzania wanaweza wakavichoma moto wakaendelea na mambo yao wanayoyataka.

Hata ukiwa na Katiba, utashi na kusudio, dhamiri na makusudio maalum ya kila aliyeko madarakani kusema hili na lile litawale, kama hiyi haipo hatuwezi kwenda.

Kwa hiyo, mimi nakubali sheria mama ni ya msingi lakini mwisho wa siku hebu angalia uhalisia uliopo. Bunge linafikiri kichama, Bunge letu la sasa ukuu wa Bunge haupo.

Umeona spika ametishwa kidogo amejiuzulu. Uchaguzi unafanya wa kumchagua mtu mmoja bungeni, eti mtu amepata kura zote za watu sijui 300 na ngapi

Hata Nyerere alikuwa hapati zote, ambaye tunaamini kweli ni Baba wa Taifa.

Unaona kabisa kwamba ule utashi wa kuwa na utawala wa sheria nchi hii haujadhamiriwa na walioko madarakani.

 
Hapa suala la kujiuliza ni kwanini uwezo ushuke wakati kila mwaka wanaongezeka wahitimu wa vyuo vikuu?

Ni elimu yetu ndio mbovu? au ukosefu wa ajira unaowakuta wahitimu mtaani ndio chanzo kwao kugeuka chawa?

Mimi naona mchanganyiko wa hayo maswali mawili ndio unaleta majibu, kwani hata kama mhitimu akimaliza chuo na ufaulu mzuri, lakini akija kukutana na ukosefu wa ajira mtaani, hapo lazima aiweke elimu yake pembeni ili apate nafasi ya kulijaza tumbo lake.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Padre anayetetea mashoga hawezi kuipenda serikali inayopinga ushoga.
 
Hii inapatikana katika kitabu kipi cha Biblia? Wameshamaliza kupambana na mambo ya aibu kama mapenzi ya jinsia moja?
Chawa kama chawa naona haya maneno yamekukurupusha kutoka shimoni....
Jifunze kutafuta riziki sio kupamba watu ili upate kitonga..utapakatwa
 
Katibu Mkuu wa TEC, Padri Dkt. Kitima akiwa kwenye mahojiano na The Chanzo amesema kuwa ule uwezo wa kuchambua masuala ya kitaifa umeshuka.

' Ule uchambuzi, kuchambua masuala, kupembua wa watu wa kawaida umeshuka. Wewe angalia sasa hivi watu wana miaka saba hatujawaongelea juu ya haki zao za msingi za kujitawala.

Hatujawaongelea uzuri wa kuwa na kitu kinachoitwa Katiba ambayo ni sheria mama ambayo kila mtu anapaswa kuwajibishwa nayo.

Hata ungewaambia watu kuwa, sasa jamani tutakuwa tuna vitabu viwili tu vinavyotawala nchi hii Quran na Biblia, ambavyo vimewekwa na muumba wenu, bado Watanzania wanaweza wakavichoma moto wakaendelea na mambo yao wanayoyataka.

Hata ukiwa na Katiba, utashi na kusudio, dhamiri na makusudio maalum ya kila aliyeko madarakani kusema hili na lile litawale, kama hiyi haipo hatuwezi kwenda.

Kwa hiyo, mimi nakubali sheria mama ni ya msingi lakini mwisho wa siku hebu angalia uhalisia uliopo. Bunge linafikiri kichama, Bunge letu la sasa ukuu wa Bunge haupo.

Umeona spika ametishwa kidogo amejiuzulu. Uchaguzi unafanya wa kumchagua mtu mmoja bungeni, eti mtu amepata kura zote za watu sijui 300 na ngapi

Hata Nyerere alikuwa hapati zote, ambaye tunaamini kweli ni Baba wa Taifa.

Unaona kabisa kwamba ule utashi wa kuwa na utawala wa sheria nchi hii haujadhamiriwa na walioko madarakani.


Rais mwenyewe anasema eti KATIBA ni kijitabu tu!! Ina maana, kwake yeye katiba siyo mwongozo wa majukumu yake.

Huyu ni mtu aliyeapa kuilinda katiba. Yaani hajui hata heshima aliyo nayo ni kutokana na katiba. Bila katiba, Samia siyo Rais, na mama tu ambaye anaweza hata kutemewa mate na mtu yeyote asiye na heshima kwa wenzake, na yeye akaishia kulalamika tu maana bila katiba, hata mahakama zitakuwa ni nyumba tu za kupigia zogo.

Kwa kauli ile tu, ingekuwa ni nchi ya watu smart, Samia leo hii asingekuwa Rais, maana amedharau na kukiuka kiapo chake.
 
Ndioo imepita hiyo hata bila ya kuisoma na kuielewa.
Ni ndiooo na nderemo.
 
Hapa suala la kujiuliza ni kwanini uwezo ushuke wakati kila mwaka wanaongezeka wahitimu wa vyuo vikuu?

Ni elimu yetu ndio mbovu? au ukosefu wa ajira unaowakuta wahitimu mtaani ndio chanzo kwao kugeuka chawa?

Mimi naona mchanganyiko wa hayo maswali mawili ndio unaleta majibu, kwani hata kama mhitimu akimaliza chuo na ufaulu mzuri, lakini akija kukutana na ukosefu wa ajira mtaani, hapo lazima aiweke elimu yake pembeni ili apate nafasi ya kulijaza tumbo lake.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Ndugu yangu fikiria ile miaka ya nyuma. Wanachuo wakisema wanamutana Nkrumah Hall kujadili mstakabali wa Taifa, serikali yote ofisi hazikaliki. Kila mmoja atataka kujua watajadili nini, na maazimio ni yapi.

Leo hii hata hao vijana wenyewe wanaosoma vyuo vikuu ni tepetepe, wala hata hawajui wana wajibu wowote kwa Taifa. Wakimaliza vyuo ndio hao wanageuka kuwa akina Mwamshamba. Watu ambao wanaishi bila ubongo wa kutafakari, wanahangaika kuimba na kusifia ili angalao matumbo yao yapate chochote.

Kwa kweli kwa sasa, na kwa aina ya vijana wa sasa na hao waliopo vyuoni, hili Taifa limegeuka kuwa Taifa la manunda.
 
Hili ni hi jibu la mpumbavu aliyekubuhu. Huwezi shambulia Mtu aliyetoa maoni kama wewe si Zuzu.
Huyo Muju4 ndio kipimo halisi cha watu punguani wa miaka hii. Ukiwa na majitu kama hayo, halafu utegemee maendeleo kwenye nchi?
 
Back
Top Bottom