Pale Bungeni simuoni Mbunge wa kuichambua ripoti ya CAG baada ya kukosekana Zitto Kabwe na wabunge wa CHADEMA

Pale Bungeni simuoni Mbunge wa kuichambua ripoti ya CAG baada ya kukosekana Zitto Kabwe na wabunge wa CHADEMA

Tukiweka itikadi pembeni, kiukweli pale bungeni simuoni mtu mwenye uwezo wa kuichambua ripoti ya CAG kama walivyokuwa Zitto Kabwe, J J Mnyika, James Mbatia na Tundu Lissu.

Kuwa mwanasiasa mzuri ni jambo moja lakini kuwa mwanasiasa " mahiri" ni jambo lingine kabisa.

Hao niliowataja unapofika wakati wa uchambuzi wa maswala ya kitaalamu iwe uchumi, sheria au fedha huwa na udadisi wa kitaaluma siyo kishabiki.

Ripoti ya CAG iliyowasilishwa kwa mh Rais Samia leo inahitaji hoja nyingi za kibobezi/ kidadisi lakini sidhani kama akina Babu Tale na Nusrat Henje wana viwango hivyo.

Itoshe tu kusema wabunge wengi wa sasa wana uwezo mdogo na ujasiri hafifu wa kujenga hoja.


Dogo naona Umebadili GIA ANGANI>
 
Tukiweka itikadi pembeni, kiukweli pale bungeni simuoni mtu mwenye uwezo wa kuichambua ripoti ya CAG kama walivyokuwa Zitto Kabwe, J J Mnyika, James Mbatia na Tundu Lissu.

Kuwa mwanasiasa mzuri ni jambo moja lakini kuwa mwanasiasa " mahiri" ni jambo lingine kabisa.

Hao niliowataja unapofika wakati wa uchambuzi wa maswala ya kitaalamu iwe uchumi, sheria au fedha huwa na udadisi wa kitaaluma siyo kishabiki.

Ripoti ya CAG iliyowasilishwa kwa mh Rais Samia leo inahitaji hoja nyingi za kibobezi/ kidadisi lakini sidhani kama akina Babu Tale na Nusrat Henje wana viwango hivyo.

Itoshe tu kusema wabunge wengi wa sasa wana uwezo mdogo na ujasiri hafifu wa kujenga hoja.
Wewe na wenzako si ndo mlikua mnawapigia chapuo wapate Sasa tuko kwenye matokeo ya ushabiki wenu

Ndo Kwanza mwaka wa kwanza bado 4 ambayo hsijaguswa kabisa


Anyway tutajua tu rangi zenu harisi kwa Sasa [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hiyo ripoti ya CAG itachambuliwa vizuri sana Hamphrey Polepole
 
Wajameni yupo Humprey Polepole, aliwahi kuchambua 'vizuri' sana zile Trillion 2.4 zilivyotumika.
😂 😂 😂 tena with DIAGRAMS..
Nimecheekaa daaah!
Ila mwendazake alichotufanyia ni kuonyesha jinsi gani katiba ni mbovu.

Everyday is Saturday................................😎
 
Johnthebaptist hastahili hata kulinganishwa na jingalao, wakudadavua, bia yetu na USSR. John hata akiamua kuandika ujinga, unaona kabisa kaamua kujifanya mjinga. Lakini hao wengine unaona kabisa kuwa ni wajinga na wanafiki.
Hahhaha ujinga haujifichi
 
Tukiweka itikadi pembeni, kiukweli pale bungeni simuoni mtu mwenye uwezo wa kuichambua ripoti ya CAG kama walivyokuwa Zitto Kabwe, J J Mnyika, James Mbatia na Tundu Lissu.

Kuwa mwanasiasa mzuri ni jambo moja lakini kuwa mwanasiasa " mahiri" ni jambo lingine kabisa.

Hao niliowataja unapofika wakati wa uchambuzi wa maswala ya kitaalamu iwe uchumi, sheria au fedha huwa na udadisi wa kitaaluma siyo kishabiki.

Ripoti ya CAG iliyowasilishwa kwa mh Rais Samia leo inahitaji hoja nyingi za kibobezi/ kidadisi lakini sidhani kama akina Babu Tale na Nusrat Henje wana viwango hivyo.

Itoshe tu kusema wabunge wengi wa sasa wana uwezo mdogo na ujasiri hafifu wa kujenga hoja.
Kwa mara ya kwanza umeandika kama Mtanzania mzalendo kabisa, kwenye maslahi mapana ya taifa letu tuweke pembeni ushabiki wa vyama vyetu.
 
Dogo, leo umeendelea vizuri na dose ya dawa ulizopewa Hospitali Ya Milembe. Keep it up, akili zitakaa sawa tu mdogo mdogo.

Na hata kwa wale wana CCM wenzio waliokua hawaelewei ile kauli ya Mama "ALIESIMAMA HAPA NI RAIS", somo ni gumu kidogo ila taratibu wataelewa tu, kama TPA leo walivyoeleweshwa wakaelewa.

Somo linaendelea muda si mrefu, subiri majibu yaletwe kuhusu amri aliopewa CAG kufanya ukaguzi wa hela zote zilizotoka Hazina kuanzia January 2021 - Mpaka mwezi huu. Hapa waliochota hela kwa advantage ya Rais kuumwa na kwa kisingizio cha matumizi ya msiba wa Rais - Wataelewa somo vizuri pia (Iwe kuna Waziri, Naibu Waziri, Katibu, Muweka Hazina au yoyote kama amehusika, basi ataelewa somo).

Mama amecheza karata zake vizuri sana, kama ikitokea kuna Mawaziri au Manaibu Waziri (Hasa waliokua hawamtii kipindi yeye ni Makamo Wa Rais, na waliokua wakidiriki hata kumchongea kwa Rais pindi alipokua akiwahoji na kuwauliza baadhi ya maamuzi wanayofanya) wamehusika kuchota hela katika kipindi hicho cha kuanzia January, basi Mama hatawafumbia macho na anapata sababu ya kulivunja Baraza La Mawaziri For Good.

#Mlimpeleka Askofu Gwajima bungeni mkategemea aende kuichambua "REPORT YA CAG" kweli. Wakati report ya michango ya kanisa lake hajui kuichambua kwa waumini wake.
Huyu jamaa yetu posho imekata
 
Hatutaki siasa tunataka matokeo. Kuanzia miaka 1961.kulikuwa na siasa nyingi hatujawahi kufika popote.
Hii nchi inahitaji utawala wa kigaidi haya masuala ya siasa ni ukinga tu. Kipindi cha mjerumani tulikuwa na miondo mbinu mingi sana kama reli maana unafanya kwa amri ukikataa ni bakora haya mambo ya haki haki cjui nini yanatuchelewesha haya[emoji23][emoji23]
 
Huyu jamaa yetu posho imekata
Hahahaaaa...... Kuna mambo ya kushabikia na kuna mambo ya kusimamia kweli.

Mtu kama Rajab Adadi hana kashfa yoyote tena kaongoza kura za maoni akakatwa na kuwekwa yule mwanaFA kwa sababu tu alipiga show ya Corona!

Sasa wanaletewa ukaguzi wa SGR na bwawa la Nyerere utasikia taarabu zao, bora hata angekuwemo tumbili mwenyewe badala ya mama tumbili!
 
Hahahaaaa...... Kuna mambo ya kushabikia na kuna mambo ya kusimamia kweli.

Mtu kama Rajab Adadi hana kashfa yoyote tena kaongoza kura za maoni akakatwa na kuwekwa yule mwanaFA kwa sababu tu alipiga show ya Corona!

Sasa wanaletewa ukaguzi wa SGR na bwawa la Nyerere utasikia taarabu zao, bora hata angekuwemo tumbili mwenyewe badala ya mama tumbili!
Hizi dawa ulizotumia jana sina wasiwasi nazo kabisa 100%, umerudi upya kabisa na umeanza kuwa mzalendo wa kweli.
 
John acha zako bwana! Ina maana Deo Sanga na hata Msukuma na Lusinde hawawezi? Basi hakuna shida, Mwana FA na Kabula wako fiti na wataichambua kwa msaada wa Mh. Dorothea
Huyo Mwana FA kama alishindwa kuongea tuu kwenye kampeni ndio ataweza kuongea bungeni?
 
Tukiweka itikadi pembeni, kiukweli pale bungeni simuoni mtu mwenye uwezo wa kuichambua ripoti ya CAG kama walivyokuwa Zitto Kabwe, J J Mnyika, James Mbatia na Tundu Lissu.

Kuwa mwanasiasa mzuri ni jambo moja lakini kuwa mwanasiasa " mahiri" ni jambo lingine kabisa.

Hao niliowataja unapofika wakati wa uchambuzi wa maswala ya kitaalamu iwe uchumi, sheria au fedha huwa na udadisi wa kitaaluma siyo kishabiki.

Ripoti ya CAG iliyowasilishwa kwa mh Rais Samia leo inahitaji hoja nyingi za kibobezi/ kidadisi lakini sidhani kama akina Babu Tale na Nusrat Henje wana viwango hivyo.

Itoshe tu kusema wabunge wengi wa sasa wana uwezo mdogo na ujasiri hafifu wa kujenga hoja.
Yupo babu tale na mwanaefuei
 
Unasemaje wewe
IMG_20210316_143951.jpg
 
Alaf Mbona Babu Tale anakua mfano kwenye mambo mengi ya msingi yahusuyo bunge?[emoji23][emoji23][emoji23] Kama jimboni kwake wapo watu wa design yake mlitakaje?[emoji23][emoji23][emoji23]

Anyway This time anaweza toa hoja moja amazing na hamtaamin masikioni mwenu[emoji23][emoji23][emoji23]
Ya kushindwa kufua boxers
 
Back
Top Bottom