Pale dunia inapofumbwa kwa yale yanotokea nchini Sudan

Pale dunia inapofumbwa kwa yale yanotokea nchini Sudan

Misri inasambaza silaha kwa jeshi wakati Urus inawapa silaha rapidly response squad.
I don't know how some qullible people are accusing the US in fact Us inafanya kazi kubwa ya kuziunganisha pande zinazohasimiana.


Bashir katika utawala wake alihisi uenda jeshi likaja kumpindua, akaamua kuunda kikosi(RPS) na kukipa nguvu Sawa na jeshi.

Leo bashar hayupo jeshi limeamua kuita kiongozi wa RPS ili waunde jeshi moja as nchi haiwezi kuwa na majeshi mawili but wameshindwa kukubaliana kwenye mgawanyo wa madaraka ndiyo vita imeibuka.
RPS anasema ni wakati wake wa kuongoza, jeshi nalo linatoa misimamo ile ile.
Sasa sijui habari za fulani walikutana na fulani zinatoka wapi.. Ikiwa insu ni kukutana Putin hajawai kutana na viongozi wa Us?.
SAMIA hakutani na viongozi wa Us? why msudani iwe hoja?
Wakati vita ya Ethiopia inapigana kuna wapumbavu wachambuzi wakawa wanaandika humu kuwa wanapiganishwa na US kwasababu tu wamejenga bwawa la umeme kitu ambacho US hai
halendi.
Yaani bwawa lenye thamani na ndege moja ya F15 moja ndiyo marekani ipate wivu!!
Bure kabisa
Waafrica kilakitu tunasungizia marekani na ulaya.
Ifike kipindi waafrica tuachane na hizi propaganda za kijinga, Kwa kinachoendelea Sudan sioni sababu ya kusingizia nchi za magharibi
 
Mi sijasema uelimishi, mimi nimekutaka u- summerize ulichokikopi uko gugo na kuiweka hapa.
Kunukuu na kuweka hapa bila "acknowledgement" ya chanzo ni "plagiarism".

Mimi huwa nafanya "acknowledgement" ya vyanzo vyangu.

Ndo maana nimeweka chanzo cha uchambuzi wangu.
 
Waafrica kilakitu tunasungizia marekani na ulaya.
Ifike kipindi waafrica tuachane na hizi propaganda za kijinga, Kwa kinachoendelea Sudan sioni sababu ya kusingizia nchi za magharibi
Inachukiza sana. tumewageuza wamarekani kuwa kama miungu vile!! Wao ndiyo wanaamua nani apigane na nani asipigane tena kwa wakati wanaotaka wao.
Hizi nyuzi zinalenga kuebdeleza inferior complex kwa mtu mweusi na kuendelea kuamini kuna taifa ama mtu ndiye anaamua hatima yetu wakati hatima yetu hipo mikononi mwetu sisi wenyewe.

Shida ya Africa kwa ujumla zipo wazi kabisa lakini kuna mtu anajikita kupotosha kwa maksudi kabisa in profitless way.

Wakati wa wale wahuni Amboni na Mukuranga kuna watu (magreat thinker wa Jf) wakawa wanaasema wanafadhiliwa na marekani.. et kwasababu kuna mikataba Tanzania imesain na China hivyo Marekani imeamua kutengeneza waasi Tanzania kupitia Dini.
Watu wanaosemwa kufadhiliwa na US, Maskini wa Mungu!!!! wengine Yebo Yebo zimeisha, kanzu chafu na chakavu na walikuwa wanatembea na viroba vya unga na dagaa silaha zao nyingi ni Mapanga na shoka ila wasomi waa Jf wakawa wanasisitza humu kuwa hao jamaa ni kazi ya Marekani na ukiwapinga unaambiwa ujui chochote kuhusu Geopolitical.
 
US ameweka dunia ktk uzani sawa hasa kudhibiti nchi zenye itikadi ya kiislamu ktk kutawala dunia.

Hizi nchi zingeweza kufanya dunia nzima imainamie wao. Kama mnatamani ulimwengu mzima uwe na itikadi zenu, tafuteni teknolojia mjisafirishe muende huko mwezini mkaishi.
Tende watamuachia nan huku dunian
 
Mataifa kama Russia kama kawaida hayawezi kupenda kuona demokrasia ikishamiri nchini Sudan, wao siku zote wapo kulea utawala wa kiimla kwa maslahi yao.

Ndio maana huyo Jenerali Mohammed Hamdan Dagalo wanayemuunga mkono anataka utawala wa kiraia urejeshwe baada ya miaka 10 ili tu muda wote huo aendelee kukaa madarakani. Kinachomsumbua ni tamaa ya kukaa madarakani.

Hata Muingereza na Marekani hawapendi kuona demokrasia inashamiri Afrika.

yaliyotokea Zanzibar 1964 ni mfano tu wa jinsi Uk ilivyoshiriki kuiondosha serikali iliyochaguliwa kidemokrasia na wananchi pia yaliyotokea Ghana wakati wa Nkrumah namna gani CIA ilivyomwondosha madarakani .
 
Inachukiza sana. tumewageuza wamarekani kuwa kama miungu vile!! Wao ndiyo wanaamua nani apigane na nani asipigane tena kwa wakati wanaotaka wao.
Hizi nyuzi zinalenga kuebdeleza inferior complex kwa mtu mweusi na kuendelea kuamini kuna taifa ama mtu ndiye anaamua hatima yetu wakati hatima yetu hipo mikononi mwetu sisi wenyewe.

Shida ya Africa kwa ujumla zipo wazi kabisa lakini kuna mtu anajikita kupotosha kwa maksudi kabisa in profitless way.

Wakati wa wale wahuni Amboni na Mukuranga kuna watu (magreat thinker wa Jf) wakawa wanaasema wanafadhiliwa na marekani.. et kwasababu kuna mikataba Tanzania imesain na China hivyo Marekani imeamua kutengeneza waasi Tanzania kupitia Dini.
Watu wanaosemwa kufadhiliwa na US, Maskini wa Mungu!!!! wengine Yebo Yebo zimeisha, kanzu chafu na chakavu na walikuwa wanatembea na viroba vya unga na dagaa silaha zao nyingi ni Mapanga na shoka ila wasomi waa Jf wakawa wanasisitza humu kuwa hao jamaa ni kazi ya Marekani na ukiwapinga unaambiwa ujui chochote kuhusu Geopolitical.
Yapo maneno mengi ambayo hutumika panapokuwa na migogoro inohusika wakubwa wa dunia maneno kama- "Geopolitics", "Hegemony", "Imperialism", Unipolar, Multipolar, Warmongering, Military Aggression, Proxy War, Nuclear Armageddon, Imperialist Powers, Strategic Autonomy, Vassalisation, Great Reset, New World Order, Deep States, Remilitarization,

Haya ni baadhi tu ya maneno ambayo katika diplomasia ya kimataifa ni lazima uyatumie.

Ila elewa Sudani ni moja ya nchi za Afrika ambazo zimegeuzwa kuwa uwanja wa vita vya miamba ya dunia kugombania rasilimali.

Kwa mfano, "Hegemony" ni kuongeza wigo wa eneo la kujidai kwa kutumia njia na mbinu za kijeshi kuingia katika ardhi ya nchi ingine.

Soma vitabu viwili vinoelezea "geopilitics" walivoandika wazee Henry Kissinger na Zbigniew Brzezinski vya Diplomacy na kitabu kingine cha "The Grand Chessboard"- "American Primacy and its Geostrategic Imperatives".

Hawa wazee wameeleza ni kwanini hata baada ya kuanguka kwa USSR sera ya Marekani ya kuhakikisha kujipanua au Expansionism yahakikisha Russia haiwi tishio kwake.
 
HiI vita ya uchumi haijawahi muacha mwafrica salama. ..Somalia-gas,mafuta...DR Congo.-madini,Chad, Niger,Sudan,libya-hill zone linautajiri mkubwa sn wa madini,mafuta and gas ambayo wamagharibi wanayahitaji sn...mnavurugwa wao wanabeba Mali. ..Libya wamefibeba wapendavyo,Somalia ndio shamba Lao kabisa...Congo jamaa wanabeba kwenda ubelgiji. ..hata vita ya Ukraine ni malighafi zilizopo mlendio wanazozitaka
 
Hakuna watu walokosa akili, vichwa vitupu kama Afrika hasa wenye itikadi za kiislamu.

Shida yoyote ambayo ipo, hawana jibu lingine zaidi ya US. Kila kitu kwao ni US, ni wapuuzi sana.

Yaliyopo Congo na yaliyotokea kwa Patric Lumumba hivi wale ni waislamu ?? Soma history ya CIA na Africa ndio utaelewa , labda una chuki zako za kibinafsi kuhusu waislamu.
 
Mpaka sasa nchi za Misri, Saudi Arabia, Iran, Syria, Ukraine, Hispania, Italia, Ujerumani, Uingereza, Ufaransa, Marekani na zingine, zimetuma ndege za kijeshi na wanajeshi maalum kufanya shughuli za uokoaji wa raia wake. Djibouti ndo pamekuwa kituo cha kufikia wageni mbalimbali kabla kusafirishwa kwenda nchi zingine.


SASA UKRAIN INAWAPELEKA WAPI RAIA WAO!? [emoji23] [emoji23]
 
"
Mgogoro na vita baina ya Jeshi la Sudan na wanamgambo wa RSF umeingia siku ya 10 huku kukiwepo na amri ya kusimamishwa mapigano kwa masaa 72.

Amri ya kusimamisha mapigano kuruhusu uokozi wa raia wa kigeni ilianza kutokea siku ya Ijumaa iliyopita ambapo watu waliruhuswa kusheherekea sikuku ya Iddi. Lakini baadae Jumapili mapigano yakaendelea tena. Juzi kati jeshi la wanamgambo hao wa RSF wakakubali maombi ya mataifa ya kigeni kufanya uokozi wa raia wake.

Mpaka sasa nchi za Misri, Saudi Arabia, Iran, Syria, Ukraine, Hispania, Italia, Ujerumani, Uingereza, Ufaransa, Marekani na zingine, zimetuma ndege za kijeshi na wanajeshi maalum kufanya shughuli za uokoaji wa raia wake. Djibouti ndo pamekuwa kituo cha kufikia wageni mbalimbali kabla kusafirishwa kwenda nchi zingine.

Watu wapatao 27,000 raia wa Sudan tayari wamekimbilia nchi jirani za Mali, Chad na Misri kwa njia ya barabara ambapo magari na mabasi yamekuwa yakibeba watu kupeleka katika nchi hizo na kuwa wakimbizi. Shirika la UNHCR ambalo lina kambi nchini Chad limekuwa likiendelea kupokea wakimbizi hao ambao idadi yao huenda ikaongezeka na kuzidi 100,000.

Uingereza ambayo imekuwa nyuma ya juhudi za uokozi wa raia wake, leo imenza rasmi zoezi hilo kwa kuwaelekeza raia wake kwenda katika kituo cha kijeshi cha Weid Seidna kilichopo kakazini mwa mji mkuu wa Khartoum. Uingereza imetuma kikosi cha jeshi lake la Raf kutokea kwenye kambi yake ya kijeshi iliyopo nchini Cyprus iitwayo Akrotiri.

Lakini serikali ya Uingereza imesisitiza kuwa ni raia wenye kubeba pasi za kusafiria za nchi hiyo na familia zao tu ndo watoruhusiwa kupanda ndege hizo kuokolewa na si raia wengine ambao ni wakazi wa namna yoyote ile nchini Uingereza kwa mujibu wa serikali ya Uingereza raia wapatao 1,000 tayari walikuwa wamewasiliana na wizara ya mambo ya nje ya nchi hiyo.

Ujerumani imetuma ndege sita za uokozi na kuokoa raia wapatao 500, Italia raia 400, Ukraine raia 138, Marekani zaidi ya raia 3000, India 3000, na raia wengine wametumia bandari ya Sudan au Port Sudani kuvuka kwa meli kwenda nchi za Yemen na Saudi Arabia.

Lakini mapigano hayo yakiwa yaendelea khasa katikati ya Khartoum, tayari kuna taarifa za kutekwa kwa maabara ya taifa ambayo imehifadhi sampuli na dawa za chanjo za magonjwa mbalimbali kama malaria na kipindupindu. Pia kuna taarifa za kuwepo kwa watoto wadogo wabebao silaha aina za AK 47 (watoto wa vita ) au Child Soldiers ambao wamekuwa wakiranda mitaani kutafuta chakula na kuanza kupora katika maduka, majengo na majumbaya watu khasa wale raia wa kigeni wanokimbia.

Watoto hawa ambao wana umri kati ya miaka 13 na 14 ni watoto hatari sana ambao wanapigana upande wa vikosi vya RSF. Kwa kawaida jeshi huwa na komandi moja ambayo hutoa amri wakti vita iikiendelea na hivyo kuwepo nidhamu baina ya wanajeshi. Kwa upande wa wapiganaji wa RSF hali ni tofauti kwani kila mpiganaji ana maamuzi yake na anachokikuta mbele yake huwa na halali kwake na hali hiyo ndo ilopelekea nchi nyingi kutuma vikosi vya jeshi kusaidia uokozi maana tayari kuna taarifa ya kushambuliwa kwa vikosi vy uokoaji.

Lakini yote haya yameanzaje na nini ni chanzo na pengine mwisho wake utakuwaje?

Mazingira khasa ya kuibuka kwa mapagano yaelezwa tofauti na vyombo vingi vya habari vikisema kuwa ni mvutano baina ya majenerali wawili Abdel Fattah-al Burhan na Dagalo au kama alijulikanavyo kama Hemedti. Taarifa zingine zadai kuwa majenerali Al Burhan na Dagalo ni majasusi wa nchi za magharibi na Russia. Zipo taarifa kadha wa kadha kuhusu majenerali hawa na ziara zao nchini Marekani na kule Kremlin.

Jenerali Al Burhan amekuwa akifanya ziara nyingi jijini Washington na ipo ziara ambayo alikutana na waziri wa nchi wa Marekani bwana Pompei mwaka 2020 na waziri wa ujasusi wa Israeli Eli Cohen mwaka 2022.

Lakini kinotokea sasa nchini humo ni kugombania madaraka au "power struggle" ambapo kila upande unashutumu mwenzie kutaka kupindua. Kwa muda mrefu tangia wanamgambo wa RSF ambao kiini chake ni wagamgambo wa Janjaweed washirikiane na jeshi kuongoza Sudan, bado uhusiano baina ya majenerali Burhan na Dagalo umekuwa ni wa kutiliana mashaka.

Jenerali Dagalo atokea Sudan ya Kusini ambayo ilipata uhuru wake mwaka 2011 baada ya mapigano ya muda mrefu kati ya wapiganaji wa SPLA/M na majeshi ya serikali ya Khartoum. Sudan ilitawaliwa na Uingereza na katika utawala wake Uingereza iliigawa Sudan katika maeneo mawili ya Kaskazini kwenye waarabu ambako walijenga mashule, mahospitali na miundombinu mingine kama barabara , madaraja na huduma zingine za msingi kama makanisa na misikiti.

Lakini wakoloni hao wa Uingereza walisahau kabisa Sudan ya Kusini ambayo ina waafrika weusi na kuiacha kama ilivyo huku miji yake mikubwa ya Juba na Darfur ikiwa ndani ya vumbi la jangwa. Hali hiyo ilifanya Sudan Kusini kuendesha kampeni ya vita na serikali ya Khartoum ambayo iliendelea kuwaadhibu wasudani weusi na baadae kuwapelekea kundi la Janjaweed ili kumaliza tatizo la wahamiaji waloitwa haramu ambao walikuwa wakitafuta maisha bira kutoka kaskazini.

Tangu ipate uhuru mwaka 2011 na kujiunga na umoja wa Afrika kuwa nchi ya 54 barani humo, Sudan ya Kusini ni nchi huru na inojitegemea. Sudan ya Kusini ina majimbo 10 ambayo wananchi wake wamekuwa kila mara walipigana kwa kuona hakuna maendeleo ya haraka yanofanywa na serikali ya Sudan ya Kusini.

Lakini ni kitendo cha jenerali Burhan kukubali kuwaleta Khartoum wanamgambo wa RSF kusaidia shughuli mbalimbali za kijeshi na pia kuanza mazungumzo ya kuwarasimisha wanamgambo hao wa RSF kuwa sehemu ya jeshi la Sudan ndicho kilicholeta zogo na vurugu na sasa mapigano makali.

Lakini wadadisi na wachambuzi wengi wanaamini kuwa mapigano ya sasa kati ya majenerali hao wawili Burhan na Dagalo yametokana na majenerali hao (Jenerali Burhan) kuunga mkono nchi za Marekani na NATO ambazo bado zasaidia nchi ya Ukraine ambayo iko kwenye vita na Russia, na Jenerali Dagalo kuwa upande wa Russia ambayo ina vikosi vyake Sudan ya Kusini.

Al Burhani pia asaidiwa na Misri kwa misaada ya vifaa vya kijeshi kutoka kwa raisi Abdel Fattah El- Sisi. Jenerali Dagalo ambae ni tajiri mkubwa wa dhahbu kutoka Sudan ya Kusini anasaidiwa pia na nchi za Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu UAE ambako amewahi kupeleka vikosi vya RSF kusaidia vita vya Yemen.

Kiasi kikubwa cha dhahabu inochimbwa Sudan ya Kusini yapelekwa nchini Russia kupitia UAE na vikosi vya jeshi la kukodi la Wagner vya Russia vipo Sudani Kusini vikilinda migodi ya dhahabu na visima vya mafuta. Russia imekuwa katika mazungumzo na jenerali Dagalo kuhusu kutaka kujenga kituo cha kijeshi katika bandari ya Sudan au Port Sudani kwenye bahari nyekundu.

Itakumbukwa baada ya Russia kuanzisha operesheni maalum ya kijeshi nchini Ukraine umoja wa mataifa uliweka azimio la kulaumu kitendo hicho cha Russia lakini Sudan haikushiriki kupiga kura kuunga mkono azimio hilo. Tangu wakati huo Marekani na washirika wake wamekuwa wakihangaka kuhaikisha Sudani inapata shida kwanza kwa kuondoa misaada ya fedha kutoka IMF na Benki ya Dunia, kuharibu mahusiano ya Sudan na Iran ambayo yaiuzia Sudan vifaa vya kijeshi, Russia na China.

Pia Marekani yaitaka Sudan kufunga mazungumzo na mijadala ya Russia kuweka kituo cha jeshi la majini kwenye bandari ya Sudan, kuimarisha uhasama na Iran na kuharibu uhusiano wa kijeshi kati ya Sudan na Iran na Russia na kuchagiza machakato wa kurudisha serikali ya kiraia chini ya waziri mkuu Abdallah Hamdok ambayo itapunguza usafirishaji wa dhahabu kwenda Russia ambapo yaaminika jambo hilo laisaidia sana Russia kukwepa vikwazo vya kiuchumi vilowekwa na Marekani na washirika wake.

Marekani imekuwa yaishutumu Russia kuwa nyuma ya mapinduzi yalomwondoa madarakani bwana Hamdok ambae kitaaluma ni mchumi na amesoma nchini Uingereza.

Mgogoro wa sasa zaidi umechochewa na majenerali hao wawili Burhan na Dagalo kutokukubaliana kwenye suala la kugawana madaraka na kwa vikosi vya RSF kuingizwa rasmi kwenye jeshi la Sudan. Jenerali Burhan binafsi hakubalini na suala hili lakini baadhi ya wanajeshi ndani ya jeshi wanaamini kuwa kuwaingiza RSF ndani ya jeshi kutapunguza na kuondoa hasira ya vijana wa RSF na pia maandamano yasokwisha mitaani kutoka kwa wananchi ambao wengi hawaungi mkono suala la RSF kuingizwa jeshini.

Jenerali Dagalo hakubaliani na suala la vikosi vya RSF kuingizwa jeshini hadi hapo serikali ya kiraia itapokuwa madarakani na pia anadai kuondolewa kwenye nafasi za kuu za serikali kwa wale viongozi wote wenye ukaribu na aliekuwa raisi Al Bashir ambae alipinduliwa mwaka 2019. Msimamo huu umemfanya jenerali dagalo kuungwa mkono na watu wengi wakiwemo wasomi vikundi mbalimbali vya kijamii ambavyo vimekuwemo katika mazungumzo ya kurudisha serikali ya ya kiraia.

Jumuiya ya kimataifa imekuwa ikionyesha wasiwasi wa kuwaingiza RSF jeshini na imekuwa ikisisitiza kuharakisha harakati za kuirudisha serikali ya kiraia chini ya Hamdok ambayo majenerali Burhan na Dagalo nao wana wasiwasi wa kukamatawa na kuwekwa jela kwa makosa mbalimbali ya uhalifu wa kivita.

Hadi sasa hakuna anaefahamu mgogoro huu utaisha vipi khasa baada ya jenerali Dagalo na vikosi vyake kuahidi kuendeleza mapigano. Hii ni aina ingine ya mifano hai kuwa bara la Afrika kwa sasa lipo katika kugombaniwa na mataifa makubwa. Sudan ya Kusini ina asilimia 75 ya utajiri wa maliasili ya visima vya mafuta, pia Sudan kaskazini ina dhahabu pamoja na madini mengine mbalimbali.

Hakika yanotokea Sudan yatupa funzo kubwa sana sisi waafrika na mstakabali wetu hapa duniani maana waafrika wenye ngozi nyeusi wamekalia maliasili yenye thamani ya mamilioni ya dola lakini ni raia kutoka nchi zingine ambao ndo wenye uwezo wa kuamua hatima ya mwafrika mweusi.
"

SANA UKRAINE INAWAPELEKA WAPI RAIA WAO [emoji23] [emoji23]
 
Waafrica kilakitu tunasungizia marekani na ulaya.
Ifike kipindi waafrica tuachane na hizi propaganda za kijinga, Kwa kinachoendelea Sudan sioni sababu ya kusingizia nchi za magharibi
Kama Afrika imetawaliwa na mataifa ya magharibi basi bara hili haliwezi kujikomboa kamwe.

Litazushiwa zogo na kila dhahama kutoka nje.

Sababu moja kubwa ni kwamba tuna hazina kubwa ya rasilimali na hao wa nje hawana.

Waliiba wakati wa ukoloni na imeisha wamepagawa.

Waafrika bado hatujajitambua tu maskini, na leo hii haohao wa nje hawatutaki huko kwao ukienda huko kama mkimbizi watakupeleka Rwanda.

Na hata hii operesheni inoendelea ya uokozi ni kwa wale raia wenye pasi za kusafiria za nchi husika kama Marekani, Uingereza, Ujerumani Italy ndo wanoruhusiwa kupanda ndege na kama una viza ya kawaida kama ya kudumu basi hiyo imekula kwako.

Waafrika tuamke usingizi mzito na mtamu lakini wenye madhara makubwa huko mbele.
 
Mpaka sasa nchi za Misri, Saudi Arabia, Iran, Syria, Ukraine, Hispania, Italia, Ujerumani, Uingereza, Ufaransa, Marekani na zingine, zimetuma ndege za kijeshi na wanajeshi maalum kufanya shughuli za uokoaji wa raia wake. Djibouti ndo pamekuwa kituo cha kufikia wageni mbalimbali kabla kusafirishwa kwenda nchi zingine.


SASA UKRAIN INAWAPELEKA WAPI RAIA WAO!? [emoji23] [emoji23]
Ukraine imeokoa raia wake ambao wengi ni wataalam wa masuala ya anga na marubani pamoja na mafundi na imewapeleka Misri.
 
  • Thanks
Reactions: B51
Mkuu Richard umeandika bandiko refu mno na kuweka mambo mengi sana kiasi cha kuhatarisha kueleweka kwa dhumuni (objective) ya mada na michango unayoitarajia toka kwa wasomaji. Usishangae kuona kila mchangiaji akisema chake bila kueleweka kama anakuunga mkono au anakupinga.

Mimi nimeona umeitaja Darfur kama sehemu ya South Sudan. Sijui kwa maana ipi hasa. Navyojua hii ni sehemu ya Sudan (Western Sudan) inayokaliwa na watu weusi ambao predominantly ni Waislamu. Na ndiko migodi ya dhahabu inayodhibitiwa na Hemedti na Urusi (Wagner forces) iliko. South Sudan inatamba zaidi na visima vya mafuta.
 
Inachukiza sana. tumewageuza wamarekani kuwa kama miungu vile!! Wao ndiyo wanaamua nani apigane na nani asipigane tena kwa wakati wanaotaka wao.
Hizi nyuzi zinalenga kuebdeleza inferior complex kwa mtu mweusi na kuendelea kuamini kuna taifa ama mtu ndiye anaamua hatima yetu wakati hatima yetu hipo mikononi mwetu sisi wenyewe.

Shida ya Africa kwa ujumla zipo wazi kabisa lakini kuna mtu anajikita kupotosha kwa maksudi kabisa in profitless way.

Wakati wa wale wahuni Amboni na Mukuranga kuna watu (magreat thinker wa Jf) wakawa wanaasema wanafadhiliwa na marekani.. et kwasababu kuna mikataba Tanzania imesain na China hivyo Marekani imeamua kutengeneza waasi Tanzania kupitia Dini.
Watu wanaosemwa kufadhiliwa na US, Maskini wa Mungu!!!! wengine Yebo Yebo zimeisha, kanzu chafu na chakavu na walikuwa wanatembea na viroba vya unga na dagaa silaha zao nyingi ni Mapanga na shoka ila wasomi waa Jf wakawa wanasisitza humu kuwa hao jamaa ni kazi ya Marekani na ukiwapinga unaambiwa ujui chochote kuhusu Geopolitical.

 
  • Thanks
Reactions: B51
Mkuu Richard umeandika bandiko refu mno na kuweka mambo mengi sana kiasi cha kuhatarisha kueleweka kwa dhumuni (objective) ya mada na michango unayoitarajia toka kwa wasomaji. Usishangae kuona kila mchangiaji akisema chake bila kueleweka kama anakuunga mkono au anakupinga.

Mimi nimeona umeitaja Darfur kama sehemu ya South Sudan. Sijui kwa maana ipi hasa. Navyojua hii ni sehemu ya Sudan (Western Sudan) inayokaliwa na watu weusi ambao predominantly ni Waislamu. Na ndiko migodi ya dhahabu inayodhibitiwa na Hemedti na Urusi (Wagner forces) iliko. South Sudan inatamba zaidi na visima vya mafuta.
Nililenga kutaja Juba, ila nikaongeza Darfur kama sehemu iloathirika na vita vya wasudani weusi na majeshi ya Khartoum.

Ila ni kweli Darfur ipo magharibi kama jimbo linojitegemea na ndiko anakotokea Jenerali Dagalo.

Lengo la mada yangu ni kuonyesha kwamba pamoja na kwamba Sudan pamekuwepo vita kwa miaka mingi, vita hivyo vimechangiwa na mataifa ya nje ambayo yana kambi tofauti, kambi ya Dagalo, kambi ya Burhan na kambi ya Hamdok.

Na kihistoria nikasema Sudan lilikuwa ni koloni la Uingereza na upande wa Khartoum ndo ulopendelewa kwa kila kitu, huku upande wa kusini ambao ndo wenye rasilimali ukiwa hauna chochote ila ndo wenye rasilimali.

Lakini leo hii, dunia imefumbwa kwa kuambiwa na kuaminishwa kwamba vita vya safari hii baina ya jeshi na RSF ionekane imetengenezwa au kuanzishwa na wasudani wenyewe lakini ukweli halisi ni kuwepo kwa mashinikizo kutoka nje.

Kumbuka safari hii hakuna raia mitaani wanopigana bali ni wanajeshi na wanamgambo, raisi wote wamejifungia ndani.
 
Kama Afrika imetawaliwa na mataifa ya magharibi basi bara hili haliwezi kujikomboa kamwe.

Litazushiwa zogo na kila dhahama kutoka nje.

Sababu moja kubwa ni kwamba tuna hazina kubwa ya rasilimali na hao wa nje hawana.

Waliiba wakati wa ukoloni na imeisha wamepagawa.

Waafrika bado hatujajitambua tu maskini, na leo hii haohao wa nje hawatutaki huko kwao ukienda huko kama mkimbizi watakupeleka Rwanda.

Na hata hii operesheni inoendelea ya uokozi ni kwa wale raia wenye pasi za kusafiria za nchi husika kama Marekani, Uingereza, Ujerumani Italy ndo wanoruhusiwa kupanda ndege na kama una viza ya kawaida kama ya kudumu basi hiyo imekula kwako.

Waafrika tuamke usingizi mzito na mtamu lakini wenye madhara makubwa huko mbele.
Ndugu yangu jihadhari na hizi hoja nyepesi nyepesi. Matatizo ya Waafrika chanzo kikuu ni sisi wenyewe.

Mfano. Tumeipigania Sudani ya Kusini ijitenge ikafanikiwa. Mara viongozi wakawahi kuanza kutengeneza madili/mikataba ya kifisadi na mafia wa kimataifa ili wajichotee mafuta na rasilimali za nchi na kuwafungulia akaunti Uswisi. Mara wakaanzisha vita ya wenyewe kwa wenyewe silaha zikitoka huko huko nje kwa mafisadi washirika! What is this?

Afrika ya Kusini ilikuwa hivyo hivyo baada ya Mandela kustaafu.

Unaweza kuamini kuwa maRais wa kiafrika walioko madarakani na waliostaafu wanakuwa na utajiri unaowazidi kwa mbali maRais wa taifa kubwa kama Marekani na wale wa Ulaya. Halafu bila aibu wanaweka hela zao huko huko Marekani na Ulaya?

Sisi ni watoto kwamba tuwe tunarubuniwa na kulazimishwa kila wakati baada ya zaidi ya miaka 60 ya uhuru? Hatukui wala kukomaa? Hatuelimiki? Hatujijengei ujasiri? Basi hatuna haja ya kuwepo duniani!
 
Ndugu yangu jihadhari na hizi hoja nyepesi nyepesi. Matatizo ya Waafrika chanzo kikuu ni sisi wenyewe.

Mfano. Tumeipigania Sudani ya Kusini ijitenge ikafanikiwa. Mara viongozi wakawahi kuanza kutengeneza madili/mikataba ya kifisadi na mafia wa kimataifa ili wajichotee mafuta na rasilimali za nchi na kuwafungulia akaunti Uswisi. Mara wakaanzisha vita ya wenyewe kwa wenyewe silaha zikitoka huko huko nje kwa mafisadi washirika! What is this?

Afrika ya Kusini ilikuwa hivyo hivyo baada ya Mandela kustaafu.

Unaweza kuamini kuwa maRais wa kiafrika walioko madarakani na waliostaafu wanakuwa na utajiri unaowazidi kwa mbali maRais wa taifa kubwa kama Marekani na wale wa Ulaya. Halafu bila aibu wanaweka hela zao huko huko Marekani na Ulaya?

Sisi ni watoto kwamba tuwe tunarubuniwa na kulazimishwa kila wakati baada ya zaidi ya miaka 60 ya uhuru? Hatukui wala kukomaa? Hatuelimiki? Hatujijengei ujasiri? Basi hatuna haja ya kuwepo duniani!
Umaskini wachangia sana ndo maana mtu akipat amadaraka yeye awaza kuiba tu kwanza kabla ya mambo mengine.

Sisi waafrika ni "vulnerable" na ni rahisi sana kurubuniwa kama haujitambui.
 
Back
Top Bottom